Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Hizo research zako za kuwa machinga na bodaboda wameacha kuiunga mkono CHADEMA ulizifanyia wapi?
Na ulienda kwa hao watu ukiwa katika sura ipi maana asikwambie mtu ile kuwaruhusu machinga warudi kufanya biashara maeneo mliyowakataza kidogo mkarejesha matumaini ila wengi wao bado hawana imani na siasa ya chama chako wewe mtoa uzi.
Kiukweli napenda nikushauri urejee maneno alioyaongea Mbunge wa Chama chako Ndg Bashe alisema serikali inacheza muziki wa CHADEMA so lengo limetimia kwa asilimia nyingi sana nguvu walizotumia serikali kuhakikisha UKUTA never exist ni nyingi sana utadhani walikuwa wanapambana na watu wale wa Uturuki waliotaka kupindua nchi.
Juliana Shonza bado haujakomaa kisiasa kwa hizo tathmini zako zisizo na uhakika. Umeshhakuwa na uhakika wa chakula cha kila siku hapo ulipo hauna kashikashi ya aina yoyote kama ilivyo kwa upinzani ila hayo ulioyaandika wewe yakiandikwa kwa serikali inakuwa ni uchochezi.Ila time will tell
Machinga hawana imani na serikalo tena wala hao bodaboda hawana hiyo imani nanyi tena wanasubiri tu ikifika muda wa kuwahukumu kwenye mabox ya kupigia kura watafanya kile wanachokililia sasa hivi maana wanapitia wakati kgumu sana katika historia ya Tanzania.
Jifikirie upya kabla ya kuja na hizo blabla zako hata kama familia ya Mzee Nyerere hawajaongea na Lowasa ila kwa hatua waliyofikia CHADEMA ni nzuri sana katika kufanya siasa yaani mlikuwa mnawatangaza kwa wananchi bila kupenda katika majukwaa yenu ya siasa wao wapo Indirect kupitia vinywa vya wanasiasa wenu.
Usiwe mbeya sana hayo ya kumpigia simu huyo mtoto wa Mzee Nyerere wala sisi hayatuhusu.
Tunahitaji siasa safi na utawala bora unaofuata sheria na katiba ya nchi .

14089284_1333115990033733_6476826038821972625_n.jpg
 
Ni dhahiri kua viongozi wa sasa wanatakiwa kupumzika na kuwapisha wengine.
 
Hizo research zako za kuwa machinga na bodaboda wameacha kuiunga mkono CHADEMA ulizifanyia wapi?
Na ulienda kwa hao watu ukiwa katika sura ipi maana asikwambie mtu ile kuwaruhusu machinga warudi kufanya biashara maeneo mliyowakataza kidogo mkarejesha matumaini ila wengi wao bado hawana imani na siasa ya chama chako wewe mtoa uzi.
Kiukweli napenda nikushauri urejee maneno alioyaongea Mbunge wa Chama chako Ndg Bashe alisema serikali inacheza muziki wa CHADEMA so lengo limetimia kwa asilimia nyingi sana nguvu walizotumia serikali kuhakikisha UKUTA never exist ni nyingi sana utadhani walikuwa wanapambana na watu wale wa Uturuki waliotaka kupindua nchi.
Juliana Shonza bado haujakomaa kisiasa kwa hizo tathmini zako zisizo na uhakika. Umeshhakuwa na uhakika wa chakula cha kila siku hapo ulipo hauna kashikashi ya aina yoyote kama ilivyo kwa upinzani ila hayo ulioyaandika wewe yakiandikwa kwa serikali inakuwa ni uchochezi.Ila time will tell
Machinga hawana imani na serikalo tena wala hao bodaboda hawana hiyo imani nanyi tena wanasubiri tu ikifika muda wa kuwahukumu kwenye mabox ya kupigia kura watafanya kile wanachokililia sasa hivi maana wanapitia wakati kgumu sana katika historia ya Tanzania.
Jifikirie upya kabla ya kuja na hizo blabla zako hata kama familia ya Mzee Nyerere hawajaongea na Lowasa ila kwa hatua waliyofikia CHADEMA ni nzuri sana katika kufanya siasa yaani mlikuwa mnawatangaza kwa wananchi bila kupenda katika majukwaa yenu ya siasa wao wapo Indirect kupitia vinywa vya wanasiasa wenu.
Usiwe mbeya sana hayo ya kumpigia simu huyo mtoto wa Mzee Nyerere wala sisi hayatuhusu.

Tunahitaji siasa safi na utawala bora unaofuata sheria na katiba ya nchi .
Unadhani kujua kama unaungwa mkono na mtu ama kundi la watu unahitaji research kubwa ya kukodi madokta na maprofesa. Observation ya kawaida kabisa ya macho yako inatosha kukuthibitishia kuwa watu gani uko nao. Machinga walienda kumpokea Magufuli Lumumba wakiwa na mabango yao na wakarudishwa kufanya kazi kwenye maeneo yao na Mkuu wa Nchi akapendekeza itengwe siku na ufanyike utaratibu wa kuwafanya machinga wafanye biashara zao bila usumbufu. Bodaboda wao walitoa na tamko kabisa kuwa hawaiungi mkono CHADEMA, kwa simple Observation hiyo ilitosha kujiridhisha kuwa chadema haiungwi mkono na makundi hayo.

Kuhusu eti chadema wamepata Promo ni wazo la kijinga, yaani hiyo itafanana na kunywa sumu na kunusurika kisha useme nilikuwa nataka nitangazwa kwenye vyombo vya habari nijulikane, sawa utajulikana with very bad reputation, kuwa coward aliyejaribu kujiua, sasa maisha yatakuwa na faida gani..? Itafafa na CUF siku moja wakitulia wasema mgogoro wetu ulitusaidia promo.

Kama walidhani kuwa chadema haisikiki na haijulikani na wakaunda mpango huu ili wapate kick ndio kusema kuwa unathibitisha uzi wangu kuwa chadema kuna ombwe la uongozi, hawana think tank ya kuwashauri strategy za maana za kuwapa kick...this shit demoralize wanachama, then unasema umepata kick, u accept a defeat bila maelezo ya kuonyesha ushujaa wako then unajigamba kuwa umesikika, na unajulikana. Kwani shida ya chadema ni kujulikana???? OMBWE la UONGOZI
 
Cdm inalindwa na kundi moja
Nalo ni lavijana wasio jitambua au wasio penda kutumia ubongo kutathimini mambo,
Wao kufuata mkumbo tu
Sasa ukiona kundi hili linaanza kujitambua polepole basi jua hawa cdm wanapata wakati mgumu sana.

Cdm hawataki kusoma alama za nyakati Magu hawezi poteza muda na watu wasio itakia mema tanzania
Wapo kwa malengo yao binafsi .

Unaacha hoja za maana na kuwatetea Mafisadi,Majizi utegemee kufika mbali!! Hapana hawa wamepotea.
 
Mmeshikwa pabaya mliyoyatarajia yatokee kwa vijana wa watu yameshindikana huku jeshi likicheza mziki wa Chadema bila kupenda na gharama zilizokuwa hazijatarajiwa
 
Leo nitaanza bila salamu,
Ndugu wanajamvi, kwa siku za nyuma kidogo, takribani mwaka mmoja uliopita niliwahi kuandika hapa kuwa CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na nikasema katika maneno ya hitimisho la andiko langu hilo kuwa;


Nakumbuka vizuri, niliambulia matusi mengi kama ninavyotaraji hata leo pia. Kama nilivyosema wakati huo nitasema tena leo kuwa WATANZANIA wameshapoteza IMANI na chadema na uongozi wake. Wasomi, wanataaluma, na makundi mengine yenye influence kwenye jamii hawaiungi tena mkono chadema, nimeshangazwa hata bodaboda na machinga nao wanajitenga mbali na chadema.

Waandishi makini wameacha kabisa kuwaunga mkono chadema, hata wale ambao waliwaandika vizuri kwenye social media akina Mwanakijiji, Chahali na hata Pasco wamekuwa wakiwashushua kila uchao juu ya maamuzi yao na uelekeo wao.

Kwa mara nyingine tena, LEO umefanyika uamuzi mwingine wa kuchekesha na wenye kuudhi. Uamuzi unaoendelea kuthibitisha kuwa Uongozi wa CHADEMA umekosa dira, maono na hawana tafakuri sahihi juu ya mabadiliko ya wakati na namna bora ya kuendesha siasa za sasa. Walipodhani kuwa FEDHA zinaweza kuwa THINK TANK ya chama na kusahau BRAINS matokeo yake ndio haya, mnakosa strategic plan na mnaishia kughairisha mikakati bila sababu za msingi zenye kueleweka kwa watu na kupoteza influnce zaidi, actually hata wanachama wanawadharau kwa mwendo huu.

Labda ilikuwa utani, lakini UONGOZI wa chadema wanapaswa kufahamu kuwa Naibu Katibu Mkuu wao na wanachama wao 27 wako korokoroni hivi sasa kwa sababu ya mpango wao wa hovyo. Watu hawa tumaini lao ilikuwa ni kuungwa mkono lakini uongozi wao umewasaliti, umewatanguliza kama CHAMBO then mpango umeahirishwa. Lakini kuna vijana chungu mzima, ambao walikuwa driven na UKUTA wakajikuta wanamtukana Mkuu wa Nchi na Serikali yake nao wananyea debe wakati uongozi wao unaghairisha kiutani utani, opresheni iliowafikisha jela.

Hivi visingizio kuwa familia ya Nyerere imekutana na Lowassa na kumuomba, naomba nisitolee maelezo ila nitampigia simu personally msemaji wa familia hiyo Ndugu Makongoro ili ikiwezekana kesho ama keshokutwa afanye press, au aende Clouds au Efm kuthibitisha kuwa walikutana na Lowassa na kumuomba a-abort mpango mzima.

UKUTA chali, kama nilivyotegemea.

Jioni Njema...!!

Ningelishangaa sana kama usingelichangia ila leo SALAAM umeweka kando, ila kilichonisikitisha ni kuweka kando KIAPO, unajuhudi kubwa sana kutaka kutokusahaulika na ninadhani siku ulipotoa kiapo THEME haikuwa utakachokisema kwa Ndugu Mnyika, ila ni kuwa nawe umo, hata hili maana naona leo umewaainisha na waandishi unaodhani wakiandika mazuri roho yako ikisuhuzika wote tukupongeze, yawezekana kwa sababu ya taaluma yako ya PHD unayoitafuta inakuaminisha hivyo au sijui nini?, ila kauli kuwa wewe utaongea na msemaji wa familia duh imenishitua maana hata hizo press conference kwa redio unazopendekezeza kuziandaa mhhhhhhhh nilidhani utaniambia wakina BBC, DW, VoA, ndani Radio One, RFA, AZAM kutaja chache zenye wana taaluma( WAHARIRI) tunaowaamini sio hawa wakukutana kwenye uMC wa shoo UCHWARA na kupeana kazi, kwa hili limenifanya niwe na wasi wasi tena juu ya weledi wako na uchambuzi wako wa mambo mazito, yumkini ndio maana uliondoka na wenzako wakaendelea tena kwa weledi mkubwa sana, mimi ningelikushauri wewe jikite kwenye Ubunge wako wa GANDA LA NDIZI, maana kama sio kupokelewa Dodoma aliyekuwa Mwenyekiti wa wakati huo,baada ya kutimuliwa na wenzenu sidhani hata wewe ungelikuwa hapo ulipo,na hii itakusaidia ili kipindi kijacho usimame DEDE sio kutegemea gari la kukuongoza halafu soma hapa chini maana nyie kwa mambo yenu ndio huwa mnasababisha:-

upload_2016-8-31_15-38-22.png


Nakutakia kazi njema katika propaganda zako.
 
CCM hakuna Ombwe la Uongozi...NITAELEZA:

Ukimtathmini Rais Magufuli utaweza kuhitimisha pasi na shaka kwamba Utawala wake unashabihiana mno na utawala wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Karume. Kwa vigezo vyovyote vile vya Utawala na Uongozi,kama alivyo Rais Magufuli, Karume alitawala kwa mkono wa chuma,alitawala kidikteta katika nyanja zote za maisha ya Wazanzibari kisiasa, kiuchumi na kijamii:

Mifano michache Magufuli na Karume wanavyoshabihiana:
  1. Tangu Mapinduzi ya Januari 12, 1964, Zanzibar haikuwa na Katiba wala sheria, bali iliongozwa kwa Amri za Rais(Presidential Decrees), kadri alivyoona inafaa....Rais Magufuli haonekani kujali katiba wala sheria, bali kauli na amri zake ndo zinapaswa kufuatwa, na wasaidizi wake kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali wanasisitiza hilo -tufuate kauli za Rai
  2. Kwa mujibu wa Gazeti la The Tanganyika Standard la 9/3/1968, Karume aliapa kutofanya Uchaguzi wala kuwa na Katiba Kisiwani kwa miaka 50 tangu 1964 - 2014 kwa madai kwamba Chaguzi zote ni vyombo vya mabeberu kuwakandamiza wananchi.....Rais Magufuli amepiga marufuku vyama vya siasa na wanasiasa kufanya kazi zao tangu sasa 2016 - 2020 kwa madai kwamba vinamzuia kufanya kazi yake ya Urais; mashaka ni makubwa sasa miongoni mwa wafuatiliaji wa siasa kwamba Uchaguzi Mkuu wa 2020 unaweza kufutwa kwa madai kwamba hali ya Usalama itakuwa hairuhusu.
  3. Wakati wa Karume, raia au kiongozi yeyote aliyelalamika au kumkosoa Karume, hata juu ya upungufu wa chakula tu, aliitwa mchochezi na adui wa Mapinduzi na hivyo mhaini....nyakati hizi za Magufuli, raia yeyote, viongozi wa upinzani, na chombo chochote cha habari wanaonekana kukosoa, kujadili au kuhoji utendaji wa serikali ya Magufuli wanaitwa wachochezi, adui wa kauli mbiu ya Hapa Kazi tu na hivyo wanakamatwa na kushikiliwa siku kadhaa kabla ya kufikishwa mahakamani na kufungiwa/kutishiwa kufungiwa biashara zao.
  4. Enzi za Karume, nduguyo akigongewa mlango usiku na kutakiwa kwa mahojiano na serikali usingemwona tena milele....wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM,July mwaka huu, Rais Magufuli alizungumza waziwazi kuwa yeye hana uvumilivu wa kukosolewa na kwamba wote ambao watathubutu kumpinga "watapotezwa" . Amesikika pia akisema yeye hajaribiwi na wote watakaothubutu kumpinga "atawashughulikia" kwa nguvu zote.
  5. Wakati wa Karume, mfumo wa mahakama wa kawaida ulipigwa marufuku. October 1966, Rais alijipa madaraka ya kuteua mahakama maalumu za kusikiliza makosa ya kisiasa kama vile uhaini, uhujumu uchumi na ubadhirifu wa mali ya umma; mahakama hizi hazikufungwa na kanuni zozote katika kusikiliza kesi, huduma za kisheria kwa watuhumiwa zilifutwa na mawakili kupigwa marufuku Zanzibar......nyakati hizi, Magufuli ameunda Mahakama Maalum ya "Mafisadi", na bila shaka lengo lake hasa ni kudhibiti raia na wanasiasa wa upinzani watakaothubutu kumkosoa.
  6. Mwaka 1971, katikati ya baa la njaa Visiwani humo, Karume alipiga marufuku uagizaji wa chakula - mchele, sukari, na unga wa ngano kutoka nje, akisisitiza kuwa Zanzibar ilikuwa na uwezo wa kujitegemea kwa chakula....miezi michache iliyopita, Magufuli alipiga marufuku uagizaji wa sukari kutoka nje, akidai kwamba nchi ilikuwa na uwezo wa kuzalisha sukari ya kutosha.
  7. Kwa hofu ya jamii ya Kizanzibari kufikiwa na fikra na mawazo mapya ya maendeleo, Karume alipiga marufuku vijana wa Kizanzibari kwenda nje kwa masomo ya elimu ya juu ikiwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; alipiga pia marufuku Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar....hapa tumeona jinsi Utawala wa Magufuli unavyosumbuka sasa kudhibiti taratibu za vijana kujiunga na vyuo vikuu pamoja na kuwaondosha vijana ambao tayari wako masomoni kwa visingizio kwamba hawana sifa; pia amezuia Bunge kuoneshwa LIVE!
Kwa hakika Rais Karume alitawala kwa hofu na vitisho visivyomithilika kwa wapinzani na wakosoaji wake, mara nyingi pia akimtisha hata Nyerere. Ya Magufuli tunaona dalili ya hali tete sana huko mbele ya safari, THE WRITINGS ARE ALREADY ON THE WALL FOR EVERYONE TO SEE.

NB.
Simulizi juu ya Utawala wa Karume zapatikana katika maandishi ya wachambuzi mashuhuri wa siasa za Zanzibar kama vile Prof.Issa Shivji, Joseph Mihangwa na Mwanaharakati Yericko Nyerere.
 
Mbowe alikuwa anaitafuta kick kaipata, amewaacha akina lissu na majeraha.
 
CCM hakuna Ombwe la Uongozi...NITAELEZA:

Ukimtathmini Rais Magufuli utaweza kuhitimisha pasi na shaka kwamba Utawala wake unashabihiana mno na utawala wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Karume. Kwa vigezo vyovyote vile vya Utawala na Uongozi,kama alivyo Rais Magufuli, Karume alitawala kwa mkono wa chuma,alitawala kidikteta katika nyanja zote za maisha ya Wazanzibari kisiasa, kiuchumi na kijamii:

Mifano michache Magufuli na Karume wanavyoshabihiana:
  1. Tangu Mapinduzi ya Januari 12, 1964, Zanzibar haikuwa na Katiba wala sheria, bali iliongozwa kwa Amri za Rais(Presidential Decrees), kadri alivyoona inafaa....Rais Magufuli haonekani kujali katiba wala sheria, bali kauli na amri zake ndo zinapaswa kufuatwa, na wasaidizi wake kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali wanasisitiza hilo -tufuate kauli za Rai
  2. Kwa mujibu wa Gazeti la The Tanganyika Standard la 9/3/1968, Karume aliapa kutofanya Uchaguzi wala kuwa na Katiba Kisiwani kwa miaka 50 tangu 1964 - 2014 kwa madai kwamba Chaguzi zote ni vyombo vya mabeberu kuwakandamiza wananchi.....Rais Magufuli amepiga marufuku vyama vya siasa na wanasiasa kufanya kazi zao tangu sasa 2016 - 2020 kwa madai kwamba vinamzuia kufanya kazi yake ya Urais; mashaka ni makubwa sasa miongoni mwa wafuatiliaji wa siasa kwamba Uchaguzi Mkuu wa 2020 unaweza kufutwa kwa madai kwamba hali ya Usalama itakuwa hairuhusu.
  3. Wakati wa Karume, raia au kiongozi yeyote aliyelalamika au kumkosoa Karume, hata juu ya upungufu wa chakula tu, aliitwa mchochezi na adui wa Mapinduzi na hivyo mhaini....nyakati hizi za Magufuli, raia yeyote, viongozi wa upinzani, na chombo chochote cha habari wanaonekana kukosoa, kujadili au kuhoji utendaji wa serikali ya Magufuli wanaitwa wachochezi, adui wa kauli mbiu ya Hapa Kazi tu na hivyo wanakamatwa na kushikiliwa siku kadhaa kabla ya kufikishwa mahakamani na kufungiwa/kutishiwa kufungiwa biashara zao.
  4. Enzi za Karume, nduguyo akigongewa mlango usiku na kutakiwa kwa mahojiano na serikali usingemwona tena milele....wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM,July mwaka huu, Rais Magufuli alizungumza waziwazi kuwa yeye hana uvumilivu wa kukosolewa na kwamba wote ambao watathubutu kumpinga "watapotezwa" . Amesikika pia akisema yeye hajaribiwi na wote watakaothubutu kumpinga "atawashughulikia" kwa nguvu zote.
  5. Wakati wa Karume, mfumo wa mahakama wa kawaida ulipigwa marufuku. October 1966, Rais alijipa madaraka ya kuteua mahakama maalumu za kusikiliza makosa ya kisiasa kama vile uhaini, uhujumu uchumi na ubadhirifu wa mali ya umma; mahakama hizi hazikufungwa na kanuni zozote katika kusikiliza kesi, huduma za kisheria kwa watuhumiwa zilifutwa na mawakili kupigwa marufuku Zanzibar......nyakati hizi, Magufuli ameunda Mahakama Maalum ya "Mafisadi", na bila shaka lengo lake hasa ni kudhibiti raia na wanasiasa wa upinzani watakaothubutu kumkosoa.
  6. Mwaka 1971, katikati ya baa la njaa Visiwani humo, Karume alipiga marufuku uagizaji wa chakula - mchele, sukari, na unga wa ngano kutoka nje, akisisitiza kuwa Zanzibar ilikuwa na uwezo wa kujitegemea kwa chakula....miezi michache iliyopita, Magufuli alipiga marufuku uagizaji wa sukari kutoka nje, akidai kwamba nchi ilikuwa na uwezo wa kuzalisha sukari ya kutosha.
  7. Kwa hofu ya jamii ya Kizanzibari kufikiwa na fikra na mawazo mapya ya maendeleo, Karume alipiga marufuku vijana wa Kizanzibari kwenda nje kwa masomo ya elimu ya juu ikiwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; alipiga pia marufuku Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar....hapa tumeona jinsi Utawala wa Magufuli unavyosumbuka sasa kudhibiti taratibu za vijana kujiunga na vyuo vikuu pamoja na kuwaondosha vijana ambao tayari wako masomoni kwa visingizio kwamba hawana sifa; pia amezuia Bunge kuoneshwa LIVE!
Kwa hakika Rais Karume alitawala kwa hofu na vitisho visivyomithilika kwa wapinzani na wakosoaji wake, mara nyingi pia akimtisha hata Nyerere. Ya Magufuli tunaona dalili ya hali tete sana huko mbele ya safari, THE WRITINGS ARE ALREADY ON THE WALL FOR EVERYONE TO SEE.

NB.
Simulizi juu ya Utawala wa Karume zapatikana katika maandishi ya wachambuzi mashuhuri wa siasa za Zanzibar kama vile Prof.Issa Shivji, Joseph Mihangwa na Mwanaharakati Yericko Nyerere.
yote haya yanakuja baada ya MBOWE kubadili gea angani? mpigeni mawe MBOWE ndiye aliyakatiza mizuka yenu
 
Back
Top Bottom