Kwa hilo utanisamehe!GAZETI ingawa inaweza kukuumbua, lakini nadhani utamtendea haki Marehemu Mwalimu wako wa ABC na 1,2,3, iwapo utataja jina lake na shule yake. Naamini humu jamvini ni wengi watakuwa wamefundishwa na ticha huyo. Pole Sana GAZET kwa masaibu hayo ingawa ndio njia yetu sote.
Ni mwalimu wangu ambaye amenifundisha darasa la kwanza, ni kipindi kile
ambacho tulikuwa hatupitii shule za awali tulikuwa tunaanza shule ya
msingi moja kwa moja.
Nilimpenda sana huyu mama na kila nilipokuwa narudi likizo ilikuwa lazima niende
nikamsalimie na kumwachia chochote kwani namuona kama mama yangu pia
nakumbuka mbali sana kila ninapomuona.
MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI... AAMIN.