Mteja wa nondo bei nzuri

Mteja wa nondo bei nzuri

Habari wadau

Ninahitaji mteja wa uhakika wa mzigo wa nondo au saruji wa haraka kwa bei nzuri kidogo, nipo Dar, kuna mzigo umenunuliwa kimakosa unatakiwa kutoka upesi

Njoo nipe specifications za mzigo unaoutaka tufanye biashara haraka.
Wewe ndio unatakiwa uweke specifications za mzigo ulionao, kama ni nondo, ni za 8mm 12mm au 16mm? Cement nayo ni aina ipi?
 
Hakawihi kukuambia njoo inbox.
Nadhani wengi wanachangamoto ya biashara na kujua biashara inahitaji nini.
Hapo hata wewe sio mfanya biashara lakini mzigo umenunuliwa kimakosa na wewe unahitaji kuutoa hiyo unayoifanya hapo ni biadhara tayari.
 
Weka bei? Na mahali ulipo
Watu kwa kupenda mteremko hawajambo.
Hizo nondo sijui cement vyote ni vya mchongo...kapiga kwenye magodown ya mchina
Ukinununua tu ni kama umeweka mguu mmoja segadence.
umenunuliwa kimakosa
OGOPA MATAPELI😀😀😀.
umenunuliwa kimakosa rudisha dukani utarudishiwa Hela zako.japo unaweza kupungua
Mzigo uliouzwa tayari means specs zake zinatambulika na ni limited.

Muuzaji ndiye anaweka specs!!
Tulilipa kamaka pesa lakini hawakutupa mzigo, na hawawezi kurudisha pesa cash Kwahiyo tunahitaji mtu yeyote mwenye interest ya kununua chochote kinachouzwa kamaka chenye thamani ya million 11 lakini tutampa price favor kidogo ili kumvutia
 
Tulilipa kamaka pesa lakini hawakutupa mzigo, na hawawezi kurudisha pesa cash Kwahiyo tunahitaji mtu yeyote mwenye interest ya kununua chochote kinachouzwa kamaka chenye thamani ya million 11 lakini tutampa price favor kidogo ili kumvutia
Haya maelezo yana ukakasi
 
Naomba specifications za mzigo wowote unaoutaka unaouzwa kamaka wenye thamani ya million 11
Sasa haya maelezo ungeweka kule juu ili kupunguza haya maswali yasiyo na ulazima.

Hapo inamaana akitokea mteja anataka nondo za 11M au bati za 11M biashara inaishia hapo?

Hiyo Kamaka ungewaambia maseneta iko wapi ili wakipiga na gharama za usafirishaji, iwe wamenufaika kwa kununua kwako.

Pole sana, kiufupi una mini hardware mkuu.
 
You might be right pia, ilimradi nikupe cement ya 13k kwa 11k halali kwani kuna tatizo gani mkuu? Njoo haraka kama upo interested hii ni offer
Yaani nifike Kamaka halafu ninunue mzigo kwa dalali? Hiyo itakuwa akili ya wapi?
 
Back
Top Bottom