Mtei - Mbowe - BoT; Connecting the dots...

Mtei - Mbowe - BoT; Connecting the dots...

Kwa akili yako Mbowe anamiliki biashara moja ya Ukumbi wa Burudani (Billicanas)?

Na kama hajalipa/ halipi kodi huoni kama huo ni udhaifu wa Serikali yetu ya CCM ktk kukusanya kodi?

Na kama, kwa namna yoyote ile walitumia nafasi zao vibaya kwa maslahi binafsi wakiwa watumishi wa UMMA kwa nini serikali haikuwachukulia hatua? Huoni kama huo nao ni udhaifu wa Serikali yetu sikivu ya Chama Cha Mapinduzi?

Mkuu msikubali kuwa distracted na hawa kenge maji.

Kuna issue tatu mbele yetu:
1) Katiba mpya
2) Mabilioni ya wakwasi Uswisi
3) Vyama vinapewa bilions of tax payers maney na havifuati sheria.


Haya wanayoyasema hawa kenge maji ni upuuzi tu na mkiyakubali basi unaondoka kwenye mstari mazima.
 
Kwanini Dr.markopolo unajidhalilisha namna hii.Yaani kwa elimu yako na umuhimu wako katika jamii hupashwi kuwa mtu wa kutengeneza majungu na kupika propaganda.Amana wagonjwa wanakufa daily kwa upungufu wa madaktari,nenda kaokoe ndugu zetu huko propaganda waachie kina le mutuz na msalan wasio na elimu yoyote
 
Pumba tupu na imeandikwa kiutashi wa kisiasa zaidi kuliko fact
 
kama unajua inalipa kilichokuaondoa Chadema ni nini kama sio njaa
na kutafuta msamaha wa makontena yenu bandarini???
Kila siku mwaiandama chadema na mbowe mbona hamzungumzii hao mafisadi wengine walioficha fedha uswizi?
mbona hamwandiki mabaya ya CCM?
Kama kweli mbowe fisadi nae ashughulikiwe
Hii biashara ya chadema inalipa sana

Na bado mnazidi kumchangia mihela
 
ZeMarcopolo, nimekuwa nikijiuliza sana kwa nini pamoja na kujiunga JF tarehe 11/5/2008 (ukiwa umenitangulia kwa siku 20) na baada ya kuwa na posts zaidi ya 10,000 (mimi nikiwa na posts chini ya 4,000), kwa nini rep power yako ni 0 (sufuri). Kwa mara ya kwanza naweza kusema nimepata jibu la swali langu hilo kutokana na post zako ambazo kila siku zinazidi kukufichua uwezo wako kifikra na kiakili. Thread yako ya kwanza jamvini lilikuwa ni la kupongeza jitihada zilizokuwa zikifanyika mjini Moshi kuwasaida watu wenye matatizo ya akili. Wakati huo sikuweza kuunganisha dots hizo juhudi zako zilitokana na msukumo gani hasa?...kwa nini nauliza hivi?

Mzee Edwin I. Mtei, alikuwa Gavana wa Benki kuu kwa kipindi cha miaka minane kuanzia 1966 hadi 1974. Wakati anateuliwa kuwa Gavana mtoto Freeman Aikaeli Mbowe alikuwa na umri wa miaka mitano (alizaliwa mwaka wa uhuru 1961) na wakati Mzee Mtei anaacha kazi Benki Kuu Kijana Mbowe alikuwa na umri wa miaka 13! ZeMarcopolo, umeanza mada yako kwa kusema nanukuu;
ZeMarcopolo said:
Mwenyekti wa kwanza wa Chadema, Mzee Edwin Mtei, alikuwa Gavana wa BoT. Mwenyeti wa sasa wa Chadema, Mh. Freeman Mbowe, alikuwa mwajiriwa wa BoT.
Hukuishia hapo ukaanza kuunganisha dots kwa kudai, nanukuu;
ZeMarcopolo said:
Je, kuunganisha familia hizi ni njia ya kuongeza uaminifu wa "ushirikiano" waliokuwa nao tangu BoT? Je, "ushirikiano" wao waliouanza BoT unaendelea ndani ya Chadema?
ZeMarcopolo, kama asemavyo Invisible, Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!:coffee:
 
Ze marcopolo andishi hili limenifanya nijue kwamba kiwango chako cha elimu ni kidogo mno ! Na kama una karatasi lolote linaloonyesha kwamba unaelimu kubwa , basi kuna mawili , utakuwa uliiba mtihani au unatumia cheti cha marehemu!
 
je Mbowe Freeman ndiye alianza kuoa BINTI wa Mtei kabla baba yake hajachangia fedha kwa. Mtumishi wa Mungu kwenda UN.
Issue ni endapo Mbowe alifungua biashara kwa kufuata Sheria
 
ZeMarcoplo post yako ingekuwa na maana na watu wengi wangechangia positively kama ungeweka walioiba pesa zetu wote ili tuweze kuchania.Kwa kumuweka Mbowe na Mtei peke yake siyo sahihi na ndiyo maana umepata fedheha kuliko pongezi.Kwa ufupi naweza kusema una chuku binafsi kwa hao wawili au kwa wachagga,maana wengi wenu wakisikia wachagga tu pressure zinawapanda.Wachagga wengi ni sawa na wahaya kwani wengi wao walitajirika kutokana na kulima kahawa.Pole sana lakini.
 
Ishara mojawapo ya mtu mlevi, mwoga, aliyekata tamaa pasi na kujua afanyalo; ni pale anapotingwa na giza na kuamua kujikusanyia mawe na kuyarusha kule anakoelekea bila kujali wala kutambua ni nani atakumbwa na madhila ya kuumizwa na mawe ayarushayo.
 
ZeMarcopolo, nimekuwa nikijiuliza sana kwa nini pamoja na kujiunga JF tarehe 11/5/2008 (ukiwa umenitangulia kwa siku 20) na baada ya kuwa na posts zaidi ya 10,000 (mimi nikiwa na posts chini ya 4,000), kwa nini rep power yako ni 0 (sufuri). Kwa mara ya kwanza naweza kusema nimepata jibu la swali langu hilo kutokana na post zako ambazo kila siku zinazidi kukufichua uwezo wako kifikra na kiakili. Thread yako ya kwanza jamvini lilikuwa ni la kupongeza jitihada zilizokuwa zikifanyika mjini Moshi kuwasaida watu wenye matatizo ya akili. Wakati huo sikuweza kuunganisha dots hizo juhudi zako zilitokana na msukumo gani hasa?...kwa nini nauliza hivi?

Mzee Edwin I. Mtei, alikuwa Gavana wa Benki kuu kwa kipindi cha miaka minane kuanzia 1966 hadi 1974. Wakati anateuliwa kuwa Gavana mtoto Freeman Aikaeli Mbowe alikuwa na umri wa miaka mitano (alizaliwa mwaka wa uhuru 1961) na wakati Mzee Mtei anaacha kazi Benki Kuu Kijana Mbowe alikuwa na umri wa miaka 13! ZeMarcopolo, umeanza mada yako kwa kusema nanukuu;

Hukuishia hapo ukaanza kuunganisha dots kwa kudai, nanukuu;
ZeMarcopolo, kama asemavyo Invisible, Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!:coffee:

Mkuu ni lizuzu limetoka usingizini na kukimbilia kuandika upuuzi wake...
 
Kwanini Dr.markopolo unajidhalilisha namna hii.Yaani kwa elimu yako na umuhimu wako katika jamii hupashwi kuwa mtu wa kutengeneza majungu na kupika propaganda.Amana wagonjwa wanakufa daily kwa upungufu wa madaktari,nenda kaokoe ndugu zetu huko propaganda waachie kina le mutuz na msalan wasio na elimu yoyote

Kibaya zaidi ni kwamba wala hapendezi kuwa katika fani hiyo ya kupika majungu na propaganda.
 
HIVI NI KWANINI TUNADANGANYANA??? Kama HIVYO MTEI alimpatia kazi MBOWE MTEI aliondoka UGAVANA 1980's wakati MBOWE akiwa na Miaka 20 sasa angempatiaje kazi?

Mbowe angepatiwa kazi na watu wengine zaidi ya MTEI sababu baba yake alikuwa anajulika serikalini enzi hizo....

Kuhusu pesa... MTEI haujui alifanya kazi WORLD BANK baada ya kuondoka UGAVANA? sasa Malipo yake yalikuwa ni Minono na alikaa kwa zaidi ya Miaka 12 Washington DC

Kwanini Wataka kudanganya Watanganyika; Yaani Unajaribu kulinda wezi wa MALI za NCHI HII kwa kutaka kulazimisha WIZI WA MTEI na MBOWE??

Sasa kama kweli huo wizi umeweza kuupata na kuconnect hizo DOTS... Vipi kwa MAWAZIRI waliokuwa serikalini DOTS zao haziwezi kuwa connected???
 
ZeMarcoplo post yako ingekuwa na maana na watu wengi wangechangia positively kama ungeweka walioiba pesa zetu wote ili tuweze kuchania.Kwa kumuweka Mbowe na Mtei peke yake siyo sahihi na ndiyo maana umepata fedheha kuliko pongezi.Kwa ufupi naweza kusema una chuku binafsi kwa hao wawili au kwa wachagga,maana wengi wenu wakisikia wachagga tu pressure zinawapanda.Wachagga wengi ni sawa na wahaya kwani wengi wao walitajirika kutokana na kulima kahawa.Pole sana lakini.

mwambie mkuu: kule uchagani hakuna nyumba ya nyasi hata moja...!!!!!
 
Kama hii ndo aina ya Madaktari tulio nao hapa Bongo, wagonjwa wengi watapasuliwa vichwa badala ya Miguu.
 
Ze marcopolo andishi hili limenifanya nijue kwamba kiwango chako cha elimu ni kidogo mno ! Na kama una karatasi lolote linaloonyesha kwamba unaelimu kubwa , basi kuna mawili , utakuwa uliiba mtihani au unatumia cheti cha marehemu!

Ha ha haaaaaa! Erythrocyte wacha kumsakama colleague he he heeeee!! Job true true...
 
Last edited by a moderator:
Mbowe alifanya kazi BOT mwaka gani na Mtei aliacha kufanya kazi BOT mwaka gani?? Miaka ikiwekwa wazi ndo tutakua na hoja ya kujadili hapa.

jibu wanalo tume wao waliunganisha dots wakajua ni fisad wakamuhoji
 
Mwenyekti wa kwanza wa Chadema, Mzee Edwin Mtei, alikuwa Gavana wa BoT.

Mwenyeti wa sasa wa Chadema, Mh. Freeman Mbowe, alikuwa mwajiriwa wa BoT.

Kabla ya kupata uenyeti wa Chadema, Mh. Freeman Mbowe, alimuoa mtoto wa Mwenyekiti wa kwanza wa Chadema, Mzee Edwin Mtei.

Mwenyekiti wa sasa wa Chadema, amekiri kwa maandishi kuwa anamiliki mabilioni ya shilingi pesa tasilimu na mali zisizohamishika yenye thamani ya mabilioni ya shilingi.

Hesabu za kiasi cha kodi alicholipa Mh. Freeman Mbowe kwa miaka kumi iliyopita hakiendani na utajiri huo mkubwa alio nao.

Mwenyekiti wa kwanza wa Chadema Mzee Edwin Mtei, hupenda kujitambulisha kama mkulima. Hata hivyo, utajiri wake ni mkubwa sana kuliko kiasi cha uzalishaji wa shamba lake lililopo Tengeru, Arusha.

Mzee Mtei amekuwa akitumia pesa zake binafsi kuendesha shughuli zote za Chadema tangu ilipoanzishwa mpaka ilipofikia hatua ya kupata wabunge na ruzuku. Huu ni utajiri wa hali ya juu. Sio mbaya kuwa tajiri, lakini utajiri wa mtu ni lazima uendane na kiasi cha kodi anacholipa. Mtu akiwa tajiri sana lakini katika orodha ya walipa kodi haonekani, ni ishara ya ufisadi.

Ukwasi huu wa wanasiasa hawa wawili walioitumikia BoT na kuamua kuunganisha familia zao kwa njia ya ndoa ya binti wa mmoja wao unatokana na chanzo gani?

Je, kuunganisha familia hizi ni njia ya kuongeza uaminifu wa "ushirikiano" waliokuwa nao tangu BoT? Je, "ushirikiano" wao waliouanza BoT unaendelea ndani ya Chadema? Je, hii ndio sababu ya Mzee Mtei kulazimisha Mbowe aendelee kuwa Mwenyekiti na kukataza wagombea "who are from nowhere"?.

Je, biashara ya ukumbi wa muziki inamuwezesha mtu kumiliki mabilioni nje ya nchi? Kiingilio bilicanas ni shilingi ngapi kila mtu? Kwa siku wanaingia watu wangapi? Je, zinatosha kununua nyumba Uingereza, Marekani, Afrika Kusini na Dubai?

Its too early to go to bed, wake up. Connect the dots...

Mwaka 1979 Mwalimu Julius Nyerere alipomsimamisha kazi Edwin Mtei(gavana wa BoT wakati huo),kinyongo kiliendelea.Ulikuwepo msuguano mkubwa kati ya Mwalimu na Mtei kuhusu utekelezaji wa sera za IMF nchini Tanzania na katika moja ya mambo ambayo Mwalimu hakutaka hata kuyasikia lilikuwa suala la kushusha thamani shilingi yetu dhidi ya fedha za nchi za kigeni (devaluation) tulizokuwa tunafanya nazo biashara.Katika moja ya hotuba za Mwalimu alishaliongelea hili.1979 haukuwa mwaka mzuri kwa Edwin Mtei ila alipata kazi katika shirika la fedha IMF na kuhamia Marekani ambapo wanawe walipata elimu yao huku akiwepo Lilian Mtei ambaye baadaye alikuja kuolewa na Freeman Aikaeli Mbowe.

Nimekuwekea haka kastori kafupi lakini kana maana kubwa sana
- Edwin Mtei ameishafanya kazi katika Shirika la IMF je huko hakupata fedha ambazo anaweza kuwa ameziendeleza na kuongezeka maradufu?
- Wakati wa Nyerere kulikuwa na uwezekano wa kiongozi kuiba fedha kama unavyojiaminisha sasa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom