mashambani kwao
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 370
- 56
Yeye yupo morogoro,mimi nipo bagamoyo nilimtembelea mwezi wa saba mwanzoni,nilikaa kwake siku kumi na mbili,baadaye nikarudi bagamoyo,ilipofika tarehe 20 mwezi wa nane alipiga simu na kunijulisha kuwa anamimba,huyu dada ni mfanyakazi wa serikali,nikamwambia nimefurahi sana nitalea mtoto wangu,baada ya kama wiki akapiga simu na kuniuliza je niwataarifu ndugu zangu?nikamwambia wajulishe tu kwa kuwa mimi nimeshajitambulisha kwao basi akapiga simu na kuwajulisha kinachoendelea,tarehe 31 mwezi wa nane alipiga simu angalieni akina dada sasa: dada.!mimi nimeona damu inatoka nimekwenda dukani nimepewa dawa za kuzuia kutoka damu,kaka:mimi nikamjibu kwa kuwa leo umechukua dawa nakuomba kesho asubuhi nenda hospitali iliukachekiwe vizuri,siku iliyofuata nikampigia simu nikauliza vipi unaendeleaje?dada akajibu kumbe zile dawa zimeongeza tatizo damu zinaendelea kutoka,nikamsisitiza lazima ufike hospitali baada ya siku mbili ndipo akafika hospital daktari akamwambia nakupa dawa za kukwangua tumbo mpaka naandika habari hii mimba haipo tena,wapendwa ninasiku mbili sijapata usingizi ninamaswali mengi ambayo sina majibu,naombeni ushauri na sio mizaha'jokes.