Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,502
- 51,098
Mtalii mmoja raia wa Uingereza, amejirekodi video akifurahia utalii huko Zanzibar.
Katika video hiyo ameonyesha kufurahia uhuru mkubwa alioupata huku Tanzania baada ya kuondoka Uingereza mwanzoni mwa mwezi January mwaka huu na Kuja Tanzania.
Mtalii huyo anasema huku Tanzania hakuna cha social distancing wala measures nyingine strict za kujikinga na korona sana sana alipimwa joto tu airport alipokuwa anaingia nchini.
Ameonekana kuvutiwa na mbinu za medani za rais Magufuli kuwa baada ya kupima mbuzi, mafenesi n. k na kuonekana hivyo vitu vina korona basi akaamua kuwa Korona siyo tatizo kubwa kivile.
Pia mtalii huyo amewashauri walioko kwenye Lockdown huko Uingereza waje Tanzania, amesema kuwa kuondoka kwenye lockdown na kuja ula bata huku Tanzania inawezekana kama yeye alivyofanya!
Hata hivyo wakati watalii wakimiminika nchini, tena wengine kutoka nchi ambazo zimeathurika vibaya kabisa na ugonjwa huu, Serikali yetu haioni haja ya kuwaweka karantini au kuwazuia mpaka hali itakapotengamaa, inazidi kuwakaribisha kwa bashasha na upendo na ukarimu mkubwa!.
Kwa hivi sasa, kuna kirusi kipya cha korona kinachoitesa Afrika ya kusini na Uingereza ambacho wataalamu wanasema ni kikali zaidi ya kile cha awali
Wakati huohuo majirani zetu wa Rwanda wamefunga tena shule na kufanya jitihada za kupunguza mikusanyiko ili kupunguza kuenea kwa kirusi hicho.
Wakati hilo likiendekea serikali ya Tanzania imeendelea kukaa kimya, Hakuna tena utaratibu wa wizara ya Afya kuwapa wananchi mafunzo ya kujikinga na janga hili.
Sasa hivi, hili janga limebaki kila mtu atajijua yeye mwenyewe!
Hata hivyo Watanzania wote siyo wenye ufahamu na masuala haya, na wengine hawaamini kuwa Korona ipo nchini baada ya kuaminishwa na serikali kuwa Korona haipo na hivyo wameacha kabisa kuchukua tahadhari.
Hapa chini ni video ya huyo raia wa uingereza akifurahia uhuru wa kutokuwepo kwa hatua ngumu za kupambana na Corona Tanzania
Katika video hiyo ameonyesha kufurahia uhuru mkubwa alioupata huku Tanzania baada ya kuondoka Uingereza mwanzoni mwa mwezi January mwaka huu na Kuja Tanzania.
Mtalii huyo anasema huku Tanzania hakuna cha social distancing wala measures nyingine strict za kujikinga na korona sana sana alipimwa joto tu airport alipokuwa anaingia nchini.
Ameonekana kuvutiwa na mbinu za medani za rais Magufuli kuwa baada ya kupima mbuzi, mafenesi n. k na kuonekana hivyo vitu vina korona basi akaamua kuwa Korona siyo tatizo kubwa kivile.
Pia mtalii huyo amewashauri walioko kwenye Lockdown huko Uingereza waje Tanzania, amesema kuwa kuondoka kwenye lockdown na kuja ula bata huku Tanzania inawezekana kama yeye alivyofanya!
Hata hivyo wakati watalii wakimiminika nchini, tena wengine kutoka nchi ambazo zimeathurika vibaya kabisa na ugonjwa huu, Serikali yetu haioni haja ya kuwaweka karantini au kuwazuia mpaka hali itakapotengamaa, inazidi kuwakaribisha kwa bashasha na upendo na ukarimu mkubwa!.
Kwa hivi sasa, kuna kirusi kipya cha korona kinachoitesa Afrika ya kusini na Uingereza ambacho wataalamu wanasema ni kikali zaidi ya kile cha awali
Wakati huohuo majirani zetu wa Rwanda wamefunga tena shule na kufanya jitihada za kupunguza mikusanyiko ili kupunguza kuenea kwa kirusi hicho.
Wakati hilo likiendekea serikali ya Tanzania imeendelea kukaa kimya, Hakuna tena utaratibu wa wizara ya Afya kuwapa wananchi mafunzo ya kujikinga na janga hili.
Sasa hivi, hili janga limebaki kila mtu atajijua yeye mwenyewe!
Hata hivyo Watanzania wote siyo wenye ufahamu na masuala haya, na wengine hawaamini kuwa Korona ipo nchini baada ya kuaminishwa na serikali kuwa Korona haipo na hivyo wameacha kabisa kuchukua tahadhari.
Hapa chini ni video ya huyo raia wa uingereza akifurahia uhuru wa kutokuwepo kwa hatua ngumu za kupambana na Corona Tanzania