MTEI: Nililipwa Mshahara sawa na Nyerere

MTEI: Nililipwa Mshahara sawa na Nyerere

Uelewa wako unatia shaka. Mzee mtei anamlinganisha Nyerere katika nafasi yake na maraisi wengine wa siku hizi katika nafasi ile ile. Kama Nyerere hakuwa na shida ni vivyo hivyo kwa Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na Jakaya. Hata hawa wasipochukuwa mishahara yao haina tofauti na Marehemu Nyerere asingalichukua. Sasa kama vile haitoshi hawa viongozi wa sasa sio hawapunguzi mishahara kwa kuwahurumia masikini bali pia huwaibia zaidi masikini na kujilimbikizia wao wenyewe na jamaa zao. Inashangaza kama huelewi mantiki ya Mzee Mtei, basi una safari ndefu sana kuweza kuchambua mambo. Mtei hamlinganishi Marehemu Nyerere na mtu kama wewe anamlinganisha na viongozi walioshika au kupata kushika nafasi kama yake. Upo hapo? Ua umejianda kutetea tu jambo lolote ili mradi uonekane umechangia? Hivi kweli unaweza kulinganisha uadilifu wa Marehemu Nyerere na kiongozi yupi wa sasa Tanzania ya leo? Mtei ingawaje haikuwa dhamira yake kupunguza mshahara wake lakini kwa kuona Boss wake amepunguza alipunguza pia mshahara wake, ina maana Mzee Mtei aliona aibu Boss wake apunguze halafu yeye apate zaidi ya Boss wake. Angalao Mtei aliona aibu, viongozi wa sasa hata HAYA hawana.
Ujinga mwingine unatisha sana,

Hivi Nyerere hata asipochukuwa mshahara alikuwa anashida ipi, nyumba bure, kula bure, kulala bure, na huku anazidi kuiangamiza Tanzania kuwa nchi masikini ya mwisho duniani.

Mtei asitafute umaarufu wa Kisiasa kwa kupitia jina la Nyerere, yeye kwanini aliachia/aliachishwa uwaziri? aeleze ukweli.
 
Kusema FAIZA FOXY amsamehe Nyerere ni matusi usirudie tena.
Tatizo sio hoja yako mrembo faiza tatizo ni chuki yako kwa Nyerere anyway sijui ni nini alichowafanyia wazazi wako maana wewe ni mtoto na utakua umesimuliwa tu na kujenga chuki. Yote kwa yote kua na moyo wa kusamehe. Sahahu yaliyopita tugange yaliyopo na yajayo. Makosa aliyofanya Nyerere wakati huo Tuyaache tufanye yetu mazuri kwa sasa. Muda bado upo
 
Uelewa wako unatia shaka. Mzee mtei anamlinganisha Nyerere katika nafasi yake na maraisi wengine wa siku hizi katika nafasi ile ile. Kama Nyerere hakuwa na shida ni vivyo hivyo kwa Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na Jakaya. Hata hawa wasipochukuwa mishahara yao haina tofauti na Marehemu Nyerere asingalichukua. Sasa kama vile haitoshi hawa viongozi wa sasa sio hawapunguzi mishahara kwa kuwahurumia masikini bali pia huwaibia zaidi masikini na kujilimbikizia wao wenyewe na jamaa zao. Inashangaza kama huelewi mantiki ya Mzee Mtei, basi una safari ndefu sana kuweza kuchambua mambo. Mtei hamlinganishi Marehemu Nyerere na mtu kama wewe anamlinganisha na viongozi walioshika au kupata kushika nafasi kama yake. Upo hapo? Ua umejianda kutetea tu jambo lolote ili mradi uonekane umechangia? Hivi kweli unaweza kulinganisha uadilifu wa Marehemu Nyerere na kiongozi yupi wa sasa Tanzania ya leo? Mtei ingawaje haikuwa dhamira yake kupunguza mshahara wake lakini kwa kuona Boss wake amepunguza alipunguza pia mshahara wake, ina maana Mzee Mtei aliona aibu Boss wake apunguze halafu yeye apate zaidi ya Boss wake. Angalao Mtei aliona aibu, viongozi wa sasa hata HAYA hawana.

Huo ni upunguani wa hali ya juu, uwe wa miaka 100 iliyopita uwe wa leo, Rais ni Rais tu.

Kuna tofauti ipi ikiwa katiba na kanuni ya kuuendesha tasisi ya Urais ni hiyo hiyo au uliibadili wewe?

Huu ujinga mtauwacha lini Watanzania? hivi mshahara wa Nyerere au wa Kikwete unamsaidia nini Mtanzania? kuna Watanzania kibao wana mishahara mikubwa na kipato kikubwa kuliko Rais x 1000.

Mbona mnakuwa wajinga kiasi hiki?
 
FaizaFoxy kwani JK anapolipwa Milion 32 kwa mwezi hapati nyumba bure?Hapati chakula bure?Hapati matibabu bure?Hapati huduma zote bure?

Mpe Nyerere sifa zake!Sikubaliani na baadhi ya maamuzi ya Nyerere alipokuwa madarakani(hasa Azimio la Arusha)lkn kwenye uadilifu aliwashinda tena kwa mbali ma Rais wote waliokuja hasa Kikwete ambaye sio MWADILIFU kwenye pesa za UMMA!

Nyerere asingekubali kujitengea Bilion 50 za safari zake(JK kajitengea) huku bohari ya madawa kwa TZ nzima ikipewa Bilion 48 tu

Sifa ipi? uadilifu upi? kudhulumu watu mali na roho zao ndio uadilifu?

Unajuwa ni wangapi waliokufa kwenye hayo maamuzi ya "Azimio la Arusha" ambayo hukubalini nayo? hata idadi hawajulikani, watu walihamishwa vijiji vyao vya asili na kupelekwa kutupwa maporini, waliokufa kwa magonjwa haya, waliokufa kwa kuliwa na wanyama haya, waliokufa kwa kugongwa na nyoka haya.

Huo ndio uadilifu?
 
Hawa mafisadi!!! Thubutu!!! Mishahara yao mikubwa sana na haikatwi kodi na bado haiwatoshi hivyo wanaamua kufanya ufisadi wa matrilioni mwaka nenda mwaka rudi kisha kwenda kuzificha nchi za nje. Maslahi ya Tanzania na Watanzania hawa mafisadi hawayajali kabisa wanachojali ni matumbo yao.

Tuanze na ruzuku ya chadema inayoishia makao makuu vp mgao umekaaje? Make katibu anakula sawa na mbunge na hiyo ni moja ya masharti yake.

Hapo ukienda kwa vingozi wengine wa chini yake bila kumsahau mwenyekiti utakuta hali ndo hizohizo hazjatofautiana sana.

Leo ni karibu miaka 22 hata ofisi mmeshindwa kujenga lakini mnajua kulipana mishahara mizuri... mikoani ofisi zimechoka alafu mnakuja na ngonjera za baba mwenyenyumba hayatola!!!

Usikimbilie kubandua banzi kwenye jicho la mwenzio wakati lako lina boriti.
 
Tatizo sio hoja yako mrembo faiza tatizo ni chuki yako kwa Nyerere anyway sijui ni nini alichowafanyia wazazi wako maana wewe ni mtoto na utakua umesimuliwa tu na kujenga chuki. Yote kwa yote kua na moyo wa kusamehe. Sahahu yaliyopita tugange yaliyopo na yajayo. Makosa aliyofanya Nyerere wakati huo Tuyaache tufanye yetu mazuri kwa sasa. Muda bado upo

Naam, mimi ni mtoto kwa wazazi wangu, lakini kumbuka pia mimi ni mtu mzima niliyekuwepo kabla ya Uhuru na nimeyashuhudia mafataki na mafashfaash ya siku ya Uhuru.

AlhamduliLlah nimeyaona ya wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete.

Unajuwa kuwa wakati wa Nyerere pekee ndiyo nchi hii ikawa na njaa ya ajabu, kula tunapiwa chakula kilo kwa wiki kwa kaya, tukaletewa unga hatuwahi kuuona toka kuzaliwa wa rangi ya manjano kabisa. Tukaletewa dawa za meno ukipigia mswaki unakosa test ya chakula kutwa nzima.

Hayajatokea hayo kwa Mkoloni, Mwinyi, Mkapa wala Kikwete. Ni madhila ya uongozi mbovu wa Kikwete.

Na ndipo wakati huo rushwa na magendo yakashamiri vibaya sana.

Kwanini hayo tuyasiyaseme? na tuendelee kusifu yasiyosifika?
 
Tuanze na ruzuku ya chadema inayoishia makao makuu vp mgao umekaaje? Make katibu anakula sawa na mbunge na hiyo ni moja ya masharti yake.

Hapo ukienda kwa vingozi wengine wa chini yake bila kumsahau mwenyekiti utakuta hali ndo hizohizo hazjatofautiana sana.

Leo ni karibu miaka 22 hata ofisi mmeshindwa kujenga lakini mnajua kulipana mishahara mizuri... mikoani ofisi zimechoka alafu mnakuja na ngonjera za baba mwenyenyumba hayatola!!!

Usikimbilie kubandua banzi kwenye jicho la mwenzio wakati lako lina boriti.

Wakumbushe wasisahau pia katibu mkuu wa chadema alivyoigeuza chadema saccos yake na mchumba kujikopesha mamia ya mamilioni kujijengea jumba la kifahari Mabwepande.

cc Dr.W.Slaa
 
Last edited by a moderator:
Ujinga mwingine unatisha sana,

Hivi Nyerere hata asipochukuwa mshahara alikuwa anashida ipi, nyumba bure, kula bure, kulala bure, na huku anazidi kuiangamiza Tanzania kuwa nchi masikini ya mwisho duniani.

Mtei asitafute umaarufu wa Kisiasa kwa kupitia jina la Nyerere, yeye kwanini aliachia/aliachishwa uwaziri? aeleze ukweli.
Michango yako hasi dhidi ya Nyerere inakufanya uonekane una chuki binafsi na huyu mtu,ambaye kwa kauli yake alikiri kuwa hakuwa malaika kuna makosa aliyafanya na mazuri mengi pia.
Lakini aliwashangaa warithi wake kufauata mabaya aliyoyafanya na kuacha mazuri,wakati mwingine inaonekana ni kwa vile hakuwa wa hitikadi yako.
 
Michango yako hasi dhidi ya Nyerere inakufanya uonekane una chuki binafsi na huyu mtu,ambaye kwa kauli yake alikiri kuwa hakuwa malaika kuna makosa aliyafanya na mazuri mengi pia.
Lakini aliwashangaa warithi wake kufauata mabaya aliyoyafanya na kuacha mazuri,wakati mwingine inaonekana ni kwa vile hakuwa wa hitikadi yako.

Kama unakiri kuwa Nyerere mwenyewe kakiri, kwa hiyo hutaki tuyaainishe makosa yake ili wengine wasirudie?

Huwa mnafikiri au mnabwabwaja tu?
 
Kama unakiri kuwa Nyerere mwenyewe kakiri, kwa hiyo hutaki tuyaainishe makosa yake ili wengine wasirudie?

Huwa mnafikiri au mnabwabwaja tu?

Kwahiyo unaanika ya utawala wa nyerere ila ya utawala wa sasa mwiko.
 
Sifa ipi? uadilifu upi? kudhulumu watu mali na roho zao ndio uadilifu?

Unajuwa ni wangapi waliokufa kwenye hayo maamuzi ya "Azimio la Arusha" ambayo hukubalini nayo? hata idadi hawajulikani, watu walihamishwa vijiji vyao vya asili na kupelekwa kutupwa maporini, waliokufa kwa magonjwa haya, waliokufa kwa kuliwa na wanyama haya, waliokufa kwa kugongwa na nyoka haya.

Huo ndio uadilifu?

Nyerere HAIKUIGEUZA Ikulu kuwa pango la WANYANG'ANYI wala yy na FAMILIA yake HAWAKUITUMIA ikulu kwa faida zao bifasi!Sikupata kushuhudia WATOTO wa Nyerere wakija Mbeya kusomewa taarifa za mkoa kama nao wapo ndani ya uongozi wa dola!!

Kwenye maadili ya matumizi mazuri ya hela zetu Nyerere anamzidi JK tena kwa mbali sana,kwenye utawala wa sheria, KIDEMOKRASIA na kuvumiliana ndiyo sifa pekee ya JK anayomshinda Nyerere! FaizaFoxy usichanganye sifa hizo mbili!!
 
Last edited by a moderator:
kuna watu ambao inawezekana walidanganywa kuwa nyerere na baba yao walipoona wala hawakumbuki basi wamejenga chuki naye kiasi kikubwa sana. faizafoxy akiona jina la nyerere tu anapata shida sana chuki imemjaa mpaka basi utadhani aliwah pewa mimba na mtu halafu huyo mtu akaikataa...chuki yake huwa haiishi. au ukute kuna mzee alimpa mimba mama yako halafu akaikataa yaan akakukataa basi ile chuki huwa haitoki hata kwa JIK ni kumsameheh tu na sasa hivi ukichnganya na swaumu basi ndi huyu dada anakuwa kama vile yupo .....maana huwa pia wanakuwa na kisiran sana wengine. mumsamehe bure maana si yeye hapo alipo atakuwa anazungumza kwa nguvu ya maimuna au subian...
 
Nyerere HAIKUIGEUZA Ikulu kuwa pango la WANYANG'ANYI wala yy na FAMILIA yake HAWAKUITUMIA ikulu kwa faida zao bifasi!Sikupata kushuhudia WATOTO wa Nyerere wakija Mbeya kusomewa taarifa za mkoa kama nao wapo ndani ya uongozi wa dola!!

Kwenye maadili ya matumizi mazuri ya hela zetu Nyerere anamzidi JK tena kwa mbali sana,kwenye utawala wa sheria, KIDEMOKRASIA na kuvumiliana ndiyo sifa pekee ya JK anayomshinda Nyerere! FaizaFoxy usichanganye sifa hizo mbili!!

Hizo ni porojo za mchana kweupe.

Msasani unapujuwa, Mwitongo unapajuwa. Mpaka leo tunakatwa kodi zetu kupalipia gharama zak kwa faida ya nani? yako wewe? au ya familia ya Nyerere?

Zingine ni porojo na kuhororoja tu, wanakula bata kwa mrija.
 
Kwahiyo unaanika ya utawala wa nyerere ila ya utawala wa sasa mwiko.

Nyumba hujengwa kwa kuanza na msingi, msingi ukiwa mbovu unategemea nini?

Nyerere ndio alitakiwa aweke msingi wa maana kwa miaka 24 aliyokaa madarakani, na vibaraka wake wawili.

Leo ndio tunaona Kikwete anabomoa huo msingi mbovu na kuujenga mwingine imara wa kidemokrasia na kisheria.
 
Mara nyingi asiye na hoja hujiita mwelevu na kuwatweza waliowelevu kuliko yeye kuwa ni wajinga. Hulka ya mjinga ni kujikweza, mweledi hujipambanua kwa hoja zake zenye uweledi ndani yake. Kuhitimisha hoja yako kwa kuwaita watanzania wenzako ni wajinga ni kiashiria tosha cha jinsi ulivyo. Punguani wa Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili huona watu wote wanamzunguka kama ni punguani wakiwemo madaktari wake. Sisemi wewe ndiwe ila unafananafanana na mfano huo.
Mtei hazungumzii jinsi ya kuendesha Taasisi ya Uraisi, anazungumzia jinsi viongozi wa sasa wasivyowaonea huruma masikini kiasi kuwa aliona apunguze mshahara wake ili kupunguza pengo la kipato kati ya walio nacho na wasionacho.
Ikiwa huoni uhusiano uliopo kati ya mshahara wa Raisi na uchumi wa nchi hapo kuna tatizo kubwa. Ikiwa sehemu kubwa ya pato la nchi linachukuliwa na wachache ina maana wananchi waliowengi hubakia kuwa masikini. Wananchi wakiwa masikini maana yake wanashidwa kumudu mahitaji yao ya kwaida kama vile kupeleka watoto wao shule, hospitali na kuwekeza kwa maendeleo yao binafsi.
Kubwa zaidi kiongozi wa nchi akiwa mbinafsi wasaidizi wake wote huwa wa binafsi kwa kuwa kiongozi wao ( their role model) ni fisadi. Raisi akijilimbikizia mshahara mkubwa kupita kiasi na wasaidizi wake pia hudai waongezewe na Raisi anakosa nguvu ya kuwazuia kwa sababu anaogopa kuzodolewa. Mawaziri, Wabunge na viongozi wengine kudai posho na marupurupu kila mara ni matokeo ya viongozi wao kujilimbikizia mali kupitia nafasi zao za uongozi. Uadilifu wa Baba au mama ni muhimu kwa uadilifu wa familia. Sio ajabu baba mzinzi kuwa na watoto wazinzi pia. Kama FaizaFoxy haya hujayaona ni kwa sababu bado hujakuwa, kuwa utayaona. Ni hulka ya watoto kuona wamekuwa sawa na wazazi wao lakini ukweli ni kuwa wanakuwa bado hawajakuwa.
Huo ni upunguani wa hali ya juu, uwe wa miaka 100 iliyopita uwe wa leo, Rais ni Rais tu.

Kuna tofauti ipi ikiwa katiba na kanuni ya kuuendesha tasisi ya Urais ni hiyo hiyo au uliibadili wewe?

Huu ujinga mtauwacha lini Watanzania? hivi mshahara wa Nyerere au wa Kikwete unamsaidia nini Mtanzania? kuna Watanzania kibao wana mishahara mikubwa na kipato kikubwa kuliko Rais x 1000.

Mbona mnakuwa wajinga kiasi hiki?
 
Back
Top Bottom