Mshitakiwa

Mshitakiwa

Makala imemu expose Seif Shariff vibaya.Inamuonyesha ni mtu kigeugeu na mwenye roho ya usaliti kwa tamaa ya madraka.Na pia imemuonyesha kuwa ni mnafiki na mtu asiyeaminika.
 
Kama ni kauli na vitendo tafauti hebu tuyaanze na kauli zake huyu kijana Nape, ile dhana ya kujivua gamba imefikia wapi? wale aliowanadi ati wezi na mafisadi si ndio hao hao anaokumbatiana nao na kucheka nao..jee yuko credible kuwajadili wengine wakati yeye mwenyewe amekosa standard na werevu wa siasa za kweli, haki na uadilifu. Kuna siku alisisimama Zanzibar na kuwaambia vijana wa CCM kuwashughulikia kwanza wale wote wanaowapinga halafu ndio waachiwe vyombo vya sharia vifanye kazi. Hana uhalali wa kuwasema wengine ikiwa yeye mwenyewe ni hypocrite mkubwa..
 
Kama ni kauli na vitendo tafauti hebu tuyaanze na kauli zake huyu kijana Nape, ile dhana ya kujivua gamba imefikia wapi? wale aliowanadi ati wezi na mafisadi si ndio hao hao anaokumbatiana nao na kucheka nao..jee yuko credible kuwajadili wengine wakati yeye mwenyewe amekosa standard na werevu wa siasa za kweli, haki na uadilifu. Kuna siku alisisimama Zanzibar na kuwaambia vijana wa CCM kuwashughulikia kwanza wale wote wanaowapinga halafu ndio waachiwe vyombo vya sharia vifanye kazi. Hana uhalali wa kuwasema wengine ikiwa yeye mwenyewe ni hypocrite mkubwa..
si unajuwa tena media zetu ni kama hakuna tu?hadi sasa kungetakiwa kuwepo na kipindi ambacho kinazungumzia,hata kwa dk moja tu,kuwa leo ni siku let's say ya mia mbili toka ccm wawape muda magamba ambao ndo wenye nguvu hivi sasa kwenye chama.
 
Nape hivi kuwadharau Watanganyika wezio ni moja ya ufahari kwako ?kwa kipindi kirefu hapa Jf watanganyika au tuseme waTanzania wamekuwa wakikuhoji mambo kadhaa yayotokea ndani ya nchi yanayohusu chama chako na Raia wasio na hatia, lakini umekuwa Du kimnya leo umezuka na (mambo ya Arba fogo wali pesa mbili) ili yale wanyoyataka jaamaa zako kujibiwa usijibu au usiyatolee ufafanuzi ,lakini kumbuka kifo cha nyani kinapofika miti yote huteleza, pia kumbuka watanganyiaka wa leo sio wale waliokuwa wakipelekwa Geza ulole kwenye vijiji vya ujamaa.
 
(makala hii imeandikwa na dr. Mohammed seif khatibu)

mwaka 1984, mkoani dodoma ndani ya ukumbi wa chama cha mapinduzi (ccm) kulikuwepo kesi kubwa. Kesi ya kiongozi wa juu wa serikali ya zanzibar. Alishitakiwa kwa kosa la kwenda kinyume cha òhati za muunganoó uliosainiwa na abeid amani karume na julius nyerere.

Mtuhumiwa, rais wa zanzibar, hakuwahi kujiandaa vyema na kufikisha hoja yake mbele ya mamlaka ya chama chake. Marafiki zake wa karibu walimuendea kinyume na kuiba waraka muhimu wa mashitaka katika shubaka la ikulu.

Bila shaka wale waliohusika walifanya wizi huu kwa siri kubwa kwani waraka wenyewe uliibiwa na kutolewa nakala na kurejeshwa ulipochukuliwa bila wahusika kujulikana. Waraka huo ukapelekwa butiama kwa mwalimu kwa ndege ya kukodi.

Njama hizo za kumwangamiza na kumtosa kiongozi huyo wa zanzibar katika majanga ilikuwa ajali kubwa ya kisiasa na ya kihistoria kutokea katika taifa letu. Mipango ikapangwa kesi ikadhihirishwa katika kikao cha chama na kuwa kama mahakama. Mshitakiwa ni rais wa zanzibar. Akasomewa mashitaka yake yote mbele ya viongozi wenzake katika ukumbi wa chuo cha cbe huko dodoma.

Mwendesha mashitaka dhidi ya rais wa zanzibar alijitokeza kwa haraka na kuona kama vile amepata bahati ya pekee. Sio mwingine ila alikuwa maalim seif. Akasimama kidete mbele ya hadhara na kuelezea kwa nini kiongozi huyo wa zanzibar amefanya kosa na dhambi kubwa ya kutaka kuubadilisha muundo wa muungano badala ya kuwa wa serikali mbili alitaka uwe wa serikali tatu kinyume na sera za chama.

Mwendesha mashitaka huyu kwa jasiri alijenga hoja zake za kutosha za kuonesha uzuri wa muungano, tija ya muungano wa serikali mbili na kwa nini kiongozi huyo wa juu wa zanzibar inapaswa achukuliwe hatua kali sana bila huruma!

Mwendesha mashitaka huyo akaungwa mkono sana na wafuasi wake akiwamo marehemu shaaban mloo. Mwendesha mashitaka huyo baadaye ikaonekana kuwa yeye ndiye aliyehusika mapema kuiba waraka huo katika shubaka au suraka ya huko ikulu.
Hivyo, basi alifanya kazi mbili za kuiba waraka na kumkabidhi nyerere na kusimama kama mwendesha mashitaka namba moja dhidi ya rais wake huyo. Mshitakiwa, rais wa zanzibar, kwa unyonge alikubali adhabu ya kujiuzulu kwa nafasi zake zote tatu. Urais wa zanzibar, makamu wa rais wa tanzania na umakamu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi.

Hakuruhusiwa kuishi zanzibar. Viongozi wenzake wa karibu, wote wakafuata nyayo zake za kujiuzulu akiwemo waziri kiongozi wake. Viongozi wake waandamizi wakawekwa katika vifungo vya nyumbani katika mikoa kadhaa ya tanzania bara.

Matokeo yote hayo, mabaya kwa rais wa zanzibar na wenzake ni kazi ònzurió ya kuiba nyaraka ikulu na kusimamia kidete mwendesha mashitaka huyu stadi, bingwa, mahiri na jasiri - maalim seif. Ni bahati mbaya kuwa mwendesha mashitaka huyo ni mwanafunzi wa mshitakiwa katika chuo cha lumumba.

Pia ni bahati mbaya mwendesha mashitaka alipewa nafasi ya masomo ya kwenda kusoma chuo kikuu cha dar es salaam na mshitakiwa. Ni bahati mbaya mwendesha mashitaka huyu alipewa kazi serikalini baada ya masomo na kumwingiza katika siasa na yeye mshitakiwa pia hata kufika nafasi aliyonayo sasa.

Hiyo ndio fadhila yake? Hiyo ndio ahsante yake? Ni bahati mbaya kuwa mwendesha mashitaka hivi sasa hayupo kizimbani kwa kutenda kosa na dhambi ileile aliyoifanya rais wa zanzibar aliyejiuzulu.

Mwendesha mashitaka huyu aliyetetea muungano wa serikali mbili kwa uchungu na hoja, leo amegeuka. Huyo ndiye leo anaongea hadharani kuwa sio tu anakataa serikali mbili bali anataka muungano huo adhimu uliomfikisha leo hapo alipo uvunjwe kabisa.

Yeye kama kiongozi wa juu na mtendaji mkuu wa chama chake anakwenda kinyume pia na sera ya chama chake ya muungano wa serikali tatu.

Hivi mwendesha mashitaka huyu wa kesi kama hii kwa nini na yeye asishitakiwe na chama chake? Uadilifu wake uko wapi? Ukweli wake uko wapi? Sheria si msumeno? Unafiki na uzandiki umemtawala. Mwendesha mashitaka ni mshitakiwa, afikishwe kizimbani. Anayo kesi ya kujibu.
kumbe ukitulia zina chaji..... Uchambuzi mzuri sana!! Sas kwa kuwa hicho chama ni mshirika wa chama chako kinachotetea muungano si muamrishe chama hicho kimchukulie hatua asiendelee kuwavuruga.
Kumbuka muungano ukivunjika mmeenda na maji maana huko zenji ndo mnakzoa kura......!!!!!
 
(makala hii imeandikwa na Dr. Mohammed Seif Khatibu)

MWAKA 1984, mkoani Dodoma ndani ya ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kulikuwepo kesi kubwa. Kesi ya kiongozi wa juu wa serikali ya Zanzibar. Alishitakiwa kwa kosa la kwenda kinyume cha Òhati za MuunganoÓ uliosainiwa na Abeid Amani Karume na Julius Nyerere.

Mtuhumiwa, Rais wa Zanzibar, hakuwahi kujiandaa vyema na kufikisha hoja yake mbele ya mamlaka ya Chama chake. Marafiki zake wa karibu walimuendea kinyume na kuiba waraka muhimu wa mashitaka katika shubaka la Ikulu.

Bila shaka wale waliohusika walifanya wizi huu kwa siri kubwa kwani waraka wenyewe uliibiwa na kutolewa nakala na kurejeshwa ulipochukuliwa bila wahusika kujulikana. Waraka huo ukapelekwa Butiama kwa Mwalimu kwa ndege ya kukodi.

Njama hizo za kumwangamiza na kumtosa kiongozi huyo wa Zanzibar katika majanga ilikuwa ajali kubwa ya kisiasa na ya kihistoria kutokea katika taifa letu. Mipango ikapangwa kesi ikadhihirishwa katika kikao cha Chama na kuwa kama mahakama. Mshitakiwa ni Rais wa Zanzibar. Akasomewa mashitaka yake yote mbele ya viongozi wenzake katika ukumbi wa Chuo cha CBE huko Dodoma.

Mwendesha mashitaka dhidi ya Rais wa Zanzibar alijitokeza kwa haraka na kuona kama vile amepata bahati ya pekee. Sio mwingine ila alikuwa Maalim Seif. Akasimama kidete mbele ya hadhara na kuelezea kwa nini kiongozi huyo wa Zanzibar amefanya kosa na dhambi kubwa ya kutaka kuubadilisha muundo wa Muungano badala ya kuwa wa serikali mbili alitaka uwe wa serikali tatu kinyume na sera za Chama.

Mwendesha mashitaka huyu kwa jasiri alijenga hoja zake za kutosha za kuonesha uzuri wa Muungano, tija ya Muungano wa Serikali mbili na kwa nini kiongozi huyo wa juu wa Zanzibar inapaswa achukuliwe hatua kali sana bila huruma!

Mwendesha mashitaka huyo akaungwa mkono sana na wafuasi wake akiwamo marehemu Shaaban Mloo. Mwendesha mashitaka huyo baadaye ikaonekana kuwa yeye ndiye aliyehusika mapema kuiba waraka huo katika shubaka au suraka ya huko Ikulu.
Hivyo, basi alifanya kazi mbili za kuiba waraka na kumkabidhi Nyerere na kusimama kama mwendesha mashitaka namba moja dhidi ya Rais wake huyo. Mshitakiwa, Rais wa Zanzibar, kwa unyonge alikubali adhabu ya kujiuzulu kwa nafasi zake zote tatu. urais wa Zanzibar, makamu wa rais wa Tanzania na umakamu mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi.

Hakuruhusiwa kuishi Zanzibar. Viongozi wenzake wa karibu, wote wakafuata nyayo zake za kujiuzulu akiwemo waziri kiongozi wake. Viongozi wake waandamizi wakawekwa katika vifungo vya nyumbani katika mikoa kadhaa ya Tanzania Bara.

Matokeo yote hayo, mabaya kwa Rais wa Zanzibar na wenzake ni kazi ÒnzuriÓ ya kuiba nyaraka Ikulu na kusimamia kidete Mwendesha Mashitaka huyu stadi, bingwa, mahiri na jasiri - Maalim Seif. Ni bahati mbaya kuwa mwendesha mashitaka huyo ni mwanafunzi wa mshitakiwa katika Chuo cha Lumumba.

Pia ni bahati mbaya mwendesha mashitaka alipewa nafasi ya masomo ya kwenda kusoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mshitakiwa. Ni bahati mbaya mwendesha mashitaka huyu alipewa kazi serikalini baada ya masomo na kumwingiza katika siasa na yeye mshitakiwa pia hata kufika nafasi aliyonayo sasa.

Hiyo ndio fadhila yake? Hiyo ndio ahsante yake? Ni bahati mbaya kuwa mwendesha mashitaka hivi sasa hayupo kizimbani kwa kutenda kosa na dhambi ileile aliyoifanya Rais wa Zanzibar aliyejiuzulu.

Mwendesha mashitaka huyu aliyetetea Muungano wa serikali mbili kwa uchungu na hoja, leo amegeuka. Huyo ndiye leo anaongea hadharani kuwa sio tu anakataa serikali mbili bali anataka Muungano huo adhimu uliomfikisha leo hapo alipo uvunjwe kabisa.

Yeye kama kiongozi wa juu na mtendaji mkuu wa chama chake anakwenda kinyume pia na sera ya Chama chake ya Muungano wa serikali tatu.

Hivi mwendesha mashitaka huyu wa kesi kama hii kwa nini na yeye asishitakiwe na chama chake? Uadilifu wake uko wapi? Ukweli wake uko wapi? Sheria si msumeno? Unafiki na uzandiki umemtawala. Mwendesha mashitaka ni mshitakiwa, afikishwe kizimbani. Anayo kesi ya kujibu.


Siasa kweli mchezo mchafu! Tangia Blaise Compaore aliposhiriki kumuua Thomas Sankara mimi nikasema siasa basi siitaki! Leo uko hivi kesho uko vile ili mradi upate mamlaka.
 
kwani mkuu wewe hujui Nape Nnauye anatumika na wakati mwingine anaongea tuuu, iko wapi falsafa ya kujivua gamba?? sijui imeishia wapi, kwenye kikao cha CCM mkoa nikiwa mjumbe nimewahi kuuliza bila kupata majibu...

Hizi falsafa huwa zinaenda kama fashen, zinakwenda na kurudi, wala hilo lisikupe shida.

Hilo la kutumika, najuwa kuwa yeye ana ajira pale CCM na ndipo anapopatumikia, au unamaanisha nini?
 
Hawa CCM wanfanya mambo ya ajabu sana....

Kwa nini awe mtuhumiwa leo wakati kosa lilifanyika miaka hiyo ya themanini na jamaa alionekana shujaa?

Why now?
 
Hana tofauti na Yuda Iskarioti, alisema "Yule nitakaye msalimia kwa kumbusu ndiye Yesu mkamateni"

Maalim Seif Sharif Hamad anahasira kwani alitarajia kwamba Mwl angemteua yeye kuwa Rais wa Zanzibar kwa kufanya kazi nzuri ya unafiki. Kumbe principles za Mwl ni kwamba "huyu aliyemsaliti mwenzie leo, kesho atakusaliti wewe"


haaaa Bora wewe umedadavua
Basi mie nilikuwa najiuliza ni nani huyu?
 
Ukitaka kujua kwamba mleta mada ni mpuuzi, check topic information....
Mleta mada hayumo kuchangia mada yake!
NEPI aaaaah, NAPE bwana!
 
hizo ni zama hizo na mzee nyerere saizi hii ni dunia ingine.....mkajipange tena alafu mrudi hapa na mshtakiwa na mwendasha mashtaka
 
Unajuwa huu ukumbi si zile maskani za vijana muliowanyima elimu na kuwaongoza katika propaganda za siasa chafu, fitna na fujo. Kwanza na tumjadili mwandishi wa hii article ambae ni Mhe Mohamed Seif Khatib na namna gani yeye mwenyewe aliandika shairi juu ya muungano na then tuweze kumpa benefit of doubt kama ni mtu msema kweli na mtetezi wa kweli chama na sera butu, au ndio kama anavyosema katika shairi lake hapo chini: Shairi la Mohamed Seif Khatib kutoka kitabu chake cha Wasakatonge shairi No 4 pg 3 :

KOSA?
1. Metufunga kamba,
Za miguuni,
Za mikononi,
Za midomoni,
Na kututosa baharini !
2. Eti mnataka,
... Tuogelee,
Tujongelee,
Tujiokoe,
Hadi tufike ufukweni !
3. Kosa letu kubwa,
Kudai haki?
Yetu miliki?
Mna hamaki,
Na huku mnatukashifu !
4. Msitunyanyase,
Siyo watwana,
Watu wa mana,
Tuloungana,
Kwa heshima na taadhima!

5. Sisi tuna kwetu,
Wenye asili,
Ilo kamili,
Na serikali
Ilopatikana kwa damu !
6. Kuheshimiana,
Kwa kupendana,
Kuelewana,
Kusikizana
Hilo tutakubaliana ! Waungwana hawa ndio akina Nape na genge lao, hili shairi aliliandika Mhe Mohamed Seif Khatib katika kitabu chake kinachoitwa WASAKA TONGE ..

Da form 3 nilikutana na ii kitu..umenikumbusha mbali sana
 
Huyu Maalim Seif kwa Usaliti aliomfanyia mwenzake hafai kabisa kuwa kiongozi Mkubwa, anaweza kuisaliti na kuiuza nchi huyu Bwana..
 
Enyi kizazi cha nyoka, mtu akikubeba sio tiketi ya kumfichia maovu yake, hii ndio inaiua ccm sasa watu wamebebwa na wanaendelea kubebana na kufichiana maovu. Nape Nnauye ulitaka Seif alipe fadhila gani kwa mouvu au atoe asante gani? Ukitetea uovu utaendelea kuwa mtumwa wa uovu Nape.

Nape Nnauye sasa hivi hatuzungumzii sera za chama tunazungumzia katiba ya nchi, unafahamu kwamba katiba ni sheria ya mama, sera za chama haziwezi ku influence mawaza ya mtu juu ya rasimu ya katiba. Kama ndio hivyo tungechukua sera za chako ndio ziwe katiba ya nchi.
 
Last edited by a moderator:
Huyu Maalim Seif kwa Usaliti aliomfanyia mwenzake hafai kabisa kuwa kiongozi Mkubwa, anaweza kuisaliti na kuiuza nchi huyu Bwana..

Kikwete pia kauza nchi kwa obama na mafisadi je atashitakiwa lini?
 
Huyu Maalim Seif kwa Usaliti aliomfanyia mwenzake hafai kabisa kuwa kiongozi Mkubwa, anaweza kuisaliti na kuiuza nchi huyu Bwana..

Hapa Msaliti alikuwa nani Seif au Abood, kwa mtazamo wangu Abood ndio alikuwa anafanya njama za chinichini ili aue muungano na ndio alikuwa msaliti na alistahili kupata adhabu kali sana.
 
Back
Top Bottom