ukweli ni kwamba kuna wageni wanauziwa pass zetu. kwa nini mtaani unakuta wanaigeria kumi wanakaa chumba kimoja na wanajifunza kiswahili cha kuondokea bongo pale uwanja wa ndege, na kuna ma agent ambao wanawatunza muda huo wote baada ya kukatiwa kitu kidogo. kazi ipo na wakuu wanaelewa mpango mzima ndiyo hivyo tena.
Wa-nigeria wameanza kuja bongo juzi tu. Passport za tanzania zimeanza kuuzwa zaidi ya miaka 15 iliyopita.
Nilishuhudia enzi hizo nimeenda uhamiaji kutafuta passport. Waliniagiza documents ambazo ilibidi nisafiri kuzitafuta na nyingine nilitakiwa niende hadi mahakamani zikapigwe muhuri, halafu nilivyoenda uhamiaji nilisimama kwenye foleni ambayo haisogei, nilikua naona wahindi tu wanaingia na kutoka na passport na hawapangi foleni. Siku ya kwanza iliisha sikupata kitu ofisi zikafungwa. Ikabidi kesho yake niende tena niandae na rushwa kwa sababu kiburi changu cha kutaka haki hakikufua dafu mbele ya wale maofisa wa passport.
Kuna kipindi passport zilibadilishwa, sasa huko kwenye kubadilisha passport walikuja wahindi mpaka wenyewe wanaona aibu, hata kiswahili hawajui.
Wa nigeria wakinunua passport ya TZ mara nyingi hawasafirishii madawa ya kulevya, huwa wanazitumia kupata viza especially kuja U.S etc kwa sababu ukiwa mnigeria viza ni ngumu kutoka. Hivyo hawazitumii hovyohovyo hizo passport, wanaweza kuzitumia kwenye ma fraud ambayo haukamatwi hapohapo na kuswekwa ndani.
Wapo wengi wana passport za south afrika, nilishakutana na mmoja anaitwa
Khumalo nikadhani msouth, kumuuliza ananiambia "
my broda dhis is nigerian name" nikaona haina haja ya kubishana nae.
Kuna mmoja alikuwa na jina la kike kabisaa halafu ni mwanaume, hapo nilichoka nao, amefoji passport ya mwanamke.
Halafu m-nigeria hata awe na passport ya TZ kama hana mtu wakumvusha JNIA atakamatwa na hakuna MTZ atakayemwamini mnigeria amfanye punda kwa sababu atakimbia na mzigo na pesa hakuletei ng'o.
Hawa wanaopita JNIA na mzigo mkubwa ni watanzania ambao wanakuwa na watu wao wakuwavusha.