Watu wana hela hawana mawazo. Watu hawana hela wana mawazo lukuki.
Nipe milion 50 baada ya miaka miwili nikurudishie milion 500.
Mnamo tarehe 11.12.2014 Big Brother Africa ilipata mshindi mpya wa season 8, na mshindi hiyo alitokea Tanzania akijulikana kwa jina Idris Sultan. Mshindi alijishindia $ 300,000 takribani Million 500 za kibongo..
Tangia ametoka kwenye nyumba wengi walisubiri waone ni kipi atakifanya na hiyo pesa.. Lakini kijana kajibu mapigo, kaja na clothing line business.. Hii idea yake imebishangaza sana na ikabidi nijiulize maswali kadhaa;
1. Is his idea viable?? Yaani pamoja na kupata mkwanja mrefu hivo ameishia kufikiri that low....
2. Kuna clothing line (brand) yeyote ya Africa inayojulikana na yenye nguvu sokoni??
3. Mwaka jana mshiriki mwenzake Army Nando alivyotolewa pia alianzisha ya kwake, naweza kusema Nando alikuwa anapendwa na alikua na fans wengi kuliko Idris Lakini hizo T-shirt aliishia kuvaa mwenyewe na hiyo biashara yake haipo tena..
Watanzania lazima tujifunze kuwa creative na tufanye research kabla ya kuanzisha biashara yoyote. Asione ana fans wengi huko kwenye mitandao ya kijamii akajua ashapata uhakika wa soko lake.
Wadau mbalimbali walimshauri alivyopata hizo pesa arudi kwao Arusha au atafute mji wowote unaukuwa kiuchumi kama Mwanza, Mtwara, Dodoma, Mbeya akafanye investment huko. Lakini naona kaamua kukomaa na jiji... Kazi kwake
Watu wana hela hawana mawazo. Watu hawana hela wana mawazo lukuki.
Nipe milion 50 baada ya miaka miwili nikurudishie milion 500.
Pesa hiyo angejenga uswahilini
nyumba za kutosha za hali ya chini.
Kila mwisho wa mwezi angekuwa na uhakika
wa kuingiza senti.
Na kwa baadae angekaa kibarazani kajifunga
msuli anakula kichwa cha samaki mkavu
ghahwa, kashata na tende.
''Life is criminal''
Ndg. Idris seems ana akili ya maisha tofauti na mastaa wengi wa Bongo (Diamond excluded). Mbali na hivyo akiamua kula/kuto.mbea hela yote ni Sawa tu,hakuna kesi
wewe ni noma ma bank yangekua yanakugombania that a huge lie
Hela ni zake, wacha afanye yake. tutafute zetu tufanye yetu.
DON FRANCIS
Bongo movie kweli hazieleweki hapo namuunga mkono.Alisema atafika Hollywood kabla ya miaka mitatu.. Lakini cha kushangaza kawaponda Bongo Movie na kasema hayuko tayari kufanya nao kazi kwasababu kazi zao hazieleweki.. Nilifiki angetumia ujuzi aliofundishwa kule ndani kuwatengeneza bongo movie pamoja na kuinua sanaa yetu.. Sasa sujui atafikaje huko Hollywood
si chumba na sebule tu.500m unafikiri atapata chumba na sebule ngapi?! Itamchukua miaka mingi sana kurejesha hiyo pesa.
Mimi naona yuko sahihi, sidhani kama mayai yake yote ameyaweka kwenye kapu moja.