Librarian 105
JF-Expert Member
- May 6, 2023
- 239
- 325
USMA walijiandaa zaidi ndani na nje ya uwanja kuikabili YANGA SC, ila YANGA SC wao mbali na kujiandaa kumkabili mwarabu, pia waliweka jitihada zao za ziada kumkomoa SIMBA SC.
Kwa mantiki hii, utani wa jadi wa timu zetu hizi mbili nchini, mara nyingi ni wenye kuumiza upande mmoja au mwingine katika ngazi ya michuano ya kimataifa kutokana na kutambiana na kupigana vijembe zaidi badala ya kuangalia maslahi mapana ya kushinda michuano hii.
Uyanga na usimba, ni vyema ukaishia ndani ya mipaka ya nchi yetu. Huko kwingine bora ukimya ukatawala kuliko kupigana vijembe na nyodo zisizo na manufaa.
Mwisho, kuteleza sio kuanguka, dakika zingine tisini zinafuata ugenini.
Yanga sc wajitathmini kisha kwenda na game plan yenye mikakati bora kuliko mpinzani wake.
Nawasilisha jukwaani.