Uanjua watu wanasemaga vitu bila kujua kuna siku vitakuja kuleta maswali.
Kama kuna mtu anasema Sokoine alikuwa akiwa njiani kuelekea Morogoro, nani alithibitisha kifo cha Sokoine? Kulikuwa na Daktari kwenye ile gari aliyempima na kujua alifia njiani wakienda Morogoro?
Nini ilikuwa sababu ya kumpitisha Morogoro Regional Hospital Ikiwa walikuwa wanajua alifilia njiani hata kabla hajafika Morogoro?
Ni vizuri wakanyoosha maelezo.
Ninachokifahamu mimi, waliompeleka Hospital ya Morogoro walikataa asipimwe kwamba alishakufa. Ni jambo dogo lakini ni vizuri kuliangalia kwa upana. Pale Morogoro hakuna Daktari alimpima Sokoine kuthibitisha amekufa ama la. Dr. Materu, aliyekuwa zamu pale, aliye wapokea hakuruhusiwa ampime.
Kama ni report iliandikwa ilikuwa ni kwa formalities na kutokana na maelezo waliyokuwa wanayapata.
Ninaogopa kusema zaidi kwa hofu ya kuambiwa naandika uchochezi.
Imetosha.