Muuza viatu
JF-Expert Member
- May 14, 2020
- 3,840
- 7,916
Bwashee punguza jazba,si Kila Jambo lipo km unavyoliona.Kwa miaka mingi sana tangu kuondolewa kwa Tido Mhando kwenye uongozi wa TBC , Channel hii imejipambanua bila kificho wala uoga wowote kama channel ya ccm , kwa kuonyesha kila kinachofanywa na ccm hata mambo ya hovyo na yasiyo na tija kwa Taifa hili , imewapuuza wapinzani katika kipindi chote hicho huku ikiwanyima hata nafasi ya kukohoa tu kwenye mic zao , Watangazaji wake wamekuwa makada halisi wa ccm wenye kusifia hata ukandamizaji , hoja zote zenye tija hazijawahi kupewa nafasi kwenye TV hii .
Kwa tabia hii TBC imepoteza kabisa watazamaji katika nchi hii baada ya wananchi kwa umoja wao kuidharau moja kwa moja , nini kimetokea leo kwa TBC kutangaza mkutano wa Chadema , Je TBC inatafuta umaarufu kupitia mgongo wa Chadema baada ya wananchi kuipuuza ?
Napinga jambo hili na sitakubali Chadema itumike kama ngazi , waendelee kuifagilia ccm sisi tutapita nyumba kwa nyumba .
Naomba kuwasilisha .