Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Ushauri kwa wapenzi wa upinzani Km mimi, Mhe Mbowe aachie uongozi wa uenyekiti wa chama. Huu mtindo wa kubadilisha gia angani ni ishara mbaya sana kwa chama kikubwa kama Chadema. Mwaka jana Lowasa alikaribishwa kugombea urais kwa gia ya angani hivi hivi na maneno mazuri mengi sana, lakini kama woga wa Chadema kuhusu ukuta wa kesho wangeacha kuandamana tu kupisha hao walinzi wa mipaka ya nchi. Halafu kukawa na mkakati mwingine Km walivyokuwa wameuaminisha umma kuwa ukuta ni operesheni endelevu. Hii ya leo inatia kinyaa na inakera Sana kwa wapenda ukweli na wanaoamini katika mikakati madhubuti.
Nani hapa naongoza kwa kubadili gia angani hana hata miaka miwili magogoni hebu cheki


Before : Serikali yangu itakuwa ya Viwanda
After: Wapinzani ndio wanakwamisha Viwanda
Before : Nitakuwa Rais wa wote
After : Watakao leta fyokofyoko nitawashugulikia
Before: Mimi nimechaguliwa na masikini
After : Serikali yangu haitatoa chakula cha mswada
Before : Walifikiri nitakuwa upande wao
After: Wazee wangu nitawalinda
Before: Mafisadi wamenikimbia
After : Ni maajabu kukutana na Lowassa
Before : Mimi sibagui vyama nataka vifanye siasa walikochaguliwa
After : Hakuna siasa mpaka 2020



Na mengine tumeyaficha kwa aibu
 
Kwani Lowassa ni nani huko chadema??
Halafu familia ya Nyerere inaingiaje?
Wameogopa sasa wanatafuta visababu? Chadema ni chama cha maigizo
 
Mwenyekiti wa chadema ana uwezo mkubwa wa kuendesha biashara, sio chama cha siasa.

Hivi Godless Lema anaendeleaje?

Huyu vipi


Before : Serikali yangu itakuwa ya Viwanda
After: Wapinzani ndio wanakwamisha Viwanda
Before : Nitakuwa Rais wa wote
After : Watakao leta fyokofyoko nitawashugulikia
Before: Mimi nimechaguliwa na masikini
After : Serikali yangu haitatoa chakula cha mswada
Before : Walifikiri nitakuwa upande wao
After: Wazee wangu nitawalinda
Before: Mafisadi wamenikimbia
After : Ni maajabu kukutana na Lowassa
Before : Mimi sibagui vyama nataka vifanye siasa walikochaguliwa
After : Hakuna siasa mpaka 2020
 
Kwani Lowassa ni nani huko chadema??
Halafu familia ya Nyerere inaingiaje?
Wameogopa sasa wanatafuta visababu? Chadema ni chama cha maigizo


Ukuta ulivuta watu kumbe mnaupenda cheki mnavyotoa povu ndoo ya omo mmemeza na dada yako shonza wazee wa slogan chadema lazima mziki wao muucheze si unakumbuka m4c yani (movement for change) mzee wa chato alicheza hiyo bit sasa mpo ukutani.
 
Huyu vipi


Before : Serikali yangu itakuwa ya Viwanda
After: Wapinzani ndio wanakwamisha Viwanda
Before : Nitakuwa Rais wa wote
After : Watakao leta fyokofyoko nitawashugulikia
Before: Mimi nimechaguliwa na masikini
After : Serikali yangu haitatoa chakula cha mswada
Before : Walifikiri nitakuwa upande wao
After: Wazee wangu nitawalinda
Before: Mafisadi wamenikimbia
After : Ni maajabu kukutana na Lowassa
Before : Mimi sibagui vyama nataka vifanye siasa walikochaguliwa
After : Hakuna siasa mpaka 2020

Huyo huyo. Yes. Tunamkubali kwa sasa. Hivyo hivyo.
 
Leo nitaanza bila salamu,
Ndugu wanajamvi, kwa siku za nyuma kidogo, takribani mwaka mmoja uliopita niliwahi kuandika hapa kuwa CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na nikasema katika maneno ya hitimisho la andiko langu hilo kuwa;


Nakumbuka vizuri, niliambulia matusi mengi kama ninavyotaraji hata leo pia. Kama nilivyosema wakati huo nitasema tena leo kuwa WATANZANIA wameshapoteza IMANI na chadema na uongozi wake. Wasomi, wanataaluma, na makundi mengine yenye influence kwenye jamii hawaiungi tena mkono chadema, nimeshangazwa hata bodaboda na machinga nao wanajitenga mbali na chadema.

Waandishi makini wameacha kabisa kuwaunga mkono chadema, hata wale ambao waliwaandika vizuri kwenye social media akina Mwanakijiji, Chahali na hata Pasco wamekuwa wakiwashushua kila uchao juu ya maamuzi yao na uelekeo wao.

Kwa mara nyingine tena, LEO umefanyika uamuzi mwingine wa kuchekesha na wenye kuudhi. Uamuzi unaoendelea kuthibitisha kuwa Uongozi wa CHADEMA umekosa dira, maono na hawana tafakuri sahihi juu ya mabadiliko ya wakati na namna bora ya kuendesha siasa za sasa. Walipodhani kuwa FEDHA zinaweza kuwa THINK TANK ya chama na kusahau BRAINS matokeo yake ndio haya, mnakosa strategic plan na mnaishia kughairisha mikakati bila sababu za msingi zenye kueleweka kwa watu na kupoteza influnce zaidi, actually hata wanachama wanawadharau kwa mwendo huu.

Labda ilikuwa utani, lakini UONGOZI wa chadema wanapaswa kufahamu kuwa Naibu Katibu Mkuu wao na wanachama wao 27 wako korokoroni hivi sasa kwa sababu ya mpango wao wa hovyo. Watu hawa tumaini lao ilikuwa ni kuungwa mkono lakini uongozi wao umewasaliti, umewatanguliza kama CHAMBO then mpango umeahirishwa. Lakini kuna vijana chungu mzima, ambao walikuwa driven na UKUTA wakajikuta wanamtukana Mkuu wa Nchi na Serikali yake nao wananyea debe wakati uongozi wao unaghairisha kiutani utani, opresheni iliowafikisha jela.

Hivi visingizio kuwa familia ya Nyerere imekutana na Lowassa na kumuomba, naomba nisitolee maelezo ila nitampigia simu personally msemaji wa familia hiyo Ndugu Makongoro ili ikiwezekana kesho ama keshokutwa afanye press, au aende Clouds au Efm kuthibitisha kuwa walikutana na Lowassa na kumuomba a-abort mpango mzima.

UKUTA chali, kama nilivyotegemea.

Jioni Njema...!!

kwa hali ilivyo ulipenda kuona watz wenzako wanaumizwa na kuuwawa kisa we upo ccm sasa, we nadhan hata ubunge wako sherekea miaka hii 5 ukapumzike.
 
Kumbe nae anamapungufu bas coment yako ipo upande wa chuki zako za moyoni kwako. Na yeye bora liende tz raha sana.

Huwezi kuijua chuki hadi uwe mwenye chuki! Acha chuki.

Hakuna binadamu asie na mapungufu. Ndio maana unaona wengine wanabadili gia angani, anytime any how na bado huoni wanachemsha.
 
Huwezi kuijua chuki hadi uwe mwenye chuki! Acha chuki.

Hakuna binadamu asie na mapungufu. Ndio maana unaona wengine wanabadili gia angani, anytime any how na bado huoni wanachemsha.
Kwa ulichikiandika hapo jionee ulichikiandika hapo chini kama kweli una maanisha





Mwenyekiti wa chadema ana uwezo mkubwa wa kuendesha biashara, sio chama cha siasa.


Hivi Godless Lema anaendeleaje?
 
Kwa ulichikiandika hapo jionee ulichikiandika hapo chini kama kweli una maanisha





Mwenyekiti wa chadema ana uwezo mkubwa wa kuendesha biashara, sio chama cha siasa.


Hivi Godless Lema anaendeleaje?

Irrelavant na nj sababu ya viroba. Hebu funga uliombee Taifa.
 
Leo sijaona hoja yako Juliana!Ingawa ni kweli Mbowe anawepleka chaka wenzie lakini amefaya vema kutokushindana na dola!Sijamuelewa tu kutaka kuendeleza kwake ukuta mwezi october!Hapa kama amekosa washauri mie nitamshauri aachane na UKUTA, haulipi!Apoe kwanza, homa ya uchguzi iishe na serikali itekeleze majukumu yake then pengine watapata cha kukosoa!Lakini kwa sasa hakuna, na watz hawatawaunga mkonio
Safi sn ,nimependa sn uchambuzi wako.
 
Irrelavant na nj sababu ya viroba. Hebu funga uliombee Taifa.


Lazima upanic unakuja na lugha za ajabu irrevant ni wewe hujui unachokiandika msahaulifu lazima unaswe swala la kufunga wahimize wenzio huko wamuokoe mtukufu asije na kauli mbili mbili mnywa viroba huwa na hasira na lugha zisizo na staha like you!!!!
 
Hata na mimi huwa najiuliza, huyu dada sijui alisahau nini huko Chadema .......... Wenye chama tusaidieni!!
Huyu dada nimemuuliza elimu yake ni ipi na aliisoma wapi (chuo). She is very shallow upstairs! Kama CDM inaweza kusurvive mpaka leo kwa mikikimikiki ya seriali na vyombo vya dola, huwezi kuibeza CDM. Think of the situation CDM ingelikuwa free kufanya siasa bila vitisho , nchi hii ingelikuwa mikononi mwa CDM au at least 2/3 ya wabunge wangelikuwa wake!
 
Kwa nini mnamjibu huyo? hakuna kitu kizuri kama kum-ignore mtu. Mimi humu huwa nachagua wa kumjibu! Kuna "takataka" nyingi sana humu covering all walks of life! Lazima uwe macho unamjibu nani! Mnapoteza muda kwa mtu ambaye ni platform politician!
Cha ajabu umeingia ktk mtego wa juliana bila kujijua maana umesoma thread yake na umesoma maoni ya wachangiaji mwishoni umeingia mwenyewe kuchangia hivyo wewe ni moja ya hao unaowaita all walks of life
 
Cha ajabu umeingia ktk mtego wa juliana bila kujijua maana umesoma thread yake na umesoma maoni ya wachangiaji mwishoni umeingia mwenyewe kuchangia hivyo wewe ni moja ya hao unaowaita all walks of life
Umejuaje kuwa nimesoma contents za thread. Nimemjibu aliyelalamika!
 
Back
Top Bottom