Msikilizeni Waziri mwenye Dhamana

Msikilizeni Waziri mwenye Dhamana

Ahaa, kumbe hii Serikali huwa inasikiliza maoni ya wananchi?
Saana tu kwenye eneo langu 👇👇👇 ikiwemo namba yangu binafsi miaka yote sms moja kwa moja, imo humo, wape na wengine kwenye mtaa wako unakoishi🤗
 

Attachments

  • IMG-20250708-WA0028.jpg
    IMG-20250708-WA0028.jpg
    151.2 KB · Views: 7
  • IMG-20250708-WA0027.jpg
    IMG-20250708-WA0027.jpg
    186.1 KB · Views: 8
  • IMG-20250503-WA0007(4).jpg
    IMG-20250503-WA0007(4).jpg
    103.2 KB · Views: 8
Nenda sasa jukwaa la wataalamu. Ni kazi ya mtoa hoja au mshiriki wa mjadala kujua, anashiriki mjadala gani na nani ba hapo ndiyo umuhimu wa kuulizana CV sasa duniani kote. Maana mnaweza kupishana content kwa kuwa, hamjuani nani mwenzangu.
Kwa kutumia kigezo chako kipya cha CV kwanza kabla ya hoja, unadhani una CV za kutosha kunihoji mimi ni nani?

Kama mjadala unategemea ubora wa CV ya mtoa hoja, kwa nini uko kwenye jukwaa ambalo 99% ya washiriki wana fake ID? Unajuaje kama unajadili na watu wenye CV unayodhani unastahili kuwajibu?

Au hili nalo kujibiwa mpawa niweke CV zangu mbele Mheshimiwa?

Kama unapima kila hoja kwa CV ya mtoa hoja, basi JF si jukwaa lako maana asilimia
99 ya wachangiaji hawajulikani majina yao halisi wala taaluma yao.

Nice to meet you.
Nikiweka sahihi huwa sirudi.
Ibn Unuq
 
Kwa kutumia kigezo chako kipya cha CV kwanza kabla ya hoja, unadhani una CV za kutosha kunihoji mimi ni nani?

Kama mjadala unategemea ubora wa CV ya mtoa hoja, kwa nini uko kwenye jukwaa ambalo 99% ya washiriki wana fake ID? Unajuaje kama unajadili na watu wenye CV unayodhani unastahili kuwajibu?

Au hili nalo kujibiwa mpawa niweke CV zangu mbele Mheshimiwa?

Kama unapima kila hoja kwa CV ya mtoa hoja, basi JF si jukwaa lako maana asilimia
99 ya wachangiaji hawajulikani majina yao halisi wala taaluma yao.
Hata mimi nashangaa kwa nini hawajulikani wanajificha ? 😃
Na mimi kazi yangu si kuanza ku audit CV za watu bali, kutaka kufahamiana pale tu ambapo, hoja imeanza kujielekeza kwenye kugusa tafsiri rasmi za kitaalam na mimi kutakiwa sasa, nikubaliane na shinikizo la mtoa hoja kuhusu tafsiri anayotoa yeye. Hapo sasa ndiyo hitaji la kujuana linaanza na mimi kuonekana korofi korofi hivi.
 
Binafsi nachokiona matatizo hayatokei from from nowhere bali makosa uzembe wa leo ndio unasababisha shida za kesho, and on that token kuna bomu fulani ambalo litawatafuta awamu za kesho ila ukweli ni mbegu mlizopanda nyie kwa kutokushughulikia hii michicha kabla haijawa mibuyu..., nilishauliza na sitachoka kuuliza (as my civic duty) na suala hili linahitaji ushirikiano wa nyie wote sio kwamba hii ni Wizara yangu basi nifanye yangu pekee... (Nadhani hayo ya Mungu / Imani, Tuyaache kwenye Imani au tuyahifadhi tukiwa kwenye nyumba za Ibada hapa tudeal na ya Kaisari )

Soma sera mpya ya wazee toleo la 2023 ambalo, tumefanikiwa kulitoa baada ya ile ya 2013 kupitwa na wakati. Nadhani humo utaona mengi kuhusu swali lako zuri na mwelekeo.
 
Soma sera mpya ya wazee toleo la 2023 ambalo, tumefanikiwa kulitoa baada ya ile ya 2013 kupitwa na wakati. Nadhani humo utaona mengi kuhusu swali lako zuri na mwelekeo.
Kwa wewe kuniambia tu nikasome inaonyesha ni vipi hayo matarajio (theories on paper) haziendi sambamba na na kinachoendelea ground...; Kumbuka mzee wa keshokutwa ni kijana wa leo kwahio ili kumsaidia mzee wa keshokutwa ni kuhakikisha kijana wa leo anapata ujira wa kutosha na kuweza kujiwekea ili aweze kulia (kula sio crying) kivulini...

Hivyo Case in point mfano sasa hivi vijana wengi ambapo dunia ni kijiji wanajitafutia mkate online kwa kurusha kazi zao (podcasts n.k.) ila ndio hivyo bundle halishikiki na kuna kipindi TCRA wanaleta sheria za online Radio gharama ya kupiga soga online inakuwa kama vile mtu anaanzisha mega billion project...


Naam na mzee huyu ili kesho aweze kupata hata pesa ya panadol inabidi hata leo aweze kujiwekea akiba (ukingatia wengi kitaa ni wabangaizaji na mtaji wao ni nguvu zao)


Ni hayo tu nadhani ifike wakati tu walk the walk kwa kuanzia tulipo na kufanya tunachoweza
 
Kwa wewe kuniambia tu nikasome inaonyesha ni vipi hayo matarajio (theories on paper) haziendi sambamba na na kinachoendelea ground...; Kumbuka mzee wa keshokutwa ni kijana wa leo kwahio ili kumsaidia mzee wa keshokutwa ni kuhakikisha kijana wa leo anapata ujira wa kutosha na kuweza kujiwekea ili aweze kulia (kula sio crying) kivulini...

Hivyo Case in point mfano sasa hivi vijana wengi ambapo dunia ni kijiji wanajitafutia mkate online kwa kurusha kazi zao (podcasts n.k.) ila ndio hivyo bundle halishikiki na kuna kipindi TCRA wanaleta sheria za online Radio gharama ya kupiga soga online inakuwa kama vile mtu anaanzisha mega billion project...


Naam na mzee huyu ili kesho aweze kupata hata pesa ya panadol inabidi hata leo aweze kujiwekea akiba (ukingatia wengi kitaa ni wabangaizaji na mtaji wao ni nguvu zao)


Ni hayo tu nadhani ifike wakati tu walk the walk kwa kuanzia tulipo na kufanya tunachoweza
Una haraka sana. Ungesoma ungeongeza maarifa zaidi, ungeona na uwepo wa mabaraza ya wazee na yanatakiwa kufika wapi. Halafu, muwe na jicho basi la kukumbuka kuwa, hata hiyo sera ilishapitwa na wakati. Kumbe unaongozaje wizara bila sera? Mabaraza ya wazee hayakuwepo na wazee walitaka awamu ya kwanza sera na mabaraza yao. Imekuwa. Sasa unataka miaka 3 na nusu ya uhai wa wizara yooooote yaishe 💯 , uliona wapi? Hivi mengine ni uelewa au sijui wivu au sijui nini? Maana inafika mahali spana zingine unacheka tu🤣

Haya basi mwendo tulianza Januari 2022, mwendo unaendelea, tumefika mahali siyo sawa na ilivyokuwa 2022, si wengine wataendelea? Watakuta na sera na mikakati ya kisera na miongozo ipo na mabaraza yapo.....

Sera na mikakati na mabaraza yangekuwa hayapo napo mngesema tu, wanaongoza kutoka mawazo ya mifukoni, hata sera na miongozo na ushirikishaji wazee hakuna....🤣,

Siku hizi nazijua veeema spana za jamii yangu 🇹🇿 tena kwa 360🤣
 
Wewe uko serikalini umepewa hilo, lichukue na ukijaliwa kurudi tena awamu ijayo basi lifanyie kazi. Hili suala ni mtambuka, hata wizara yako inahusika kwa kuwa jamii na watoto ndio wahanga.

Vv
Wizara kuwa mtambuka haina maana kuwa milango ya wizara husika mahsusi imefungwa. Huenda wewe huko ukauliza maswali na ukapewa na elimu ya ziada kama ninavyofanya mimi. Hapa mimi nitaondoka na nyie mtakuwa hamjajenga ukaribu na wizara zenu zingine, je anayekuja akiwa hana akaunti hapa au siyo mtu wa online , hizi spana zenu za hoja mtakuwa mnampa nani? Jiunganisheni na wizara zote mahsusi kwa faida ya maoni yenu jamii siyo faida yangu binafsi.

Kurudi au kutorudi ni majaliwa ya Mungu, nchi inao watu wengi wa kukaa sehemu mbalimbali na mimi kwenda sehemu tofauti kabisa, kikubwa uzima.
 
Una haraka sana. Ungesoma ungeongeza maarifa zaidi, ungeona na uwepo wa mabaraza ya wazee na yanatakiwa kufika wapi.
Nadhani hujaona tatizo mimi nikisoma wangapi wamesoma na nchi hii ni watu wangapi wana hulka za kusoma hususan hiki kipindi cha instant news na Tik Tok ? Kwahio hapo utagundua kwamba habari hazifiki kwa haraka huku chini na pia kuona maandishi sio reality.., na mimi nimeona reality ground na kuhusu hili bomu ndio maana nimeuliza tunajitayarisha vipi.., wewe unaniambia nikasome; kumbuka hawa sio wazee wa leo bali ni wa kesho na hatuwezi tukasema tutawapa pesa (hizo ni kodi zetu na wala hatuna za kutosha) kwahio shortcut ni kuhakikisha wanapata ujira wa kutosha leo; Na ndio maana nikasema hili sio lako peke yako bali na wenzako huko watunga Sera;
Halafu, muwe na jicho basi la kukumbuka kuwa, hata hiyo sera ilishapitwa na wakati. Kumbe unaongozaje wizara bila sera? Mabaraza ya wazee hayakuwepo na wazee walitaka awamu ya kwanza sera na mabaraza yao. Imekuwa. Sasa unataka miaka 3 na nusu ya uhai wa wizara yooooote yaishe 💯 , uliona wapi? Hivi mengine ni uelewa au sijui wivu au sijui nini? Maana inafika mahali spana zingine unacheka tu🤣
Sera gani ? Mabaraza yapi ? Tatizo hatupo kwenye same page kwangu mimi hata hayo mabaraza ni kutumia tu Kodi katika brah brah brah na story nyingi bila kufanya vitu practical; Mzee wa kesho ni kijana wa leo na mimi sijaongelea mzee wa leo bali kijana wa leo ambae ni mzee wa kesho (angalau wazee wa leo wachache wana pensheni, wengi vijana wa leo hata mkate wa leo tu hawana let alone savings za kesho) kwahio sio kwamba nimeleta tu story au sijui kupiga spana au eti wivu, mimi kama Mtanzania na raia nimeona ni vema tukashauriana kuhusu hili bomu la kesho ambalo litatupa athari angalau kuweza kufanya maisha ya kijana wa leo yawe rahisi kwa kujipatia ujira ili kesho aweze kujiangalia na sio kusubiri kupewa charity...; Je hayo yanahitaji Baraza au tungoje huyu azeeke ili ajiunge kwenye Baraza ?
Haya basi mwendo tulianza Januari 2022, mwendo unaendelea, tumefika mahali siyo sawa na ilivyokuwa 2022, si wengine wataendelea? Watakuta na sera na mikakati ya kisera na miongozo ipo na mabaraza yapo.....

Sera na mikakati na mabaraza yangekuwa hayapo napo mngesema tu, wanaongoza kutoka mawazo ya mifukoni, hata sera na miongozo na ushirikishaji wazee hakuna....🤣,

Siku hizi nazijua veeema spana za jamii yangu 🇹🇿 tena kwa 360🤣
Narudia tena tatizo Siasa zimekuwa nyingi hususan Politics za sasa hivi ni attack and survival mtu akisema kitu unaona kana kwamba ameku-attack na majibu mengi yanakuwa survival instinct (tumefanya hiki na kile); badala ya kuona kwamba sasa hivi Dunia kwa ujumla imekumbwa na mabadiliko ya mode of production; sasa hivi nguvu kazi haiitajiki kama zamani, teknolojia na automation itafanya watu kila siku wazidi kukosa ujira, sasa tunafanyaje kuondokana na hilo..., mfano mmojawapo ni mambo ya bundle na gharama ya bundle ambayo TCRA imesababisha imepanda; Je nikikuuliza hilo utasema sio Wizara yako wakati na wewe linakuhusu kwamba kizazi cha kesho kitakuwa hakina required skills ? au utasema ni kweli na mimi kama Mtanzania na Raia ngoja wakati tukiwa tunakunywa chai na watunga Sera wenzangu tuangalie ni kipi tunafanya ?

Narudia tena sipo kufanya politicking bali just putting my two cents on how I perceive things (na kuna mengi tunayoweza kufanya kidogo tu kwa leo ambayo impact yake itakuwa immediate, sustainable and long lasting)
 
Wizara kuwa mtambuka haina maana kuwa milango ya wizara husika mahsusi imefungwa. Huenda wewe huko ukauliza maswali na ukapewa na elimu ya ziada kama ninavyofanya mimi. Hapa mimi nitaondoka na nyie mtakuwa hamjajenga ukaribu na wizara zenu zingine, je anayekuja akiwa hana akaunti hapa au siyo mtu wa online , hizi spana zenu za hoja mtakuwa mnampa nani? Jiunganisheni na wizara zote mahsusi kwa faida ya maoni yenu jamii siyo faida yangu binafsi.

Kurudi au kutorudi ni majaliwa ya Mungu, nchi inao watu wengi wa kukaa sehemu mbalimbali na mimi kwenda sehemu tofauti kabisa, kikubwa uzima.
Mheshimwa, wala hili usinijibu, wewe umekuwa mtumishi wa umma kwa taaluma yako kabla ya kuwa Waziri. Kule kwenye ofisi za umma kuna 'visanduku vya maoni', siku hizi watu hawaandiki wala kutumbukiza maoni yao. Ukoandika barua na ikajibiwa basi kuna muujiza uko kwenye hiyo ofisi.

Vv
 
Nadhani hujaona tatizo mimi nikisoma wangapi wamesoma na nchi hii ni watu wangapi wana hulka za kusoma hususan hiki kipindi cha instant news na Tik Tok ? Kwahio hapo utagundua kwamba habari hazifiki kwa haraka huku chini na pia kuona maandishi sio reality.., na mimi nimeona reality ground na kuhusu hili bomu ndio maana nimeuliza tunajitayarisha vipi.., wewe unaniambia nikasome; kumbuka hawa sio wazee wa leo bali ni wa kesho na hatuwezi tukasema tutawapa pesa (hizo ni kodi zetu na wala hatuna za kutosha) kwahio shortcut ni kuhakikisha wanapata ujira wa kutosha leo; Na ndio maana nikasema hili sio lako peke yako bali na wenzako huko watunga Sera;

Sera gani ? Mabaraza yapi ? Tatizo hatupo kwenye same page kwangu mimi hata hayo mabaraza ni kutumia tu Kodi katika brah brah brah na story nyingi bila kufanya vitu practical; Mzee wa kesho ni kijana wa leo na mimi sijaongelea mzee wa leo bali kijana wa leo ambae ni mzee wa kesho (angalau wazee wa leo wachache wana pensheni, wengi vijana wa leo hata mkate wa leo tu hawana let alone savings za kesho) kwahio sio kwamba nimeleta tu story au sijui kupiga spana au eti wivu, mimi kama Mtanzania na raia nimeona ni vema tukashauriana kuhusu hili bomu la kesho ambalo litatupa athari angalau kuweza kufanya maisha ya kijana wa leo yawe rahisi kwa kujipatia ujira ili kesho aweze kujiangalia na sio kusubiri kupewa charity...; Je hayo yanahitaji Baraza au tungoje huyu azeeke ili ajiunge kwenye Baraza ?

Narudia tena tatizo Siasa zimekuwa nyingi hususan Politics za sasa hivi ni attack and survival mtu akisema kitu unaona kana kwamba ameku-attack na majibu mengi yanakuwa survival instinct (tumefanya hiki na kile); badala ya kuona kwamba sasa hivi Dunia kwa ujumla imekumbwa na mabadiliko ya mode of production; sasa hivi nguvu kazi haiitajiki kama zamani, teknolojia na automation itafanya watu kila siku wazidi kukosa ujira, sasa tunafanyaje kuondokana na hilo..., mfano mmojawapo ni mambo ya bundle na gharama ya bundle ambayo TCRA imesababisha imepanda; Je nikikuuliza hilo utasema sio Wizara yako wakati na wewe linakuhusu kwamba kizazi cha kesho kitakuwa hakina required skills ? au utasema ni kweli na mimi kama Mtanzania na Raia ngoja wakati tukiwa tunakunywa chai na watunga Sera wenzangu tuangalie ni kipi tunafanya ?

Narudia tena sipo kufanya politicking bali just putting my two cents on how I perceive things (na kuna mengi tunayoweza kufanya kidogo tu kwa leo ambayo impact yake itakuwa immediate, sustainable and long lasting)
Kusoma ni muhimu kwa mtu yeyote ambaye hupenda kuchangia mijadala. Hata asiposoma leo, kesho atasoma. Ninaonavyo mimi, hiyo sera, imeongelea yote haya kisekta. Suala la maendeleo ya wazee ni la sekta zote. Afya, ufugaji, ajira, kilimo, sheria, uchumi nk. Na haya yote yamo humo. Kwa ufupi niishie hapa. Nina mijadala mingi mkumbuke, bado sms inbox wanasema mama njoo huku, bado instagram na fb pia, hivyo, twende kwa ufupi ufupi tafadhali, ahsante sana ubarikiwe 🤗
 
Mheshimwa, wala hili usinijibu, wewe umekuwa mtumishi wa umma kwa taaluma yako kabla ya kuwa Waziri. Kule kwenye ofisi za umma kuna 'visanduku vya maoni', siku hizi watu hawaandiki wala kutumbukiza maoni yao. Ukoandika barua na ikajibiwa basi kuna muujiza uko kwenye hiyo ofisi.

Vv
Labda wako kidigitali? Kama taasisi husika hazijibu, waambieni wakuu wa taasisi husika, wakuu wa wilaya na mikoa husika na mawaziri wa sekta husika. Nijuavyo mimi kwa sekta hii niliko ni tumejisogeza karibu na jamii kidigitali hata kwa sms za kitochi tunafikika. 👇Na tunaachilia hadi za kila halmashauri sasa.
 

Attachments

  • IMG-20250503-WA0007(4).jpg
    IMG-20250503-WA0007(4).jpg
    103.2 KB · Views: 8
  • IMG-20250708-WA0028.jpg
    IMG-20250708-WA0028.jpg
    151.2 KB · Views: 8
  • IMG-20250708-WA0027.jpg
    IMG-20250708-WA0027.jpg
    186.1 KB · Views: 6
Kusoma ni muhimu kwa mtu yeyote ambaye hupenda kuchangia mijadala. Hata asiposoma leo, kesho atasoma. Ninaonavyo mimi, hiyo sera, imeongelea yote haya kisekta. Suala la maendeleo ya wazee ni la sekta zote. Afya, ufugaji, ajira, kilimo, sheria, uchumi nk. Na haya yote yamo humo. Kwa ufupi niishie hapa. Nina mijadala mingi mkumbuke, bado sms inbox wanasema mama njoo huku, bado instagram na fb pia, hivyo, twende kwa ufupi ufupi tafadhali, ahsante sana ubarikiwe 🤗
Ukishajua watu hawapendi kusoma wala hawasoni na unataka kuwalenga basi ni vema uwafikie kule walipo (kuna njia nyingi za mawasiliano) kama unaona sms ni nyingi na unaitwa pengi haushindwi kupunguza kidogo package zenu za ujira ili kuweka watu wa kuweza kufikisha ujumbe wenu na kuwajibu watu (after all ukosefu wa ajira ni janga kubwa sana). Na sasa hivi kuliko kulishana maneno mnaweza kupunguza mbinyo mnaofanya kwa wenyenchi angalau wakabakiwa na chenji...

 
Ukishajua watu hawapendi kusoma wala hawasoni na unataka kuwalenga basi ni vema uwafikie kule walipo (kuna njia nyingi za mawasiliano) kama unaona sms ni nyingi na unaitwa pengi haushindwi kupunguza kidogo package zenu za ujira ili kuweka watu wa kuweza kufikisha ujumbe wenu na kuwajibu watu (after all ukosefu wa ajira ni janga kubwa sana). Na sasa hivi kuliko kulishana maneno mnaweza kupunguza mbinyo mnaofanya kwa wenyenchi angalau wakabakiwa na chenji...

Mbona yote tumefanya? Kipendacho roho tu. Ngoja na wewe nikupe mawasiliano ili unisaidie kuwa sehemu ya kupitia huko wanakovuka wengi kuja kwangu, nawarejesha huko wanasikilizwa ila wanasema, basi tu mama we ❤️ youuuu🤣👇 endelea tafadhali
 

Attachments

  • IMG-20250708-WA0028.jpg
    IMG-20250708-WA0028.jpg
    151.2 KB · Views: 10
  • IMG-20250708-WA0027.jpg
    IMG-20250708-WA0027.jpg
    186.1 KB · Views: 10
  • IMG-20250503-WA0007(4).jpg
    IMG-20250503-WA0007(4).jpg
    103.2 KB · Views: 8
Mbona yote tumefanya? Kipendacho roho tu. Ngoja na wewe nikupe mawasiliano ili unisaidie kuwa sehemu ya kupitia huko wanakovuka wengi kuja kwangu, nawarejesha huko wanasikilizwa ila wanasema, basi tu mama we ❤️ youuuu🤣👇 endelea tafadhali
Kwa kuacha kulima kwangu karanga hapa na mchicha na kukwambia wewe yanayoendelea huku nimekusaidia even beyond my obligation na kufanya my civic duty..., ukizingatia wala silipwi na mwenzangu anagalau hii ni part of your job (kwahio benki inasoma na hapa upo kazini)..., kwahio tusichukulie kama ni attack au lawama bali pongeza watu kama mimi ambao wanatoka beyond their way.... kuonyesha nini au kulalamika kwamba kwanini hiki hakipo sawa (ni kwamba wanajenga) by the way mimi taendelea kukusaidia kwa hili na wewe nisaidie kwa hao kina TCRA (najua mnagongana kwenye makorido) kwa kusababisha bei ya Bundle isishikike...

 
Kwa kuacha kulima kwangu karanga hapa na mchicha na kukwambia wewe yanayoendelea huku nimekusaidia even beyond my obligation na kufanya my civic duty..., ukizingatia wala silipwi na mwenzangu anagalau hii ni part of your job (kwahio benki inasoma na hapa upo kazini)..., kwahio tusichukulie kama ni attack au lawama bali pongeza watu kama mimi ambao wanatoka beyond their way.... kuonyesha nini au kulalamika kwamba kwanini hiki hakipo sawa (ni kwamba wanajenga) by the way mimi taendelea kukusaidia kwa hili na wewe nisaidie kwa hao kina TCRA (najua mnagongana kwenye makorido) kwa kusababisha bei ya Bundle isishikike...

Hata mimi kushiriki mijadala saa 24 nipo tu ni nje ya muda wa kazi, ni upendo tu kwa kuwa, saa za kazi za umma si zinaisha saa 9.30 jioni siku za kazi na weekendni mapumziko?. Hivyo, Wote tuko vizuri tunatoa CSR ya muda wetu binafsi. Ila sasa, nikirejea hoja yako mwenyewe kuwa, na wengine nao wafanye huko kama nazidiwa na sms, na mimi kwa upendo kabisa nikakusogezea mawasiliano ya call center. Mimi nadhani hatujapishana popote tunaenda vizuri sana.
 
Labda wako kidigitali? Kama taasisi husika hazijibu, waambieni wakuu wa taasisi husika, wakuu wa wilaya na mikoa husika na mawaziri wa sekta husika. Nijuavyo mimi kwa sekta hii niliko ni tumejisogeza karibu na jamii kidigitali hata kwa sms za kitochi tunafikika. 👇Na tunaachilia hadi za kila halmashauri sasa.
Mheshimiwa, "labda" inatoka wapi tena? Kama wako kidigitali sasa hivyo visanduku ni vya nini? Sifurahii kubishana juu ya hili, yaani leo imekuwa ni jukumu letu wananchi kuwafundisha au kuwakumbusha wenye mamlaka jinsi ya kuendesha mambo? Wamewekwa hapo kufanya nini, kama wameshindwa si waachie ngazi wawapishe wengine?

Vv
 
Hata mimi kushiriki mijadala saa 24 nipo tu ni nje ya muda wa kazi, ni upendo tu. Wote tuko vizuri tunatoa CSR ya muda wetu binafsi. Ila sasa, nikirejea hoja yako mwenyewe kuwa, na wengine nao wafanye huko kama nazidiwa na sms, na mimi kwa upendo kabisa nikakusogezea mawasiliano ya call center. Mimi nadhani hatujapishana popote tunaenda vizuri sana. Tuendelee tu na ushirikiano.

Mheshimiwa, labda inatoka wapi tena? Kama wako kidigitali sasa hivyo visanduku ni vya nini?

Vv
Labda imejengwa na msingi wa hoja yako kuwa, visanduku vipo na havifanyi kazi. Ndiyo nikasema, labda walishahamia kidigitali wamesahau kuwatangazia au walitangaza hamkusikia? Kama sisi tulivyotangaza call center ila wapo watu wanafunga safari ya gharama kuja wizarani wakati shida yao ingesikilizwa tu hata kwa teleconference? Mambo mengi eti tuendelee kukumbushana.
 
Hata mimi kushiriki mijadala saa 24 nipo tu ni nje ya muda wa kazi, ni upendo tu kwa kuwa, saa za kazi za umma si zinaisha saa 9.30 jioni siku za kazi na weekendni mapumziko?. Hivyo, Wote tuko vizuri tunatoa CSR ya muda wetu binafsi. Ila sasa, nikirejea hoja yako mwenyewe kuwa, na wengine nao wafanye huko kama nazidiwa na sms, na mimi kwa upendo kabisa nikakusogezea mawasiliano ya call center. Mimi nadhani hatujapishana popote tunaenda vizuri sana.
Tofauti ya mimi ni kwamba overtime yangu kama mlima nyanya ingebidi niwe kwenye magroup ya wakulima wenzangu ila nikaona huyu mama anayejitolea hata zaidi ya saa za kazi kujibu hoja nimsukumizie hizi angalau wakati anakunywa chai aweze kuwasukumizia hao wenzake na wao wafanye mambo..., sasa ukinipa tena Mawasiliano ya Call Centre ambayo ningeweza kuyapata google huoni hata kwenye group la wakulima wenzangu itabidi nijiuzulu ili nifanye kazi ambayo haina kipato na inahitaji pesa (si nitala njaa) ? Hapa tu nimeweka tenga chini na kutumia pesa yangu ya chakula cha mchana kununua bundle (ambalo halishikiki)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom