Mtei awashauri viongozi CCJ wahamie CHADEMA

Na hata CCJ ikisajiliwa -- MKJJ ana uhakika gani kwamba serikali ya CCM haitafanya systematic campaign against it, tena in top gear, if at all it will pursue what Chadema was doing -- that is exposing ufisadi in CCM and its government? CCj inaweza ikapona kufinywafinywa iwapo tu itafunga mdomo wake katika suala la ufisadi -- au lkubali kuunga mkono ufisadi! yaani kama vile vyama vingine visivyosikika hadi wakati wa uchaguzi tu.

CCm haitakubali tishio lolote dhidi yake -- na tishio kubwa kwake ni kuumbuliwa kwenye masuala ya utafunaji nchi.
 
Mwanakijiji,
Nimesoma posts zako, nimevuta kigoda nikakaa kwa kukata tamaa kama ni wewe unaandika haya dhidi ya Chadema.
Natamani CCJ isajiliwe tu tena bila mkwara wowote:welcome:lakini nakuhakikishia mwezi wa kumi na moja uchaguzi utakuwa umekwisha na hamtakuwa na kiti hata kimoja bungeni. Note hili na niulize baada ya uchaguzi.
Na hapo sitaki kuzungumzia vyama vingine. Mwisho tunyamaze kimya maana hatutaweza kuiondoa sisi m katika uharibifu wa nchi hii milele.
Narudia kusema mmkjj kwamba sisi j hawataweza kushinda kiti hata kimoja kama mawazo yako ndio mawazo ya sisi j Tanzania.
Kwaheri lala salama.
 
Mwanakijiji anadhani CCJ ni kila kitu, kiasi cha kudharau ushauri wa Mzee Mtei. nafikiri ni kiburi tu kuwa CCJ wataleta miujiza within a short time.

Naona Mwanakijiji anapungua uzito wa hoja siku hadi siku.

Tusubiri
 
Mwanakijiji,
Nimesoma posts zako, nimevuta kigoda nikakaa kwa kukata tamaa kama ni wewe unaandika haya dhidi ya Chadema.
Natamani CCJ isajiliwe tu tena bila mkwara wowote:welcome:lakini nakuhakikishia mwezi wa kumi na moja uchaguzi utakuwa umekwisha na hamtakuwa na kiti hata kimoja bungeni. Note hili na niulize baada ya uchaguzi.
Na hapo sitaki kuzungumzia vyama vingine. Mwisho tunyamaze kimya maana hatutaweza kuiondoa sisi m katika uharibifu wa nchi hii milele.
Narudia kusema mmkjj kwamba sisi j hawataweza kushinda kiti hata kimoja kama mawazo yako ndio mawazo ya sisi j Tanzania.
Kwaheri lala salama.

Mwanakijiji ni nani? si ni raia kama wewe ambaye ametokea kuwa na akili, muda mwingi wa kukaa kwenye computer na mawazo yake binafsi. Wengine sisi tulijua tu kuwa hapa kuna mshikeri na tukaanza mapema kusema. Hili la kwamba watakuwa hamna kiti hata kimoja wakati kule pemba cuf hata wakisimamish nyani wanashinda sio kweli.

Hili ni swala zuri tu kwani lazima ni fundisho kwa watu, iwe vyama vya upinzani, ccm, activits au wale wanaona kuwa wanaweza kutumia umaarufu wao kuvuruga kitu kwa maslahi binafsi. History huwa inaonesha kuwa maandamano na nguvu ya uma huwa haina chama wala kiongozi. wakiwepo hao tu basi sura inakuwa tofauti.

Kumbuka uongozi wa Kennedy ulipohaha kuwapa uongozi wakina malcom X na King juu ya yale maandamano ya Match to washington basi utajua ni kwa nini nguvu ya umma huwa haiitaji kiongozi bali viongozi (vyama)wanatakiwa kuwa tayari kuongoza nchi
 
Mwanakijiji anadhani CCJ ni kila kitu, kiasi cha kudharau ushauri wa Mzee Mtei. nafikiri ni kiburi tu kuwa CCJ wataleta miujiza within a short time.

Naona Mwanakijiji anapungua uzito wa hoja siku hadi siku.

Tusubiri

Kwenye red. Nakubaliana nawe Mkuu. isitoshe siku hizi anaanzisha topic nyingine hazina maana kabisa, anakuwa kama vile Malaria Sugu vile.
 
Naona Mwanakijiji anapungua uzito wa hoja siku hadi siku.
Tusubiri
Ni wachache sana wanaosalimika inapokuja suala la kukubali hoja dhidi ya kitu/mtu unaempenda..,Yeye ni mwanachama mwanzilishi na mpanga mikakati mshilikishi wa CCJ, Unategemea akubali kushindwa?? Ni wachache wenye ujasili wa kukubali kushindwa..!
 
TUache mambo ya kulazimishana hapa. Ukweli ni kuwa Vyama vya Siasa Tanzania havina mwelekeo, sera imara wala Itikadi zinazoeleweka.

TUanze na CCM, Katiba inasema CCM ni chama cha Kijamaa na kinafuata siasa za Ujamaa. Lakini hata baada ya mabadiliko ya kinafsi ya Watawala wakuu wa CCM kuwa Mabepari na CCM na Serikali yake kuukumbatia Ubepari, bado kin adai chenyewe ni chama cha kijamaa!

Sasa ukija kwa wengine, hakuna mwenye msimamo kamili wa kusema "sisi ni mabepari" "sisi ni wajamaa" "sisi ni wakomunisti" "sisi ni maliberali" "sisi ni wahafidhina-conservative" kwa kuwa Tanzania na siasa zake bado hazijaweza kujitambulisha na kueleweka kuwa siasa zipi ni za mrengo wa kushoto na ni kushoto ipi, mrengo wa kati kati ya namna gani na mrengo wa kulia, kulia ya mbali au ya karibu.

Pasipokuwa na Chama chochote kutambulika Itikadi yake na ikaeleweka, ni vigumu tuamini kuwa eti Vyama vikiungana, kutakuwa na mafanikio hata kama lengo ni kuing'oa CCM.

Leo hii muungano wa CUF na Chadema unafanikiwa, wanashika madaraka ni siasa za nani tutazifuata? Kama tayari tushadai CUF ni wadini na Chadema ni wachagga, je tutaongozwa kichagga au kidini? je kama mmoja ni mkomunisti na mwingine ni bepari, je tutafuata la nani na kumuamini nani? Je hatuoni kuwa udhaifu huu ni rahisi kwa CCM ambao japo kimatendo si wajamaa, lakini ni rahisi kwa wao kudai wao ni wajamaa na kupokelewa na wananchi?

Hivyo ni lazima vyama vindelee kujijenga kwa ubinafsi na kuongeza nguvu za kuuza si sera za kuking'oa CCM pekee, bali kuwahubiria Watanzania Itikadi wao ili Watanzania wawe waumini wa Itikadi kwa kujifananisha na kuelewa Itikadi za Chama kuendana na maisha yao na si adha ya kushindwa kuivumilia CCM.
 
GS,

Tatizo ni kuwa tuna sehemu kubwa kati yetu ambao tunang'ang'ania ushabiki na kuamini kuwa Chadema ndicho chama mbadala. Labda ni ule mvuto wa Dr. Slaa, Chacha Wangwe, Zitto na Kitila. Lakini, hatuwezi kuendelea kuburuzwa kama enzi zile za kuwa Chipukizi wa CCM ambazo tulivutiwa na kunogewa na kusahau kuwa wadadisi na kuhoji mambo.

Humu ndani ya JF, kuna ngome kubwa sana inayoilinda Chadema, wala sitashangaa kuwa sehemu kubwa ya wana JF ni washabiki kama si wanachama wa Chadema. Sasa ukiandika kuwakosoa Chadema, fukuto litakalokufuata ni kubwa la kubezana na wala si kujenga hoja au kujibu hoja.

Mambo ya ubinafsi na kushambulia nafsi na si kuchambua hoja huanza, na ndio maana sehemu kubwa ya majadiliano hapa yamegeuka si kuchambua hoja na kujenga hoja za kukubaliana au kupingana bali ni kudai Mwanakijiji kapotoka au kaanza ku-dilute the message kisa kaongea dhidi ya Chadema.

Kama umeona, Shalom kanirukia na kudai eti nafuata nyayo za Mwanakijiji, na siku nikionyesha uhuru wa mawazo atatoa zaka! EBO!

Watu wameichoka CCM, lakini hawajui kupanga hoja ziuzike kwa kila roho Tanzania ili CCM ianguke. Ukitoa ushauri kwa mtazamo mwingine, unitwa msaliti au hujui unachokisema. Lakini kama nilivyomwwambia Dr. Slaa kwenye ile mada yangu ya Udhaifu wa Operesheni Sangara, ni kuwa huu ni mwaka karibu 20 tangu vuguvugu la Chadema na Upinzani kuanza kudai ni lazima CCM iondoke na kuondolewa, lakini kila siku zinavyozidi kusonga mbele, unaona CCM inazidi kushika hatamu pamoja na migongano waliyonayo ndani mwao.

Najiuliza kama Watanzania wameichoka CCM kama tunavyodhania, iweje ile kasi liyofanywa na TAA na TANU kumn'goa mkoloni ilifanikiwa kwa haraka, lakini vyama vya upinzani vinashindwa kuiangusha CCM? Je tuendelee na majaribio kuamini TLP, Chadema, CUF, NCCR, DP na hata sasa kukimbilia mgombea huru ndiyo suluhisho mpaka lini kama si kwa vyama hivi kujipima na kuanza kujiuza kwa kutuambia Itikadi zao ni zipi ili tuwe na uchaguzi basi wa kuamua tumtakaye?

Hatuwezi kujenga mfumo bora wenye msingi mzuri wa kisiasa bila kuwa na utambulisho wa kiitikadi ambao utatoa tofauti za kichama na kuwapa Watanzania uwezo kuchagua itikadi wanayopenda, sawa na dini zilivyo.

Hivyo tunaacha kujenga hoja, tunaanza shambuliana kisa hatutaki kusikia kukosolewa na hivyo kuwaacha CCM wakiendelea kukenua meno na kutamba ushindi mwingine ile Jumatatu bada ya uchaguzi mkuu.
 
Rev Kishoka said:
TUache mambo ya kulazimishana hapa. Ukweli ni kuwa Vyama vya Siasa Tanzania havina mwelekeo, sera imara wala Itikadi zinazoeleweka
.

Reverand hili hata hao ccj ambao wanasema wao ni mbadala bado hawajaweza kuliweka wazi,hata hivyo tujifunze kutoka kwa wenzetu ie labor party na conservative huko UK ambao wamekuja pamoja regardless of the tremendous difference,all for the National interest....For the people,na hata US,kuna voting blocks kutoka mrengo wa kati kulia,na kati kushoto ambao huwa wanapiga kura either Republican ama democrats depending on sera za anayetaka kuingia madarakani kwamba watalifanyia nini taifa na wananchi wake especially kwenye yale wanayokabiliana nayo ie uchumi, terrorism,job creations nk.na wasipofanya huwa wako held accountable kwa kutokuchaguliwa tena,na si kama Tanzania ambapo mtu atakuja kusema uongo wa wazi ie maisha bora "Kwa kila mtanzania" wakati ni uongo mtupu halafu bado wanasahau....Sasa tunakabiliwa na ufisadi na wananchi wanaelewa kuwamaisha bora hayawezi kuja kama ufisadi ukiendelea kuwepo kwa kasi hii....

Ni muhimu tukajikita kwenye reality,shida tumeona si kufanya yale yaliyomo kwenye makaratasi,shida ni watendaji,uzuri wa sera na itikadi ni utekelezaji wake na si makaratasi,tumeweza kuona wazi ccm wenyewe wameshindwa kuekeleza sera zao za kwenye makaratasi,umeshasema mwenyewe kuwa unaweza kufanya tofauti na ulichoandika kama wanavyofanya ccm,preac this and do fifferenttly...cha muhimu ni uthubutu wa mabadiliko ndiyo haswa nguzo kuu ya kuelekea kwenye mabadiliko ya kweli na ya muda mrefu na tija kwa Taifa,la sivyo ni sawa na kucheza "gombania goli" ambapo kufunga upande wowote ni halali madhali unapiga bao,basi unaweza hata kujipiga bao wewe mwenyewe,naona ndiko tunaelekea sasa....

TUanze na CCM, Katiba inasema CCM ni chama cha Kijamaa na kinafuata siasa za Ujamaa. Lakini hata baada ya mabadiliko ya kinafsi ya Watawala wakuu wa CCM kuwa Mabepari na CCM na Serikali yake kuukumbatia Ubepari, bado kin adai chenyewe ni chama cha kijamaa!

Hiyo ndiyo haswa definition ya ccj kwasababu wao wamesema wanayo hiyo "combination" ya ubepari na ujamaa na hata kusema kuwa ujamaa una misingi ya ideologies za mrengo wa far right.

Sasa ukija kwa wengine, hakuna mwenye msimamo kamili wa kusema "sisi ni mabepari" "sisi ni wajamaa" "sisi ni wakomunisti" "sisi ni maliberali" "sisi ni wahafidhina-conservative" kwa kuwa Tanzania na siasa zake bado hazijaweza kujitambulisha na kueleweka kuwa siasa zipi ni za mrengo wa kushoto na ni kushoto ipi, mrengo wa kati kati ya namna gani na mrengo wa kulia, kulia ya mbali au ya karibu.

Kwenye dunia ya sasa vyama vinategemea wapiga kura kutoka kwenye ideologies na misimamo ya tofauti,kwa hiyo ni rahisi kukuta chama kina behave kama ni far right kwenye baadhi ya maamuzi na wakati mwingine center etc,mfano kuendelea kwa Obama kwenye vita ya Afganistan ni msimamo mzuri kwa wale wanaodai ni far right ambo walimpa Obama kura kutokana muendelezo wa sera hiyo,hata hivyo hakuwatupa wale wa far left na hata center left kwani pia walifurahishwa na yeye kufunga guatanamo nk licha ya kwamba vita hakujitoa Afghanistan,hata hivyo aliweka misingi ya kufanya hivyo huko Iraki,unaweza kuona ni tafauti ambazo hata hivyo zote zina lengo moja yaani maslahi ya Taifa la marekani na wananchi wake....Issues ni nyingi zitakazoweza kuchangia namna wananchi watakavyochagua viongozi wao na mara nyingi iantegemea na Taifa linakabiliwa na mambo gani,hata US pia kuna mambo kama abortion,issue ambayo inawagawanya wamarekani vilivyo,lakini shangaaa mtu asiye aimini in abortion anampigia kura rais asiye na msimamo mkali kuhusu hilo,mwenye ku beleive in freedom to choose ama kama maisha ya mzazi yamo hatarini....cha msingi ni sababu na nia ya kuing'oa ccm...Kama Taifa,tuangalie kwanza ni nini tunataka,then we build on it,huwezi tu kukaa na kutayarisha sera na kudhani it just magically works....Wananchi hivi sasa wanakerwa na ufisadi,hilo ndo la kwanza,sera za ccm haziruhusu ufisadi,neither would any parties policies initiate ufisadi,ufisadi unafanyika...Sasa wananchi wanataka viongozi waaminifu,waadilfu wenye nia njema na Taifa....Wananchi wapewe wanachokitaka na wasilishwe mambo ya kwenye makaratasi...

Ni kweli lazima chama kiwe na msimamo ambao ndiyo utakuwa na msingi wa base ya wapiga kura,kwa mfano republicans base yao ni far right where as democrats ni far left,hao hawawezi ku cross over,lakini always kuna moderates ambao wao huwa ndiyo mara nyingi wanaamua uchaguzi ama ushindi uelekee wapi base on sera za wanaogombea...Siasa zimebadilika Rev na ni lazima tubadilike accordingly.

Pasipokuwa na Chama chochote kutambulika Itikadi yake na ikaeleweka, ni vigumu tuamini kuwa eti Vyama vikiungana, kutakuwa na mafanikio hata kama lengo ni kuing'oa CCM.

Wanadai topic si kuungana bali "kuhamia" Hata hivyo hayo mambo ya kuwa na "itikadi na ikaeleweka" hayazidi nia ya wenye nia kukaa chini na sababu za kufanya hivyo kama zipo...Ikiwa sababu ni pamoja na kuweka mikakati kwa malengo ya kulinufaisha Taifa na vizazi vijavyo,the hakutaharibika jambo...tunapozungumzia "mafanikio" tujiulize in what context do we hold the term mafanikio....?Tuangalie kwa mapana zaidi...Kwamba malengo ya mafanikio yetu yaelekezwe wapi....?Tukielekeza kwenye maslahi ya Taifa certainly hakuna kitakachoharibika.

Leo hii muungano wa CUF na Chadema unafanikiwa, wanashika madaraka ni siasa za nani tutazifuata? Kama tayari tushadai CUF ni wadini na Chadema ni wachagga, je tutaongozwa kichagga au kidini? je kama mmoja ni mkomunisti na mwingine ni bepari, je tutafuata la nani na kumuamini nani? Je hatuoni kuwa udhaifu huu ni rahisi kwa CCM ambao japo kimatendo si wajamaa, lakini ni rahisi kwa wao kudai wao ni wajamaa na kupokelewa na wananchi?

Hatuwezi kusonga mbele kama tuna migogoro ya kutugawanya,haijalishi kidini ama kikabila....certainly hilo haliwezekani,haiwezekani kabisa tukaendelea kama misngi ya mmamuzi yetu imejikita kwenye hayo ya udini na ukabila....kama hatuna yanayotuunganisha kama taifa,na tukawa tunaamini kabisa kuwa nothing comes above them.....basi haijalishi,tutakuwa mbayu wayu kikweli kweli kwa kuyumbishwa hovyo hovyo tu,hatuwezi kuongozwa kwa hear says,half backed stories and innuendos na kutegemea better outcomes,kama ni kweli vyama hivyo vinaongozwa na hayo mnayoyasema basi sioni ni kwanini issue hizo hazitatuliwi kama ni kweli tuna agenda moja ya maslahi ya taifa....

Taifa la marekani ni watu wenye imani tofauti za kisiasa nk,lakini kuna national interest issue ambazo zinalileta taifa pamoja na kuiweka identity yao intact no matter what,na ndio maana kuna maendeleo tangible na si bla blah za kisiasa....sisi tumebakia kutumia madhaifu yetu sisi wenyewe dhidi yetu sisi wenyewe na dhidi ya vizazi vijavyo,tumegeuka kuwa adui yetu sisi wenyewe.....Ni kama mtoto anayecheza na wembe,vyote wembe na utoto ni adui wa mtoto huyo....We're our own enemies...Na ushauri ambao tumeshawapa vyama hivyo na bado tutaendelea kuwapa;kwamba wasiyapuuzie malalamiko ya wananchi kama kweli ni valid,basi shurti yafanyiwe kazi na wananchi waonyeshwe evidence of whatever is done to correct it,hata kama ni kwa nia njema,kutokana na uelewa wa wananchi,there is always something that can be done,its politics...However kama siyo valid,basi ni ya kuyapuuziwa.

Hivyo ni lazima vyama vindelee kujijenga kwa ubinafsi na kuongeza nguvu za kuuza si sera za kuking'oa CCM pekee, bali kuwahubiria Watanzania Itikadi wao ili Watanzania wawe waumini wa Itikadi kwa kujifananisha na kuelewa Itikadi za Chama kuendana na maisha yao na si adha ya kushindwa kuivumilia CCM.

Hatuna hiyo luxury,honestly rev hiyo ni ya kufikirika kwa mtanzania wa kawaida,wananchi walio wengi hawaitaki ccm sema hawajui wafanye nini na pengine labda hawajui waende wapi,vyama vya upinzani vinaweza kulitumia hilo kama somo la kujifunza,hao walioenda ccj,na sizungumzii the so called "mamluki" bali nazungumzia wale valid ambao hawakujiunga na vyama vingine vya upinzani hadi ccj ilipojitangaza....na pengine wale wana ccm wenye kutaka na wanaotaka kumeguka ila pa kumegukia pakawa ama ni shida...Wapinzani waangalie what went wrong na ama what is wrong,as in kwanini wananchi hao hawakujiunga na vyma vyao na ama hawajiungi nao, ili kama kuna mabadiliko na marekebisho kwa upande wa upinzani basi wayafanye....Na validity ya mabadiliko hayo ikawa established,yani kama mabadiliko hayo hayataathiri well being ya vyama hivyo kiujumla,basi yawepo.....Pengine inaweza kuwa sababu ama kichocheo kwa wale waloshauriwa kuhamia kwenye vyama flani flani kusita kufanya hivyo...?Again kama maslahi ya Taifa ndiyo mbele basi sioni kwanini watu wasikae chini na mazungumzo kufanyika?

Pia ukweli ni kwamba lazima kutakuwa na tofauti za kuwagawa baadhi ya wananchi ambao wanapenda wenyewe ubaguzi ubaguzi...Ama kugawanyika kama ilivyo asili ya watu flani flani....Kuna ma anti this and anti that....Siasa si dini....Kama chama cha republican,voting block yao kubwa ni pamoja na wale tea partiers ambapo kuna wale birthers ambao hawaamini kama Obama kazaliwa marekani,wengine wakiamini ni muislam nk....ni wabaguzi wakubwa,lakini hiyo haina maana kwamba wale ambao si wabaguzi watasema kuwa chama cha republican sasa ni cha wabaguzi na kwa hivyo siwezi kumpigia kura mgombea wake,hilo halipo...Tukifikiria kwa mapana zaidi tutalikwamua Taifa,kuna wale waumini wa kusema hawa ama wale hawafai kuongoza nk,hayo ni ya kuturudisha nyuma,tukiamini kuwa tutaweza kuleta mabadiliko na si kujikata kata wenyewe kama vile tunaongozwa na suicidal mind set.....Ama pia labda sijaelewa ulimaanisha nini kusema vyama vijiendeshe kibinafsi binafsi kwanza?naona kama tumepoteza malengo ama tunajilazimisha kupoteza malengo....?!Jamii tuliyo nayo ya watanzania kwa ukweli reverand Kishoka, haina hiyo luxury ya kusoma sera na itikadi kwenye makaratasi na kusahau kuiondoa ccm madarakani,nani asome na wakati hajui atakula wapi?wananchi walio wengi hawafanyi hivyo,wananchi walio wengi hawazungumzi haya tunayoyazungumza humu....Hawana hiyo luxury......Maisha ni ya taabu na wanataka something other than ccm,kinachohitajika ni kukaa pamoja for the sake of the people...Ni muhimu kutafuta njia rahisi ya kuwapatia wananchi haya tunayoazungumza humu kwa lengo la kuwafungua macho kuwa ni mwelekeo gani unawafaa...Hiyo luxury ya kukijenga chama kiipite ccm kwa sera ni ndoto ya alinacha,certainly umeshakiri mwenyewe kuwa ccm wenyewe wameshindwa kuyafanya yale yaliyomo kwenye makaratasi ie ujamaa na wao kupractice ubepari kwa hivyo tatizo si sera na itikadi flani,haya unayoyataka yameshindikana na ccm licha ya kwamba wako madarakani toka uhuru.....Halafu Since when kuiondoa ccm kukawa si priority tena the first one?

Lets not get our eye off the ball.
 
Tatizo ninaloliona humu ndani ya JF ni issue ya mwelekeo – yaani trajectory kuhusu masuala fulani – hususan ya kisiasa. Trajectory inatakiwa ibadilishwe haraka.

Tukubali kwamba kwa muda mrefu sana Chadema, kwa kiasi kikubwa na kwa muda mrefu, ili-reign supreme katika mada mbali mbali zilizokuwa zinajadiliwa humu JF – hasa kutokana na msimamo wa chama hicho kuhusu masuala ya ufisadi, ambapo viongozi wa chama hicho wamekuwa wakiiyaibua dhidi ya watawala. Mada hizi zilikuwa popular sana na hivyo kuifanya Chadema kuwa popular pia humu ndani.

Sasa hivyo hali hiyo inatakiwa ibadilishwe, kutokana na maamuzi (inavyoonekana) yaliyopitishwa, kwamba Chadema basi, na chama kingine, hata bado hakijapata usajili, kipandishwe chati ndani ya JF.

Ghafla mada ambazo ni hasi kwa Chadema na chanya kwa CCJ zimekuwa zikianzishwa at an alarming rate, nyingi ya hizo by Mwanakijiji.

Bado sijaipata sawasawa mantiki ya yote hii, hasa ile ya kukikweza chama hicho kama kitafanya better kuliko Chadema, hata kabla ya chama kuandikishwa. Hii inashangaza kabisa, hasa ikizingatiwa kwamba hao viongozi wa muda wa CCJ wamekuwa waki-blunder katika almost kila hatua ya kutaka kuandikishwa, na hasa vurugu za juzi kule Mwembeyanga. Wameshindwa kabisa kuzisoma au kuzibaini ghilba za watawala na hivyo kuzikabili.

Na mtu anayespeaheard vigorously hii ‘anti-Chadema, pro-CCJ' campaign humu ndani ni Mwanakijiji, ambaye wakati mwingine anaonekana boring, kutokuwa na nguvu ya hoja, bali lengo moja tu – kuandikishwa kwa CCJ.

To him, Chadema can as well go to hell.

Kwa ujumla hali hii inasikitisha sana kutokea katika JF. Inakatisha tama wachangiaji, hasa wale wa masuala ya ufisadi. It pains a lot. It really does.
 
Tatizo ni kuwa tuna sehemu kubwa kati yetu ambao tunang'ang'ania ushabiki na kuamini kuwa Chadema ndicho chama mbadala. Labda ni ule mvuto wa Dr. Slaa, Chacha Wangwe, Zitto na Kitila. Lakini, hatuwezi kuendelea kuburuzwa kama enzi zile za kuwa Chipukizi wa CCM ambazo tulivutiwa na kunogewa na kusahau kuwa wadadisi na kuhoji mambo. Humu ndani ya JF, kuna ngome kubwa sana inayoilinda Chadema, wala sitashangaa kuwa sehemu kubwa ya wana JF ni washabiki kama si wanachama wa Chadema. Sasa ukiandika kuwakosoa Chadema, fukuto litakalokufuata ni kubwa la kubezana na wala si kujenga hoja au kujibu hoja.
Rev. Kishoka na Mwanakijiji

Kama mnasema Chadema na vyama vya upinzani havijafanya kitu tupeni basi alternatives zenu, tuachane na mfumo huu turudi kwenye chama kimoja au tufanyeje, kuendelea kuwalaumu viongozi walio risk maisha yao na vyama ambavyo at least vina record na kukumbatia chama hewa ambacho hakipo lazima mtakuwa na tatizo kubwa la ki-imani na kuwabadili si kazi ndogo.

Kuhusu ngome ya Chadema humu JF, umeshawahi kujiuliza kwanini Chadema inajadiliwa sana na wala si UDP? kwani Chadema imefanya nini ambacho UDP na vyama vingine havijafanya, au muulize rafiki yako MMKJ kwanini anapost sana mambo ya Chadema na si ya PONA au Jahazi Asilia kwani kaona nini ndani ya Chadema utakapojiuliza maswali haya lazima utakuja na jibu, and the difference will be revealed.
 
Mwanakijiji anadhani CCJ ni kila kitu, kiasi cha kudharau ushauri wa Mzee Mtei. nafikiri ni kiburi tu kuwa CCJ wataleta miujiza within a short time.

Naona Mwanakijiji anapungua uzito wa hoja siku hadi siku.

Tusubiri

Haikuwa lazima kwa CCJ kufuata ushauri wa mzee Mtei.

Kinachoonekana hapa kuwa CCJ si chama cha kutumainiwa kwa vile kwanza hakijasajiliwa, pili hata kikisajiliwa hakitakuwa na tofauti na TLP. Anayoonyesha bwana Kyabo yamekuwa preceded na Bwana Mrema, wenye macho wanaona na wenye masikio watayasikia.
 
Teh teh teh

si mda mrefu mwanakijiji na Kishoka mtaitwa vibaraka/jasusi (The traitors) wa ccm ama lile fagio mrefu wa RA umemifagia kama inavosadikika na baadhi ya wana jf kwamba ulimpitia Zitto.
 
tumeona haya watu walipozungumza dhidi ya CCM wakaaitwa wao ni Chadema, wanapozungumza dhidi ya Chadema wanaitwa wao ni hivi au vile. Maswali ya msingi yanaogopwa kujibiwa. Tunatakiwa kupanga mstari na kujiunga nyuma ya Chadema... tukiuliza ili kiwe nini tunaambiwa "alimradi CCM iondoke madarakani". Tunasema "sawa" halafu ikiondoka madarakani "then what".. hatujibiwi tunaambiwa hilo si tatizo "tuwaondoe kwanza CCM madarakani then tutajua cha kufanya".

Tukisema hiyo si falsafa nzuri tunaambiwa tumefulia kwa sababu ati hatutaki "CCM iondolewe madarakani!".

Tunaambiwa tuungane ili "kuimarisha upinzani". Wasemao hivi wanaona wanasema kitu cha maana lakini hawataki kufikiria wanachokisema. Tunauliza.. msingi wa muungano "uwe nini" wanatuambia "tuiondoe CCM madarakani"! Ala..

Tunarudi tena na kuwaliza haya tumeungana (bila kuvunja chama, kukubaliana itikadi, malengo. n.k) na CCM haiko madarakani.. then what? Wanatuambia "it doesn't matter CCM iondoke kwanza madarakani".

CCJ imekuja na mapendekezo ya nini cha kufanya kikiwa madarakani, of course siyo perfect kama watu wangependa lakini kwa ujasiri zaidi kuliko Chama kingine chochote. Matokeo yake hata nafasi ya kupewa usajili wa kudumu inakataliwa!

Well..

Mimi niko tayari kabisa (na nimekuwa hivi muda mrefu) kuunga mkono Chadema au chama kingine chochote ambacho kitasimamia mabadiliko ya kweli siyo kutuahidi kashfa na takwimu za kashfa! Taifa haliwezi kujengwa kwa kuibua kashfa juu ya kashfa na kutuambia "how bad CCM is".. Tunauliza mtafanya nini? Tunaambiwa.. ...
 
tumeona haya watu walipozungumza dhidi ya CCM wakaaitwa wao ni Chadema, wanapozungumza dhidi ya Chadema wanaitwa wao ni hivi au vile. Maswali ya msingi yanaogopwa kujibiwa. Tunatakiwa kupanga mstari na kujiunga nyuma ya Chadema... tukiuliza ili kiwe nini tunaambiwa "alimradi CCM iondoke madarakani". Tunasema "sawa" halafu ikiondoka madarakani "then what".. hatujibiwi tunaambiwa hilo si tatizo "tuwaondoe kwanza CCM madarakani then tutajua cha kufanya".

Tukisema hiyo si falsafa nzuri tunaambiwa tumefulia kwa sababu ati hatutaki "CCM iondolewe madarakani!".

Tunaambiwa tuungane ili "kuimarisha upinzani". Wasemao hivi wanaona wanasema kitu cha maana lakini hawataki kufikiria wanachokisema. Tunauliza.. msingi wa muungano "uwe nini" wanatuambia "tuiondoe CCM madarakani"! Ala..

Tunarudi tena na kuwaliza haya tumeungana (bila kuvunja chama, kukubaliana itikadi, malengo. n.k) na CCM haiko madarakani.. then what? Wanatuambia "it doesn't matter CCM iondoke kwanza madarakani".

CCJ imekuja na mapendekezo ya nini cha kufanya kikiwa madarakani, of course siyo perfect kama watu wangependa lakini kwa ujasiri zaidi kuliko Chama kingine chochote. Matokeo yake hata nafasi ya kupewa usajili wa kudumu inakataliwa!

Well..

Mimi niko tayari kabisa (na nimekuwa hivi muda mrefu) kuunga mkono Chadema au chama kingine chochote ambacho kitasimamia mabadiliko ya kweli siyo kutuahidi kashfa na takwimu za kashfa! Taifa haliwezi kujengwa kwa kuibua kashfa juu ya kashfa na kutuambia "how bad CCM is".. Tunauliza mtafanya nini? Tunaambiwa.. ...

Mwanakijiji ama kweli unatia mashaka, unajuwa ukifanya mambo kama si wewe huwezi ficha... Sasa inashangaza mno, coz maswali haya nilikuuliza ukasema kuwa kama mkikutana na vizuizi huko mbeleni kuhusiana na usajili,ukasema mambo ya "daraja" sasa naona umebadili mawazo sijui umeota mbawa na unataka kupaa?

Huwezi kuwa na muungano wa kuing'oa ccm halafu kwenye muungano huo muache kujadili kwamba itakuwaje mara baada ya kuing'oa ccm? Sababu za kuungana ni baada ya nia ya kufanya hivyo kuwekwa wazi...Nia ikiwa ni kuiong'oa ccm... Hayo maswali ya "muungane ili iweje" inaonesha wazi kabisa hamna nia ya kuungana na hivyo mnapelekea mashaka mengi....

Mlisema kwamba hamwezi kukosa usajili kwasababu hakuna sababu ya kukosa, nikasisitiza kwamba mnaweza kukosa, ukasema you dont worry about it,bali mna worry on issues baada ya "kusajiliwa" na ukasema kama iki happen kuwa mkaletewa mizwenge kwenye usajili basi mtajenga daraja na mtavuka, sasa naona mnataka kupaa, hamwitaji daraja..... Unajiuliza muungane ili iweje na wakati ilitakiwa mujiulize kama mkikosa usajili itakuwaje?Mbona hukujiuliza kuwa mkikosa usajili itakuwaje na sasa unajiuliza eti muungane ili iweje?ubinafsi tu,sijui mmenyweshwa nini? Eti kuiondoa ccm si priority? Maajabu!

Hata hivyo na nyie ccj bado ni hoax hoax tu,labda na hao kina mzee Mtei na nyie mnajuwa mambo ambayo sisi hatuayajui, mnajuwa i can bet you umaaraufu wa ccj utakwisha kama hakuna hao vigogo wa ccm watakaojitoa, na pia nawashauri kama hamna cha maana cha kuprovide kwenye kuuimarisha upinzani acheni blah blah vyama vingine vyenye kufanya hivyo viendelee kufanya hivyo coz naona sasa haya yote mwishowe yatakuwa kuinufaisha ccm kwa kuwavuruga wananchi bure.

Muda huu si wa kuugawa upinzani, wakati ambapo ni miezi michache imebakia kabla ya uchaguzi mkuu, wengine haya tuliyatabiri lakini hatukujua yangekuja kwa sytle hii, unless proven otherwise,hapo ndo u hoax wa ccj ndipo utakapowekwa wazi.... Coz inashangaza kama huelewi kuwa mara baada ya kuiong'oa ccm si inatakiwa muunde serikali?
 
Mwanakijiji, ndugu yangu CCM itoke kwanza,zaidi ya hapo hamna nyimbo.

itoke ili kiwe nini? hili ni swali ambalo hamtaki kujibu. Tutakuwa ni watu wajinga zaidi duniani kuuondoa chama tawala halatu hatujui tutaweka nini.. remember Somalia? Si walimuangusha Siad Barre? and then what.. Kenya walimuangusha Moi.. then What? Malawi walimuangusha Hastings then what? Zambia walimuangusha Kaunda then what?
 
Back
Top Bottom