ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,681
- Thread starter
- #81
Mwaka 1979 Mwalimu Julius Nyerere alipomsimamisha kazi Edwin Mtei(gavana wa BoT wakati huo),kinyongo kiliendelea.Ulikuwepo msuguano mkubwa kati ya Mwalimu na Mtei kuhusu utekelezaji wa sera za IMF nchini Tanzania na katika moja ya mambo ambayo Mwalimu hakutaka hata kuyasikia lilikuwa suala la kushusha thamani shilingi yetu dhidi ya fedha za nchi za kigeni (devaluation) tulizokuwa tunafanya nazo biashara.Katika moja ya hotuba za Mwalimu alishaliongelea hili.1979 haukuwa mwaka mzuri kwa Edwin Mtei ila alipata kazi katika shirika la fedha IMF na kuhamia Marekani ambapo wanawe walipata elimu yao huku akiwepo Lilian Mtei ambaye baadaye alikuja kuolewa na Freeman Aikaeli Mbowe.
Nimekuwekea haka kastori kafupi lakini kana maana kubwa sana
- Edwin Mtei ameishafanya kazi katika Shirika la IMF je huko hakupata fedha ambazo anaweza kuwa ameziendeleza na kuongezeka maradufu?
- Wakati wa Nyerere kulikuwa na uwezekano wa kiongozi kuiba fedha kama unavyojiaminisha sasa?
Ukimtaja mtuhumiwa mmoja tu wa ufisadi wa mali ya umma ambaye ni jobless basi kauli yako hii itakuwa na mashiko.