Mtanzania atengeneza satelaiti

Mtanzania atengeneza satelaiti

Engineer
 

Attachments

  • Screenshot_20240604-200522.jpg
    Screenshot_20240604-200522.jpg
    408.9 KB · Views: 9
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano.

Ni engineer Léonard Shayo ambaye pia ni fundi mitambo wa Azam Media, amefanikiwa kutengeneza satelaiti mahususi kwa ajili ya kukusanya taarifa za hali ya hewa.

Satellite hiyo imefanyiwa majaribio katika mikoa kadhaa na kutoa matokeo chanya.

Kongole Engineer Léonard Shayo

Chanzo: Azam news
Ameassemble vifaa kadhaa na kupata receiver, kutengeneza kunatafsiri pana sana
 
Natamani kujua alifanya majaribio lini ya kuipeleka angani na alifanyia wapi na kwa gharama gani
 
Asije akawa kama wale wanaotengeneza matoy ya
🔹 Ndege

🔹Cartapila

🔹Vituo vya redio

🔹Magari kwa kutumia engine za pikipiki au dizel engine
 
Kaleteni taarifa za kutosha na video ni muhimu pia. Na ikiwezekana atangazwe hadi kwenye taarifa ya habari.

Mlikosea kitu kimoja, siku ya kuzindua hiyo satelite mlitakiwa mrushe tukio laivu ili kuhamasisha wanasayansi wa ndani.

Swali kwenu wataalamu!

1. Je, hiyo satelite imerushwa kwa kutumia mtambo gani?
2. Je, hiyo satelite imerushwa humu humu Tanzania?

Au satelite huwa inarushwa kama drone tu?

Majibu ya kitaalamu tafadhali, sisi ambao hatujui tujue kabla ya kutoa pongezi mana bongo kwa sasa tunachezeana sana. Badala ya kuwa siriasi tunaleta utani huku vitu vizuri tunavitaka. Rejea gari la UDSM na Robot Yunisi
 
Back
Top Bottom