Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi

Ni kweli CHADEMA wamekosa uongozi na umakini kwa sababu mtu kama huyu mleta mada alipaswa alalamikiwe na viongozi wa chadema kwani ni zaidi ya mchochezi.

Mleta mada ni mtu wa ajabu sana anayefikiri mchuano utakaofanyika kati ya CHADEMA na JWTZ, FFU, Magereza, JKT na vikosi vingine maalum ni kama mechi ya simba na Yanga wanaocheza kwa kutumia mpira mmoja.
Mleta mada anasahau kuwa Chadema hawajawahi kufanya fujo kwenye maandamano lakini wamekua wakipoteza watu wao na kwa sasa wameona hali inaweza kuwa ni mbaya na msiba mkubwa kwa taifa ambao utaacha uadui mkubwa kati miongoni mwa watanzania.

Hawa vijana wa CCM ni waajabu sana ,kwa sasa ndio wanaochochea maandamano. Na walikua wanayasubiri kwa ham kubwa ili waone taifa likinuka damu. Na kuhakikishia wewe mleta mada risasi zikiwaua watu mamia ,maelfu ujue ndio laana ya nchi hiyo.
Damu ina tabia ya kuongeza unasiri na visasa.
Ni aibu kubwa kabisa kwa mtu na akili zake tena msomi kushabikia maandalizi ya kuua watu. Huu ni Ujinga mkubwa kupita maelezo. Hata kama ni siasa za kufukuzwa kwenye chama sio hivyo. Hivi vyama vimeanzishwa na watu sio vyama vya kimungu mpaka mtu unahamasisha mauaji na chuki kwa kiwango hiki.
Ninaimani waliokuwa wanaiunga mkono CCM sio zaidi ya 52% kwa mwaka jana. Afrika na Tanzania hakuna uchaguzi huru na wa haki kwa kiwango cha chama tawala kushinda kihalali kwa 58% hapo maguvu ya dola na kila aina ya uchafuzi ni lazima ufanyike kwenye nchi changa kidemokrasia. Kwa hiyo baada ya uchaguzi tulipaswa kufanya juhudi za kuwaunganisha hawa watu ambao wanaonekana walikua na nguvu zinazolingana japo mmoja alikua anatokana chama dola na mwingine upinzani.
Sio busara kwa vijana wa CCM kuendeleza zile hulka za kupata madaraka kwa kupiga watu na kujenga chuki.
Kama mnataka kuheshimika ni lazima muheshimu wengine.
CCM ndio walio na dhamana ya amani ya nchi hii lakini cha ajabu nao wamekua ndio wanaotoa matamko na lugha zisizo na staha kwa watu wengine. Mara ****** ,nyumbu, kushikishwa ukuta, kushughulikiwa na wafungwa gerezani, majipu, mafisadi,majizi n.k. Huku ni kujenga uhalali wa kuwachukia wengine bila sababu za kisheria.
Siasa za kupata umaarufu kwa kujenga chuki kwa wengine ni hatari sana.
Naamini mwaka kesho Uchaguzi wa CCM utakua wa kutisha kama hawa vijana hawatafundwa na kuwa wazalendo waachane na vita ya madaraka yatokanayo na chuki.

Nilitegemea kuwasikia wanaCCM wapenda amani wakijitokeza na kumpongeza Mbowe na Chama chake kwa kuepusha mauaji na vurugu ambazo zingeweza kutokea lakini badala yake wanajitokeza na kuonyesha wazi kutofurahishwa na hatua ya chadema ya kusitisha maandamana.
Hivi inawezekana kweli kwa binadamu kufurahia mwenzako akipigwa risasi kwa kuvaa tisheti na kushika bendera mkononi tu. Ajabu kabisa.!!
Usifikiri askari aliyekua amemuua Mwangosi hata kama ataachiwa huru ataishi kwa furaha kila anapokumbuka tukio la kumtoa mtu utumbo akiwa ameshika kalamu na karatasi tu. Very sad kwa msomo kama mleta mada kufurahia maandamano ya kumpinga Rais wa nchi. Huyu mleta mada hafai hata ndani ya CCM. Ni mtu wa chuki na mchochezi aliyepitiliza. Angalieni mwinyi anavyoishi maisha marefu na ya amani kwa upendo wake kwa watanzania. Chuki ni sumu mbaya sana kwenye maisha ya binadamu. Kujito kwa Dr. Slaa chadema ni hiyari yake alibembelezwa sana akakataa sasa kuendeleza siasa zake za chuki kwa utawala wa JK na kuhamasisha watu kuandamania na kuua itakua sio kuwatendea watanzania haki. Amejitoa basi . Tangu enzi za kudai uhuru watu walitofautiana na wakatengana kisiasa na baada ya uhuru pia mambo hayo yapo mpaka leo. Kudanganya watu eti kitakuja chama chenye mwenyekiti anayeongoza kwa mfano ambao hata mbinguni haupo ni unafiki ,uongo na upotoshaji. Tofauti ndani ya vyama hazikuanza leo na hazitaisha leo. Ishu sio Mbowe wala Lowasa, wala Slaa . Ishu ni wanasiasa wasaka tonge kujichomeka ndani ya vyama kutumikia chama tawala kwa ahadi ya vyeo ambavyo ndani ya chama tawala vinapatikana kwa mamlaka waliyopewa na katiba. Ni rahisi sana kuhama upinzani kuliko kuhama CCM kwenda upinzani pasipo na vyeo kama Ukuu wa Wilaya,uRC, ubalozi,uwaziri, ukuu wa idara na mashirika mbalimbali tena kwa mishahara minono. Upinzani hakuna kitu zaidi ya kuwekwa mahabusu makesi kila kukicha.
Ukiona mtu ametoka CCM na kwenda upinzani ujue amejitolea kweli kweli lakini ukiona mtu ametoka Upinzani na kurudi CCM ujue amechoka kuishi maisha magumu.

Nawapongeza wanaChadema kwa kuamua kuachana na maandamano na kulinda amani ya nchi yetu. Nilikua nayapinga sana haya maandano mwanzo mwisho na sasa yameahirishwa nawaunga mkono viongozi wa CHADEMA kwani kupingana na dola sio jambo la busara. Siasa nzuri ni mazunguzo na sio nguvu ,matusi na vurugu.
Big up Mbowe kwa kuepusha shari.
Nawaomba wale wote wanaojua umuhimu wa amani wajitokeze kumuunga mkono Mbowe.
Pongezi pia kwa mh. Rais kwa kujitokeza na kueleza furaha yako ya kukutana na kushikana mkono na Mh. Lowasa , umeonyesha kuwa unajali umoja na upendo wa watanzania pamoja na ukweli kuwa wafia vyama kama mleta mada hupenda kupandikiza chuki kuliko kujenga amani.
Umeandika maneno meeengi, lakini hayana content yeyote.
 
Hivi wewe si ndio ulikuja na kipeperushi chako humu ukitaka watu wapigwe sijui pigo takatifu Mods wakaishia kuufutilia mbali ,
kumbe ulikuwa umejitega ukitegemea kesho watu watapigwa eeh ? Hongereni sana ,
Inawezekana Chadema kuna ombwe la uongozi ila kama ndio hivi kuja na mkakati kama wa ukuta nakuitingisha serikali nzima wacha hilo ombwe lidumu milele.


Halafu naomba kuuliza hivi una mume ??
Braza huyu hafai kuoa kabisa utajuutraa kumjua
 
Wadau, kuna sinema ya zamani (sikumbuki jina) imeigizwa na Van Damme, na Boro Yeung. Wanayoyafanya sasa akina Shonza na watu wanaofanana naye, inanikumbusha sana ile sinema. Mwishoni mwa sinema hiyo, kulikuwa na mpambano mkali kati ya Damme na Boro Yeung. Lakini mpambano huo, ulijaa hila na udanganyifu (Hila hizo zilifanywa na Boro Yeung) ili kupata ushindi.... kwa wale ambao walishaoina sinema hiyo ya zamani wanakumbuka sana. Ndivyo wana CCM wanavyoonekana sasa. Unawezaje kushangilia ushindi wa pambano la ngumi ambalo mmoja wa mabondia ametumia kwanza mabaunza wake kumfunga mikono yote mpinzani wake, na kisha akajisifu kwamba amempiga mpinzani huyo kwa knockout?? Come on, you can fight? please give us a fair fight.. ili tuone kweli kama unaweza kusimama mwenyewe raundi zote 12!
 
Leo nitaanza bila salamu,
Ndugu wanajamvi, kwa siku za nyuma kidogo, takribani mwaka mmoja uliopita niliwahi kuandika hapa kuwa CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na nikasema katika maneno ya hitimisho la andiko langu hilo kuwa;


Nakumbuka vizuri, niliambulia matusi mengi kama ninavyotaraji hata leo pia. Kama nilivyosema wakati huo nitasema tena leo kuwa WATANZANIA wameshapoteza IMANI na chadema na uongozi wake. Wasomi, wanataaluma, na makundi mengine yenye influence kwenye jamii hawaiungi tena mkono chadema, nimeshangazwa hata bodaboda na machinga nao wanajitenga mbali na chadema.

Waandishi makini wameacha kabisa kuwaunga mkono chadema, hata wale ambao waliwaandika vizuri kwenye social media akina Mwanakijiji, Chahali na hata Pasco wamekuwa wakiwashushua kila uchao juu ya maamuzi yao na uelekeo wao.

Kwa mara nyingine tena, LEO umefanyika uamuzi mwingine wa kuchekesha na wenye kuudhi. Uamuzi unaoendelea kuthibitisha kuwa Uongozi wa CHADEMA umekosa dira, maono na hawana tafakuri sahihi juu ya mabadiliko ya wakati na namna bora ya kuendesha siasa za sasa. Walipodhani kuwa FEDHA zinaweza kuwa THINK TANK ya chama na kusahau BRAINS matokeo yake ndio haya, mnakosa strategic plan na mnaishia kughairisha mikakati bila sababu za msingi zenye kueleweka kwa watu na kupoteza influnce zaidi, actually hata wanachama wanawadharau kwa mwendo huu.

Labda ilikuwa utani, lakini UONGOZI wa chadema wanapaswa kufahamu kuwa Naibu Katibu Mkuu wao na wanachama wao 27 wako korokoroni hivi sasa kwa sababu ya mpango wao wa hovyo. Watu hawa tumaini lao ilikuwa ni kuungwa mkono lakini uongozi wao umewasaliti, umewatanguliza kama CHAMBO then mpango umeahirishwa. Lakini kuna vijana chungu mzima, ambao walikuwa driven na UKUTA wakajikuta wanamtukana Mkuu wa Nchi na Serikali yake nao wananyea debe wakati uongozi wao unaghairisha kiutani utani, opresheni iliowafikisha jela.

Hivi visingizio kuwa familia ya Nyerere imekutana na Lowassa na kumuomba, naomba nisitolee maelezo ila nitampigia simu personally msemaji wa familia hiyo Ndugu Makongoro ili ikiwezekana kesho ama keshokutwa afanye press, au aende Clouds au Efm kuthibitisha kuwa walikutana na Lowassa na kumuomba a-abort mpango mzima.

UKUTA chali, kama nilivyotegemea.

Jioni Njema...!!
kuna kitu mbaya ulifanywa na mtu fulani Chadema wewe binti si bure. na inaonekana ni kitu kibaya mno....cha aibu!
 
ombwe la uongozi cha unawanyima usingizi watawala, sasa hapo maanake nini
 
Kwani mlipokuwa mnang'aka ukuta upo pale pale hamkulijua hilo la damu kumwagika? Mliombwa na viongozi wa dini mkagoma, mkidhani serikali itawaogopa wasaliti wa taifa. Hakuna mchezo huo. Tushirikiane kujenga nchi huu ukibaraka wa mataifa ya magharibi tuachane nao hauna tija kwa taifa.
Unatetea uvunjifu wa katiba ili iweje?
 
Hivi hizi siasa za nchi yetu sizitakagi, si ccm wala upinzani wote ni walewale , leo ukiwa chama A Utakiponda sana chama B , kesho ukihamia chama B utakisifia na kukiponda chama A, sasa ndo siasa gani hizi jamaniiiii, sisi sote ni ndugu na tunategemeana kwa nini tusisikilizane?? MUNGU AILINDE TANZANIA YETU .
Vyovyote vile, usimuunge mkono anaedai analeta maendeleo kwa kukanyaga katiba ya nchi
 
Leo nitaanza bila salamu,
Ndugu wanajamvi, kwa siku za nyuma kidogo, takribani mwaka mmoja uliopita niliwahi kuandika hapa kuwa CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na nikasema katika maneno ya hitimisho la andiko langu hilo kuwa;


Nakumbuka vizuri, niliambulia matusi mengi kama ninavyotaraji hata leo pia. Kama nilivyosema wakati huo nitasema tena leo kuwa WATANZANIA wameshapoteza IMANI na chadema na uongozi wake. Wasomi, wanataaluma, na makundi mengine yenye influence kwenye jamii hawaiungi tena mkono chadema, nimeshangazwa hata bodaboda na machinga nao wanajitenga mbali na chadema.

Waandishi makini wameacha kabisa kuwaunga mkono chadema, hata wale ambao waliwaandika vizuri kwenye social media akina Mwanakijiji, Chahali na hata Pasco wamekuwa wakiwashushua kila uchao juu ya maamuzi yao na uelekeo wao.

Kwa mara nyingine tena, LEO umefanyika uamuzi mwingine wa kuchekesha na wenye kuudhi. Uamuzi unaoendelea kuthibitisha kuwa Uongozi wa CHADEMA umekosa dira, maono na hawana tafakuri sahihi juu ya mabadiliko ya wakati na namna bora ya kuendesha siasa za sasa. Walipodhani kuwa FEDHA zinaweza kuwa THINK TANK ya chama na kusahau BRAINS matokeo yake ndio haya, mnakosa strategic plan na mnaishia kughairisha mikakati bila sababu za msingi zenye kueleweka kwa watu na kupoteza influnce zaidi, actually hata wanachama wanawadharau kwa mwendo huu.

Labda ilikuwa utani, lakini UONGOZI wa chadema wanapaswa kufahamu kuwa Naibu Katibu Mkuu wao na wanachama wao 27 wako korokoroni hivi sasa kwa sababu ya mpango wao wa hovyo. Watu hawa tumaini lao ilikuwa ni kuungwa mkono lakini uongozi wao umewasaliti, umewatanguliza kama CHAMBO then mpango umeahirishwa. Lakini kuna vijana chungu mzima, ambao walikuwa driven na UKUTA wakajikuta wanamtukana Mkuu wa Nchi na Serikali yake nao wananyea debe wakati uongozi wao unaghairisha kiutani utani, opresheni iliowafikisha jela.

Hivi visingizio kuwa familia ya Nyerere imekutana na Lowassa na kumuomba, naomba nisitolee maelezo ila nitampigia simu personally msemaji wa familia hiyo Ndugu Makongoro ili ikiwezekana kesho ama keshokutwa afanye press, au aende Clouds au Efm kuthibitisha kuwa walikutana na Lowassa na kumuomba a-abort mpango mzima.

UKUTA chali, kama nilivyotegemea.

Jioni Njema...!!
Naanza kupata wasiwasi na elimu yako!!!!mbali na elimu,nakuona pia una matatizo ya kiakili.Kwanini nasema unamatizo ya kiakili?soma hapa😛SYCHOPATHOLOGY.
Huo ni ugonjwa wa akili unaosababishwa na aidha mazingira ya makuzi au kurithi.mgonjwa hua na tabia ya kufuatilia mambo ya mwenzake kuliko yake,pia mgonjwa huwa na tabia ya kuropoka hovyo hata kama mazingira hayamruhusu kufanya hivyo,pia mgonjwa hua na roho ya kupenda vita na mambo ya kuhatarisha maisha ya mwenzake kuliko yake,pia mgonjwa hupenda kuwa kinyume na wengine wote ili aonekane yeye ndio mshindi ilihali sio,pia mgonjwa ana tabia ya kuchukia pasipo sababu za msingi.Kwa hizo dalili hapo juu,kubali kuwa wewe ni mgonjwa wa akili.
kwanini nasema ninawasiwasi na elimu yako?soma hapa:GREAT MINDS DISCUSS IDEAS,AVERAGE MINDS DISCUSS EVENTS,LOW MINDS DISCUSS PEOPLE.
Kulingana na kiwango cha elimu ulichonacho sasa hivi sio wakati wa kumjadili mtu/watu,ungetakiwa utupatie "new ideas" katika taifa ambalo linakutegemea lakini naona huna tofauti na mtu aliye komea darasa la 2B kama sisi huku mukabuye.unajadili watu na matukio???????its too sad....eti unaosha umpigie simu makongororo,kwani ukimpigia au usipompigia itamsaidia nini kabwela wa songwe?????buni mbinu za kuisaidia serikali ili tutoke hapa tulipo na tusonge mbele,sio kuja JF na kutoa chuki zako humu.. kaa chini utizame vyeti vyako kisha urudi usome ulichokiandika,kisha ujiulize je ni vyako kweli au ulipewa tu ili uje utuhadae watanzania ambao tulikomea std 2B?.
Hata ubunge wako pia naanza kupata wasiwasi nao au ndo "JIKOMBE,UKOMBOKE"???????????
 
Execuse zinazotolewa ndio zinaudhi zaidi, Siku kumi nyuma unasema tumekutana na Viongozi wa dini tumezungumza nao na mkasema kuwa UKUTA uko pale pale leo mnasema tumezungumza na Viongozi wa dini (kama vile ni kitu kipya) na kuongeza tumezungumza na familia ya Mwalimu Nyerere (haijawahi kutokeo) tumeamua Kughairisha UKUTA, sio kuvunja kabisa bali kughairisha eti wakitegemea kutakuwa na tension kama ya awali.

Hesabu mbofu sana hii
ulimsikiliza mh.mtukufu waziri wa mambo ya ndani kipindi anahojiwa na bbc?sababu zake zimekaa vp?,je ulimsikiliza kamanda wa jeshi la polisi alipokuwa akiwapongeza wapinzani,je hapo unasemaje?wewe na wadhifa uliopewa lakini naona kama bado hujielewi unatoka wapi wala unaenda wapi"kama ule wimbo wa prof.j"
 
Back
Top Bottom