Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Mmeshikwa pabaya mliyoyatarajia yatokee kwa vijana wa watu yameshindikana huku jeshi likicheza mziki wa Chadema bila kupenda na gharama zilizokuwa hazijatarajiwa
Hivi jamaa huoni aibu kuandika hivi? Aliyetaka kumwaga damu nani Kama si nyinyi. Ukuta upo palepale! Kumbe mnawadanganya wenzenu. Serikali hii haiishii kwa waandamanaji bali mpaka kwa waliohamasisha maandamano. Viongozi wameona na wao watakumbwa na dhoruba wameaharisha.
 
Dada chuki ni mbaya sana katika maisha inakosesha baraka Na mafanikio umeondoka chadema waache chadema na mambo yao amani ya nchi aiwezi kuletwa Na ccm Bali pande zote mbili za upinzani Na watawala hekima ni Bora kuliko Mali nawapongeza chadema kwa kutumia hekima
Aibu tu zimewajaa!
 
Hivi wewe si ndio ulikuja na kipeperushi chako humu ukitaka watu wapigwe sijui pigo takatifu Mods wakaishia kuufutilia mbali ,
kumbe ulikuwa umejitega ukitegemea kesho watu watapigwa eeh ? Hongereni sana ,
Inawezekana Chadema kuna ombwe la uongozi ila kama ndio hivi kuja na mkakati kama wa ukuta nakuitingisha serikali nzima wacha hilo ombwe lidumu milele.


Halafu naomba kuuliza hivi una mume ??
 
Leo sijaona hoja yako Juliana!Ingawa ni kweli Mbowe anawepleka chaka wenzie lakini amefaya vema kutokushindana na dola!Sijamuelewa tu kutaka kuendeleza kwake ukuta mwezi october!Hapa kama amekosa washauri mie nitamshauri aachane na UKUTA, haulipi!Apoe kwanza, homa ya uchguzi iishe na serikali itekeleze majukumu yake then pengine watapata cha kukosoa!Lakini kwa sasa hakuna, na watz hawatawaunga mkonio
Mbona siku zote mlikuwa mnang'ang'ana, UKUTA upo palepale. Tuliwashauri, mkashupaza shingo. Siku ya mwisho serikali ikawa ngangari kama serikali yoyote imara inavyopaswa kuwa, mnajifanya eti mmeharisha. Eti mnampongeza Mbowe kwa kuhepusha vurugu!
 
Kwani mlipokuwa mnang'aka ukuta upo pale pale hamkulijua hilo la damu kumwagika? Mliombwa na viongozi wa dini mkagoma, mkidhani serikali itawaogopa wasaliti wa taifa. Hakuna mchezo huo. Tushirikiane kujenga nchi huu ukibaraka wa mataifa ya magharibi tuachane nao hauna tija kwa taifa.

Huo ukibaraka unaosema unaushahidi nao au ni hisia zako tu!
 
Hivi hizi siasa za nchi yetu sizitakagi, si ccm wala upinzani wote ni walewale , leo ukiwa chama A Utakiponda sana chama B , kesho ukihamia chama B utakisifia na kukiponda chama A, sasa ndo siasa gani hizi jamaniiiii, sisi sote ni ndugu na tunategemeana kwa nini tusisikilizane?? MUNGU AILINDE TANZANIA YETU .
 
Yaani wewe umpigie simu makongoro? Kama nani wewe? Duu
 
Hivi jamaa huoni aibu kuandika hivi? Aliyetaka kumwaga damu nani Kama si nyinyi. Ukuta upo palepale! Kumbe mnawadanganya wenzenu. Serikali hii haiishii kwa waandamanaji bali mpaka kwa waliohamasisha maandamano. Viongozi wameona na wao watakumbwa na dhoruba wameaharisha.
Aibu itoke wapi wakati polisi walikuwa wanalala na viatu wapo attention mpaka vituo vya redio vinafungia bila sababu za maana hapo unaona nani kaabika..mkubali msumali umeingia Tundu linalouma
 
Yaani wewe umpigie simu makongoro? Kama nani wewe? Duu
Kwani Makongoro anapigiwa simu na nani.. ?
Lakini pia kuna utofauti mkubwa kati yangu na wewe. Wewe ni nobody mimi ni somebody, inatosha hiyo kuwa tofauti inayoniwezesha simu yangu kuthaminiwa na kupokelewa...
 
Mimi sio mwanasiasa ila kwa hili pambano lilivyokuwa linaendelea ninaipa chadema ushindi, wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa na sikujua kama inaogopwa namna hiyo kiasi cha kupelekea serekali kutumia gharama kubwa namna hiyo...
 
Kwani Makongoro anapigiwa simu na nani.. ?
Lakini pia kuna utofauti mkubwa kati yangu na wewe. Wewe ni nobody mimi ni somebody, inatosha hiyo kuwa tofauti inayoniwezesha simu yangu kuthaminiwa na kupokelewa...
...ona sasa mnavyokuwa na madharau mnapojiona mna madaraka....wewe wajiona somebody kwa nani??...kwa unaowavulia ama?...acha madharau mama....ukidharau jua kua nawe waweza kudharauliwa....kiongozi gani wewe unayedharau wengine??....ama ndio mnavyojengwa muwe??....
 
Wakati watu wakiitafuta amani kwa taabu kubwa, kuna watu waliisubiri shari kwa hamu kubwa.

Nadhani walipenda kusikia maafa, vurugu nk

Mmoja wapo ni huyu Juliana Shonza mwenye mada chochezi hapo chini ambaye hajafurahishwa kabisa na habari ya kusitisha maandamano

Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi
Huyo haujamsoma vzuri. Hafurahii kuahirishwa wala hashangilii kiuchumia tumbo kama baadhi yenu mnavyoshangilia kiushabiki wa mpira bila kujenga hoja humu jf. Yeye kapigilia msumari palepale kwenye kizungumkuti cha unafiki wa Mwenyikiti kubadili gia angani. Hakuna msaada wowote unaotolewa na chama kwa viongozi wanaonyea debe kwa sasa, pia wasiweza kugetoa msaada wowote kwa watu ambao wangeshindwa kutii mamlaka,wakaenda kuandamana. Maandamano hayo, ambayo viongozi wanayanadi kuwa ya amani. Kiuhalisia siyo ya amani kwakuwa hayana ulinzi na baraka za serikali na jeshi la polisi. Majanga ambayo yanagesababishwa na maandamano hayo, hao viongozi wasingesimama siku za usoni kuyatolea maelezo yoyote ya maana dunia ya wapenda amani ikawaelewa, ndiyomaana wamejikinga kwa shuka la viongozi wa dini,wameona.
Hivi ninyi washabiki, mambo yote yaliyosemwa kwa ufafanuzi mkubwa na kipenzi cha wanamageuzi, Dr Slaa,wakati anajiuzuru kwamba hawezi kumeza matapishi yake na mambo yote machafu yaliyotendeka Chadema wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu, mnadhani ule ni uzushi ama utani?
Hadi leo ni kiongozi ama mfuasi gani aliyesimama kukanusha kisayansi akaeleweka? Mtaje na umnukuu alichokisema,ili tubadilishane mawazo tukubaliane.
Wengine kuanzia hapo tukajua kuwa tatizo limeshaingia upinzani na kamwe hawawezi kuja kujiweka sawa kwa chama kilekile na viongozi walewale.
Watu wanapenda upinzani kwa kuwa upinzani ni kioo cha kurekebishia utawala. Lakini siyo upinzani wenu huu wa kuzomea na kutukana bila kujenga hoja,hamtafika popote. Nadhani mpinzani mzuri atakayeweza kuungwamkono na wapenda mageuzi wa kweli asitokane na hilo genge la wachumia tumbo, awe mtu mpya na aanzishe chama kipya chenye sera mpya,ambazo ukizipima utaziona kuwa hizi kweli ni sera bora zinazokosoa na hata kama kitashika hatamu ya madaraka kinaweza kutuletea maendeleo tunayoyataka, kiongozi huyo ataungwa mkonosana, kwa kuwa upinzani si uandui bali ni ushindani wa hoja kwa ajili ya kujenga maendeleo ya nchi.
 
Mleta bandiko ni Mkuu wa Wilaya? Ni bora ashauriwe kutumia anonymous ID ili angalau aweze kuheshimika na wananchi wake wote kikamilifu. Bila shaka kazi hiyo inahitaji staha kiasi fulani.
 
Ni kweli CHADEMA wamekosa uongozi na umakini kwa sababu mtu kama huyu mleta mada alipaswa alalamikiwe na viongozi wa chadema kwani ni zaidi ya mchochezi.

Mleta mada ni mtu wa ajabu sana anayefikiri mchuano utakaofanyika kati ya CHADEMA na JWTZ, FFU, Magereza, JKT na vikosi vingine maalum ni kama mechi ya simba na Yanga wanaocheza kwa kutumia mpira mmoja.
Mleta mada anasahau kuwa Chadema hawajawahi kufanya fujo kwenye maandamano lakini wamekua wakipoteza watu wao na kwa sasa wameona hali inaweza kuwa ni mbaya na msiba mkubwa kwa taifa ambao utaacha uadui mkubwa kati miongoni mwa watanzania.

Hawa vijana wa CCM ni waajabu sana ,kwa sasa ndio wanaochochea maandamano. Na walikua wanayasubiri kwa ham kubwa ili waone taifa likinuka damu. Na kuhakikishia wewe mleta mada risasi zikiwaua watu mamia ,maelfu ujue ndio laana ya nchi hiyo.
Damu ina tabia ya kuongeza unasiri na visasa.
Ni aibu kubwa kabisa kwa mtu na akili zake tena msomi kushabikia maandalizi ya kuua watu. Huu ni Ujinga mkubwa kupita maelezo. Hata kama ni siasa za kufukuzwa kwenye chama sio hivyo. Hivi vyama vimeanzishwa na watu sio vyama vya kimungu mpaka mtu unahamasisha mauaji na chuki kwa kiwango hiki.
Ninaimani waliokuwa wanaiunga mkono CCM sio zaidi ya 52% kwa mwaka jana. Afrika na Tanzania hakuna uchaguzi huru na wa haki kwa kiwango cha chama tawala kushinda kihalali kwa 58% hapo maguvu ya dola na kila aina ya uchafuzi ni lazima ufanyike kwenye nchi changa kidemokrasia. Kwa hiyo baada ya uchaguzi tulipaswa kufanya juhudi za kuwaunganisha hawa watu ambao wanaonekana walikua na nguvu zinazolingana japo mmoja alikua anatokana chama dola na mwingine upinzani.
Sio busara kwa vijana wa CCM kuendeleza zile hulka za kupata madaraka kwa kupiga watu na kujenga chuki.
Kama mnataka kuheshimika ni lazima muheshimu wengine.
CCM ndio walio na dhamana ya amani ya nchi hii lakini cha ajabu nao wamekua ndio wanaotoa matamko na lugha zisizo na staha kwa watu wengine. Mara vilaza ,nyumbu, kushikishwa ukuta, kushughulikiwa na wafungwa gerezani, majipu, mafisadi,majizi n.k. Huku ni kujenga uhalali wa kuwachukia wengine bila sababu za kisheria.
Siasa za kupata umaarufu kwa kujenga chuki kwa wengine ni hatari sana.
Naamini mwaka kesho Uchaguzi wa CCM utakua wa kutisha kama hawa vijana hawatafundwa na kuwa wazalendo waachane na vita ya madaraka yatokanayo na chuki.

Nilitegemea kuwasikia wanaCCM wapenda amani wakijitokeza na kumpongeza Mbowe na Chama chake kwa kuepusha mauaji na vurugu ambazo zingeweza kutokea lakini badala yake wanajitokeza na kuonyesha wazi kutofurahishwa na hatua ya chadema ya kusitisha maandamana.
Hivi inawezekana kweli kwa binadamu kufurahia mwenzako akipigwa risasi kwa kuvaa tisheti na kushika bendera mkononi tu. Ajabu kabisa.!!
Usifikiri askari aliyekua amemuua Mwangosi hata kama ataachiwa huru ataishi kwa furaha kila anapokumbuka tukio la kumtoa mtu utumbo akiwa ameshika kalamu na karatasi tu. Very sad kwa msomo kama mleta mada kufurahia maandamano ya kumpinga Rais wa nchi. Huyu mleta mada hafai hata ndani ya CCM. Ni mtu wa chuki na mchochezi aliyepitiliza. Angalieni mwinyi anavyoishi maisha marefu na ya amani kwa upendo wake kwa watanzania. Chuki ni sumu mbaya sana kwenye maisha ya binadamu. Kujito kwa Dr. Slaa chadema ni hiyari yake alibembelezwa sana akakataa sasa kuendeleza siasa zake za chuki kwa utawala wa JK na kuhamasisha watu kuandamania na kuua itakua sio kuwatendea watanzania haki. Amejitoa basi . Tangu enzi za kudai uhuru watu walitofautiana na wakatengana kisiasa na baada ya uhuru pia mambo hayo yapo mpaka leo. Kudanganya watu eti kitakuja chama chenye mwenyekiti anayeongoza kwa mfano ambao hata mbinguni haupo ni unafiki ,uongo na upotoshaji. Tofauti ndani ya vyama hazikuanza leo na hazitaisha leo. Ishu sio Mbowe wala Lowasa, wala Slaa . Ishu ni wanasiasa wasaka tonge kujichomeka ndani ya vyama kutumikia chama tawala kwa ahadi ya vyeo ambavyo ndani ya chama tawala vinapatikana kwa mamlaka waliyopewa na katiba. Ni rahisi sana kuhama upinzani kuliko kuhama CCM kwenda upinzani pasipo na vyeo kama Ukuu wa Wilaya,uRC, ubalozi,uwaziri, ukuu wa idara na mashirika mbalimbali tena kwa mishahara minono. Upinzani hakuna kitu zaidi ya kuwekwa mahabusu makesi kila kukicha.
Ukiona mtu ametoka CCM na kwenda upinzani ujue amejitolea kweli kweli lakini ukiona mtu ametoka Upinzani na kurudi CCM ujue amechoka kuishi maisha magumu.

Nawapongeza wanaChadema kwa kuamua kuachana na maandamano na kulinda amani ya nchi yetu. Nilikua nayapinga sana haya maandano mwanzo mwisho na sasa yameahirishwa nawaunga mkono viongozi wa CHADEMA kwani kupingana na dola sio jambo la busara. Siasa nzuri ni mazunguzo na sio nguvu ,matusi na vurugu.
Big up Mbowe kwa kuepusha shari.
Nawaomba wale wote wanaojua umuhimu wa amani wajitokeze kumuunga mkono Mbowe.
Pongezi pia kwa mh. Rais kwa kujitokeza na kueleza furaha yako ya kukutana na kushikana mkono na Mh. Lowasa , umeonyesha kuwa unajali umoja na upendo wa watanzania pamoja na ukweli kuwa wafia vyama kama mleta mada hupenda kupandikiza chuki kuliko kujenga amani.
 
Huyo haujamsoma vzuri. Hafurahii kuahirishwa wala hashangilii kiuchumia tumbo kama baadhi yenu mnavyoshangilia kiushabiki wa mpira bila kujenga hoja humu jf. Yeye kapigilia msumari palepale kwenye kizungumkuti cha unafiki wa Mwenyikiti kubadili gia angani. Hakuna msaada wowote unaotolewa na chama kwa viongozi wanaonyea debe kwa sasa, pia wasiweza kugetoa msaada wowote kwa watu ambao wangeshindwa kutii mamlaka,wakaenda kuandamana. Maandamano hayo, ambayo viongozi wanayanadi kuwa ya amani. Kiuhalisia siyo ya amani kwakuwa hayana ulinzi na baraka za serikali na jeshi la polisi. Majanga ambayo yanagesababishwa na maandamano hayo, hao viongozi wasingesimama siku za usoni kuyatolea maelezo yoyote ya maana dunia ya wapenda amani ikawaelewa, ndiyomaana wamejikinga kwa shuka la viongozi wa dini,wameona.
Hivi ninyi washabiki, mambo yote yaliyosemwa kwa ufafanuzi mkubwa na kipenzi cha wanamageuzi, Dr Slaa,wakati anajiuzuru kwamba hawezi kumeza matapishi yake na mambo yote machafu yaliyotendeka Chadema wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu, mnadhani ule ni uzushi ama utani?
Hadi leo ni kiongozi ama mfuasi gani aliyesimama kukanusha kisayansi akaeleweka? Mtaje na umnukuu alichokisema,ili tubadilishane mawazo tukubaliane.
Wengine kuanzia hapo tukajua kuwa tatizo limeshaingia upinzani na kamwe hawawezi kuja kujiweka sawa kwa chama kilekile na viongozi walewale.
Watu wanapenda upinzani kwa kuwa upinzani ni kioo cha kurekebishia utawala. Lakini siyo upinzani wenu huu wa kuzomea na kutukana bila kujenga hoja,hamtafika popote. Nadhani mpinzani mzuri atakayeweza kuungwamkono na wapenda mageuzi wa kweli asitokane na hilo genge la wachumia tumbo, awe mtu mpya na aanzishe chama kipya chenye sera mpya,ambazo ukizipima utaziona kuwa hizi kweli ni sera bora zinazokosoa na hata kama kitashika hatamu ya madaraka kinaweza kutuletea maendeleo tunayoyataka, kiongozi huyo ataungwa mkonosana, kwa kuwa upinzani si uandui bali ni ushindani wa hoja kwa ajili ya kujenga maendeleo ya nchi.
Nashukuru kwa ufafanuzi murua, mimi nadhani wanafahamu ila wanajifanyisha tu.
 
Back
Top Bottom