Kabla sijachangia ningependa kujuwa umri wako kwanza halafu nenda kasome kuna thread humu ya mapenzi na umri ndio tutaelewana.
Maana yake tusije kujadili mambo ya pesa hapa kumbe hujawahi hata kumiliki 1 million yako mwenyewe wakati humu kuna watu millioni kwao ni buku tu.
Atoto labda nikukumbushe pindi unakuwa japo nahakika bado ni mdogo tu anyhow kulingana na wishes zako.
Kipindi cha utotoni kila mtu huwa akiulizwa ynataka kuwa nani baada ya kumaliza shule, wengi hujibu daktari, rubani, mwalim n.k lakin hata mimi binafsi niliyetamani kuwa daktari leo hii nimejikuta mjasiliamali hahahaha, so always nature inatake charge nothing you can do,
Ushauri wangu kwako ni kuachana na misimamo ambayo haina tija kwako na kwa atakae kuoa maana kila mtu angeweka mashart ya namna hiyo basi zaid ya 90% za ndoa zingevunjika including ya wazazi wako, otherwise best of lucky!!!
kutokufahamiana kwa sura hapa kuna tugharimu sana..
Mkuu hapo umesema jambo, utakuta mtu hoehae kila siku anachomwa na jua, na mvua yake...kifupi hajafikia viwango kabisaaaa, ni mtu ambae hutakuja maishani muwe na mahusiano yoyote ya karibu...
Unapokaa yeye hawezi kutia mguu, unapofanya manunuzi yeye hawezi kushop huko..halafu ndio wa kwanza kutoa masharti kwa watu.???
Halafu kutwa kucha kulalamikia yafuatayo...
1. wazuri hamuolewi
2. Amenichezea na kunipotezea muda
3. Ananipa kila kitu lakini hanipendi
4. Yaani nipo pale kwa sababu ya watoto tu
5. .....
halafu wewe na mleta hii sredi lenu moja eenh...:angry:
MSIMAMO WANGU
1. Changu ni changu, cha mume/mpenzi wangu tunashea.
2. Mwanaume bahili akae mbali na mimi.
3. Sina huruma na pesa ya mwanaume, labda atakaekuwa mume wangu wa ndoa.
4. Ntafanya majukumu yote kama mpenzi/mke wake, lakini when it comes to my money asahau, imeandikwa "mwanamke atazaa kwa uchungu na mwanaume atakula kwa jasho" so let him provide.
5. Ni marufuku mambo ya joints a/c eti mmoja wetu anaweza kutoa pesa pasipo saini ya mwingine sitaki.
6. Pesa zangu ni zangu ata password cmpi, bora nimpe Mama angu ata nikifa ajifutie nazo machozi.
7. Hata kama nina pesa kuliko yeye, mwanaume ni lazima awajibike, sio pesa ake awanufaishe wengine, maana kuna wanaume ndani wabahili ila nje wanahonga balaa.
8. Nyumba tutasaidiana kujenga, na itakuwa na jina langu na lake, au kama tutakuwa na watoto nao tutawaweka humo.
9. Ni marufuku ndugu wa mume kujihusisha na mali zetu, narudia tena ni marufuku ndugu wa mume kujisogeza karibu na mali zangu mm na mume wangu! Hizi haziwahusu kabisa tena mkae mbali.
NIMEMALIZA
Wadada wengi katika umri fulani huwa na mtizamo na "msimamo" kama wako. Sio kitu cha ajabu kwa binti wa 20-25yrs kufikiri kama wewe, i'd put you in that age group. Lakini ubinafsi huo unakuwa na mwisho au msimamo kupungua na vigezo kushushwa. Hamna mwanamke asiyependa kufanyiwa na mumewe vile unavyosema, lakini katika reality ni asilimia ndogo sana wanapata toka kwa waume zao (hapa siongelei vibuzi).
Jaribu kupunguza ubinafsi, maisha ni kushirikishana, kusaidiana pale mmoja anaposhindwa, kupeana n.k...!
hahaha ndo inamfaa huyu....Hahahaaa...hiyo kaliii
Vibinti vipenda hela vizuri sana. Unajimegea utakavyo then unatupa kule. Kenyewe kanajua kamekukimoa kumbe we umetumia chenji ya rada.
Hapa ndo napompendea Liyumba.