Msikilizeni Zitto Star TV

Msikilizeni Zitto Star TV

Nataka kurudi Chadema mara baada ya .....

Nitayaamini maneno yanayotolewa na wanachadema siku siku haya maswali yakipatiwa majawabu

Natamani sana kuwa Kamanda lakini haya yananitatanisha,naombeni majibu ili nifanye maamuzi magumu.

1.Walituambia kuwa chama cha wananchi CUF ni tawi la ccm,wakaenda mbali kwa kuwaita kuwa ni chama cha Mashoga ghafla wakasahau matusi yao na wakaanza mashirikiano Mapya,Je ile tuhuma iliishia wapi?

2.Chadema walituaminisha kuwa Chama cha NCCR mageuzi kimejaa Usalama wa Taifa,wakaenda mbali wakamkejeli Mbatia, tena ndani ya Bunge kuwa,yupo Upinzani huku akiitumikia ccm,ghafla tu Mbatia ni Mshirika namba Mbili wa Ukawa bila watanzania kuelezwa kama zile tuhuma zilikuwa za kweli au za kutunga kwa nia ya kuwalaghai watu.

3.Chadema kwenye Ilani yake 2010 walituambia kuwa tukiwachagua hawatachukua posho kama hatua mojawapo ya kuonyesha kwa vitendo kuchukizwa na matumizi mabaya ya serikali.Je Kwanini wamekiuka Ilani yao?

4.Chadema Mwaka 2011 walikataa kushirikiana na vyama vya Upinzani ili kuunda kambi ya Upinzani yenye sauti na nguvu,wakatuambia kuwa Vyama vyote ni mawakala wa ccm isipokuwa Chadema,hivyo kushirikiana nao ni kurudisha nyuma harakati za ukombozi,ghafla tu baraza kivuli la mawaziri likavunjwa na wale vibaraka wa ccm wakaingizwa kwenye kambi ya upinzani bila sisi wafuasi kuambiwa ni lini ukibaraka wao umeisha mpaka wakaaminiwa.

5.Tuliambiwa kuwa David Kafulila ni mtu hatari kwa ustawi wa Upinzani hasa Chadema,tukaambiwa ni Sisimizi ambae hana umuhimu wowote ndani ya Chadema ,ghafla tu Sisimizi kageuka tembo,Mtu hatari kageuka Shujaa na sasa ananadiwa na viongozi wa Chadema kuwa ukawa imepata tuzo,Je ni lini kafulila alianza kuaminiwa ?

6.Tuliambiwa tena kuwa ,Serikali kutumia mashangingi huku Zahanati hazina dawa ni kiwango cha juu cha Ubinafsi,Mbowe akalikataa Shangingi la Kiongozi wa Upinzani....ghafla nimemuona Bukoba akiwa na Shangingi lenye maandishi KUB. Je ndio lilelile alilolikataa hadharani au ni lingine?

7.Mbowe alituahidi kwenda mahakamani,na kudai kuwa wanasheria wake wanaandaa mashtaka dhidi ya Zitto Kabwe baada ya Zitto kumtuhumu kuwa alipokea fedha toka kwa makada wa ccm na kuwa alicheza dili ns Kinana kuhusu deni analodaiwa na NSSF.Je taratibu za ufunguaji kesi ziliishia wapi ?

8. Chadema Mwaka 2011 ilitangazia Umma kutomtambua Rais Kikwete kwakuwa alishindwa na Slaa,ghafla wanatangaza kuomba mashauriano na Rais waliemkataa,wakafika Ikulu kujadiliana juu ya maswala mbalimbali ya Kitaifa,wakanywa Juice na kupiga picha,Je ni lini Chadema ilianza kumtambua Rais na kwanini sisi wananchi hatukuelezwa kuwa kuanzia sasa Kikwete ni Rais?
Sina nia ya kuibua Marumbano yasiyotujenga bali nataka mtu mwenye uelewa mkubwa kuliko mimi anaondoe Uvulivuli ili nami nijitambue.


Naomba nijibiwe hayo ili nami niwe Kamanda nitakaeitetea Chadema popote.

Hayo Majawabu yakipatikana,ndio utakuwa mwisho wa Chama cha ACT-Wazalendo maana umma utaiamini Chadema na hivyo kuiunga mkono.

Kama Maswali yakikosa Majibu basi Chadema itakosa uhalali wa kutuhumu ACT-Wazalendo na viongozi wake na hivyo wananchi wataendelea kujiunga na ACT-Wazalendo kwa kuamini kuwa maneno yoyote yanayotolewa na Chadema ni Ulaghai.

Karibuni kwa majibu Makamanda ili nasi tupate chakuwaambia wananchi ili waipuuze ACT-Wazalendo.

Uko kamili upstairs? Kila thread ikianzishwa unatupia huu utumbo
 
Tatizo hamtapata akina shibuda, watakaokatwa ccm wataenda act na sio cdm kwani wameshaona wenzao kilichowapata huko. Kuna sura hata ukizipeleka appt au chausta zitashinda tu na ndo hizo zitaibeba act. Ila kama mnaamini hana madhara basi wacheni kumfuata kila anakopita muone cha mtemakuni.
CHADEMA kumejaa hakuna nafasi za kina Shibuda.Ukawa tumeshamaliza kai ya kugawana majimbo na CHADEMA wagombea wetu wote wanajulikana.Shibuda mwenyewe nafasi yake inazibwa na Kamanda mwingine. Nyinyi subirini watakaotemwa na mabwana zenu magamba.
 
ok mkuu. Vipi zitto amepata zile milion 700 toka kwa mamvi na ccm?

Mzalendo wa kweli mwenye uchungu na nchi hii atachangia tu, kwa sasa tunaanza kuweka kapu baada ya kupigwa neno la ukombozi wa kizalendo unatupia noti kwenye kapu, mihadhara sasa ni mwanzo mwisho hadi nchi irudi kwenye misingi yake.
 
Tatizo hamtapata akina shibuda, watakaokatwa ccm wataenda act na sio cdm kwani wameshaona wenzao kilichowapata huko. Kuna sura hata ukizipeleka appt au chausta zitashinda tu na ndo hizo zitaibeba act. Ila kama mnaamini hana madhara basi wacheni kumfuata kila anakopita muone cha mtemakuni.

Kwahiyo mkuu unataka Chadema tuache kufanya kazi zetu kwasababu ya ziara za Zitto? hahahaa
 
Team ccm please tuendelee kumpa support ya kutosha kijana wetu zzk
Tunajua CCM wamemwambia ayatullah siku akithubutu kuchukua mwanachama hata mmoja kutoka CCM ndiyo itakuwa mwisho WA kukifadhili hicho kikundi cha act wasaliti.
 
Zzk ni janga la upinzani hapa tanzania
Ulitaka baada ya kufukuzwa cdm akalime na aache siasa? poleni sana wachagga, yamewafika!na ziara mikoa 14 iliyobaki inaanza next week, watu watafurika na kuchukua kadi kama kawaida!!
 
Bila shaka ni hazina ya Mama yako

Mi sitaki kuamini kama kweli wewe ni Chadema! Unamtukana mama yake? We sio wa Chadema. Siamini kabisa! Inaonekana huna elimu hata ya chekechea! Elimu ndogo ni tatizo! Lasivyo yawezekana ulimchungulia mzazi wako jinsia ya KE sehemu nyeti ukapata laana! Sio bure! manaake huwaheshim akina mama!

Hiyo laana uloachiwa itaendelea kukutafuna milele daima! Ungama dhambi zako hujachelewa. Mheshim mama ako na akina mama wote ili upate baraka.

Siasa sio ugomvi na matusi dhidi ya wazazi wetu tena wasiohusika. Washabiki wa MAGAMBA waache washabikie au waelimishe, wafuasi wa ACT nao vivyohivyo.

Nikweli CCM imetuchosha, ila harakati za kuitoa CCM madarakani haziwezi kufanikiwa kwa matusi na vitu vingine vinavyofanana na hivyo. Jenga hoja Watanzania wakuelewe.
 
Zitto na ACT wanatoa hoja za kujenga Taifa! CDM na misukule yao wanaporomosha matusi tu.

Nimemsikiliza vizuri, hakuna la maana aliloongea ambalo naweza lilipoti hapa!! Acha kuwa msukule wa Zitto, jitambue utoke kuwa mfuasi wa mtu uwe mfuasi wa itikadi!! CDM ina majibu yote kuhusu kuporomoka kwa thamani ya shilingi pamoja na matatizo yanayotukabiri wanyonge!! Sio hizo porojo za umimi za Msaliti Zitto!!
 
hapa ndo unagundua zito anawalaza milango wazi chadema, ikiwekwa habari ya zito maskio yanawasimama kama sungura
 
hapa ndo unagundua zito anawalaza milango wazi chadema, ikiwekwa habari ya zito maskio yanawasimama kama sungura
kwa hiyo jukwaa ni la zitto ikiletwa habari yake isijadilie poor JF inashushwa hadhi na wanazi wa zitto kwa kasi ya ajabu
 
Mi sitaki kuamini kama kweli wewe ni Chadema! Unamtukana mama yake? We sio wa Chadema. Siamini kabisa! Inaonekana huna elimu hata ya chekechea! Elimu ndogo ni tatizo! Lasivyo yawezekana ulimchungulia mzazi wako jinsia ya KE sehemu nyeti ukapata laana! Sio bure! manaake huwaheshim akina mama!

Hiyo laana uloachiwa itaendelea kukutafuna milele daima! Ungama dhambi zako hujachelewa. Mheshim mama ako na akina mama wote ili upate baraka.

Siasa sio ugomvi na matusi dhidi ya wazazi wetu tena wasiohusika. Washabiki wa MAGAMBA waache washabikie au waelimishe, wafuasi wa ACT nao vivyohivyo.

Nikweli CCM imetuchosha, ila harakati za kuitoa CCM madarakani haziwezi kufanikiwa kwa matusi na vitu vingine vinavyofanana na hivyo. Jenga hoja Watanzania wakuelewe.

Umeongea kitu cha maana sana, chadema wanachofanya ni philosophy ya kimarekani inayoitwa "affirmative action" na philosophy ya kijerumani inayoitwa "Black Propaganda" pia wanatumia philosophy ya kirusi iliyotumiwa na Stalin iliyoitwa "Lumpen proletarian" kwa wakati ule theory hizi zilifanikiwa ila kwa siasa za Tanzania tayari zimeshachelewa, ukitumia mbinu hizi kwa muda mrefu watu wanaanza kugutuka polepole.
 
Mi nilidhani ni ACT kama chama kumbe ni Zitto kama a.y.atula.h?? Siku mkimjua rangi yake ndo akili itawakaa sawa!!
 
Back
Top Bottom