tatizo lenu hamsomi, mnakurupuka tu kuchangia.
mtei alipunguza mshahara kwa kuona aibu atamzidi nyerere na sio kuwaonea huruma wananchi
nyerere hata asingelipwa hana cha kupoteza maana kila kitu alichohitaji ilikuwa juu ya kodi zetu
mtei alipunguza mshahara kwa kuona aibu atamzidi nyerere na sio kuwaonea huruma wananchi
nyerere hata asingelipwa hana cha kupoteza maana kila kitu alichohitaji ilikuwa juu ya kodi zetu
Big up jembe letu la moshi mtei
jembe la Arusha na Meru
Mzee umechoka pumzika, Maelezo yako yanadhihirisha ulivyo na hata Chama chako pia. Bila aibu unawaambia watz Kuwa ulipunguza mshahara wako kwa Kuwa Mwalimu Nyerere alipunguza wa kwake na kwa kuona Kuwa usingefanya hivyo mshahara wako ungekuwa mkubwa kuliko was Mwalimu, kumbe hukusukumwa na uzalendo wala huruma kwa wananchi wa kipato cha chini, una tofauti gani na wale waliopunguziwa kwa nguvu? Huu ni unafiki usiovumilika kusikika masikioni. Eti Huyu ndio mwasisi wa Chama mbadala! Tumekusikia Mzee hatutafanya makosa kamwe.
Uwe unasoma na kuelewa kabla Ya kupost, Mshahara wake ulikuepo kisheria na sheria ilikua inamlinda asiguswe na mamlaka yoyote ile juu mshahara wake. Hivyo uamuzi wa kupunguza kipato chake ilikua ni heshima kwa mkuu wake na kwa wananchi.
Je, kwenye CCM Ya sasa nani anaweza kupunguza mshahara wake kwa hiyari achilia mbali kwa lazima.?
Huyo mzee hakutaka kabisa kutumikia wa-Tz, hakushiriki kabisa hata kutafuta uhuru japo tayari alikuwa ana kaelimu kake. Na hata kuja kufanya kazi Tz ilikuwa ni kwa masharti ya kulipwa pesa nyingi sana. Hana hata chembe ya uzalendo.
Jamani lini tutaacha ushabiki? Wakati mwingine tutumie akili ya kawaida kubishana wakati aliyoyasema Mtei ni mambo ya msingi na hayagusi vyama kabisa. Yana akisi utaifa mbele na si vinginevyo.
Kuhusu Nyerere hata asipochukua mshahara alikuwa na shida ipi? Jamani! Kama rais hana shida kwa vile anapewa kila kwa nini wanalipwa mshahara wa zaidi ya mil.30?