Mshauri wa CCM na Msekwa: JamiiForums tishio kwa CCM; wadai ni ya CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Hata hao consultants wanao tumiwa na ccm mimi nawatilia shaka..
Na ndi hao mara nyingi wanategemewa kusukuma hili gurudumu letu la maendeleo
 
Leo nimekuwa msomaji zaidi, nimegundua watu wengi mnaifahamu JF. Zaidi ya nilivyodhania mwanzo.

Inasikitisha members wengine hapa pamoja na kuwa wao ndio wanaandika hoja zao wanataka iaminike kuwa waendeshaji ndio wanaopanga nini kijadiliwe; ni uzushi usio na ukweli.

Hivi hawa hawa wana JF wangekuwa ni mali ya CDM, jana na juzi wangehangaika kufuatilia kinachojiri Dodoma kwenye shughuli ya CCM? Si wangehakikisha hakisikiki kabisa? Naamini kuwa wengi ni wazalendo, walikuwa wanataka kujua hatma ya CCM, hatma ya taifa (kwa kuwa ndicho chama tawala).

Mshauri huyu wa CCM alifanya kazi yake, kwa kutafuta ujira wake. Wasiwasi wangu ni kuwa kama mambo yote kafanya kwa mtindo huu basi viongozi wa juu wa CCM wamenyweshwa 'sumu' na kuna watu watakuwa wameonewa sana, msishangae baadae kukaibuka mvurugano mzito ndani ya CCM ambao kuzimika unaweza kuwa kazi kubwa na kupelekea kumegeka kwa chama.

Yangu mie macho
 
  • Thanks
Reactions: Paw
CCM wameshindwa kusoma nyakati, watu wemeshajua porojo za magazeti sasa wamehamia kwenye free journalism ambapo hakuna filters. Unasema JF, nenda kaangalie Kumekucha ya hapo Kenya uone jinsi moto unawaka huko.

CCM wanamtafuta mchawi kwenye chumba cha mama mkwe, watampata tuu. Tulipo kuwa Youngafrican kule midahalo mizito ilikuwa ni jinsi ya kujikwamua kiuchumi, ambapo CCM wengi vijana walikuwa wanachangia. Lakini walipopata nafasi kwenye serikali hayo yote yamepotea, JF imeleta enzi mpya ambapo hata matonya kule Dodoma anaweza kusema analoona ni bora na Mwasiti kule Kigoma akalisoma.... Hiyo ndio CCM wameshindwa kujua.......

Wakaanzishe CCMforums kisha waone kama zidumu fikira za mwenyekiti zitawafikisha hata asubuhi.
 
..mabilioni waliyotumia wakati wa uchaguzi mkuu bado wana wasiwasi CDM inapata wapi pesa!!
 
Hili wote tulioko JF tulilitegemea muda mrefu ila sikutegemea litakuja kupitia kwa wataalamu na wasomi waliobobea. Tuna shida kubwa zaidi ya hii tunayoiona kwa sasa.
 
Leo nimekuwa msomaji zaidi, nimegundua watu wengi mnaifahamu JF. Zaidi ya nilivyodhania mwanzo.

Inasikitisha members wengine hapa pamoja na kuwa wao ndio wanaandika hoja zao wanataka iaminike kuwa waendeshaji ndio wanaopanga nini kijadiliwe; ni uzushi usio na ukweli.

Hivi hawa hawa wana JF wangekuwa ni mali ya CDM, jana na juzi wangehangaika kufuatilia kinachojiri Dodoma kwenye shughuli ya CCM? Si wangehakikisha hakisikiki kabisa? Naamini kuwa wengi ni wazalendo, walikuwa wanataka kujua hatma ya CCM, hatma ya taifa (kwa kuwa ndicho chama tawala).

Mshauri huyu wa CCM alifanya kazi yake, kwa kutafuta ujira wake. Wasiwasi wangu ni kuwa kama mambo yote kafanya kwa mtindo huu basi viongozi wa juu wa CCM wamenyweshwa 'sumu' na kuna watu watakuwa wameonewa sana, msishangae baadae kukaibuka mvurugano mzito ndani ya CCM ambao kuzimika unaweza kuwa kazi kubwa na kupelekea kumegeka kwa chama.

Yangu mie macho

mkuu ni sawa kabisas!

Labda point nyingine ni kutokana na viongozi waandamizi wa CDM mara kwa mara kujitokeza hapa Jamvini kama Zitto, Regia Mtea,Dr. Slaa na wengineo.

Walichofanya CDM ni kutumia opportunity iliyojitokeza kuweza kupata mawazo ya wasomi ambao wengi wao hukutanishwa mahali hapa.

Ingekuwa ni vyema kama vyama vingine basi vikatumia nafasi hii, ikiwezekana kwa viongozi wao waandamizi kujibu au kutolea ufafanuzi wa baadhi ya hoja kama wanavyofanya CDM.

nafikiri CCM inabidi wakae chini na wajiulize, watafute busara ya kutafuta namna ya kujipenyeza kwenye jamii bila kudharau. Hebu pata picha kama Makamba au Chiligati angekuwa anajibu hoja humu ndani, sidhani wangefika hapo walipofika.

Sisemi ni lazima wafanye hivyo, isipokuwa waache kufanya mambo mengi kisiri siri, hii ni demokrasia, na chama ni vizuri kikawajibika kwa wananchi kwa kutumia njia zozote zinazowezekana.

Inawezekana chuki wanayoipata hapa huenda siku moja ikahamia CDM, CUF au NCCR. Watu kamwe hawataacha kuikosa serikali na vyombo vyake.

CCM imeipa CHADEMA heshima isiyostahili. Sidhani ni kweli CDM wamepata nguvu kiasi cha kushika maeneo yote yanayoonekana yana upinzani.

Angalizo pia kwa CDM, kwamba wasibweteke na kila kinachoendelea hapa JF, wengi ni washabiki tu ambao kesho wanaweza kushabikia upande mwingine.

Pia heshima kwa JF kutoka kwa CCM naona pia imezidi mno. Sidhani kundi la watu hawa humu jamvini likawa na athari kwa nchi nzima kwa maana ya kuiporomosha heshima ya CCM. Wapiga kura wengi wako vijijini ambao hawajui hata maana ya Internet. Na pia ni sehemu ndogo sana ya Watanzania wenye uwezo wa kupata huduma ya internet achilia mbali kupenda siasa. Hivyo basi ni kuitwisha mzigo JF na wamiliki wake ambao hauna mantiki yoyote.
 
Always the blame lies with somebody else.

CCM wanatakiwa kuweka mikakati thabiti ya kuweza kushinda 2015. Kitu kimoja ambacho waelewe ni kuwa, siku zinavyozidi kwenda, wao ndio wanazidi kupoteza wapiga kura. Sababu moja ni kwamba, vijana walio na miaka 13 mpaka 17, ambao walikuwa hawajafikia umri wa kupiga kura kwenye uchaguzi uliopita, watakuwa wamefikia huo umri. Na hawa vijana wengi wako kwenye households ambazo zimeichoka CCM. Kila kukicha wanawasikia wazazi wao wakilalamika kuhusu maisha magumu, ufisadi, mabomu, umeme..nk, vyote vilivyosababishwa na CCM.

Kwa hiyo ni dhahiri, wakati wao wa kupiga kura ukifika, hawataipigia CCM, na hawa vijana kwenye hii age bracket ni wengi. Wao wanataka kubaki kuilaumu JF. Lakini hata kwa mfano ni ya Chadema, so what? Ni sawa na kulalamika kuwa Barcelona wana Messi! Sasa asicheze, au wamevunja sheria?
Point noted,JK ama Makamba wameshazuiliwa kujiunga JF kama Slaa na wengineo?
 
Magazeti mengi yana longo longo na habari za kuwafeva baadhi ya watu kutokana na matakwa yao, ndio maana jamii yote sasa hivi inahamia kwenye free media na journalism huku hakuna longo longo ,na kwanza vigazeti vyao vingi wanachukua taarifa kutoka hapa JF.

JF is everything
 
Inamaana CCM wanashindwa kujua kwamba JF ni mkusanyiko wa wananchi ambao wamepewa uhuru wa kutoa maoni yao bila kuchujwa? kama wanahisi JF ni hasimu wao, basi ni sawa na kusema wananchi wote ambao hatukubaliani na uongozi wao ni mahasimu wao.

Waende wakamwage hizo pesa kufungua website zao za kupambana na JF na wasisahau KUANDAA PESA ZA KUWANUNUA WATOA MAONI WA KUSUPPORT UCHAFU WAO. Hapa wananchi wako uhuru kutoa maoni. Sidhani hizo website zao zitakosa maoni yanayotolewa hapa JF kama hawata chuja. Wamuulize michuzi anachuja maoni mangapi kwa siku yanayopinga uchafu wa ccm.
 
Kuuza VIWANJA vya Michezo?

Lini hiyo wanataka kufanya? Hiyo nayo itabidi sisi wa Tabora tugome maana tulijenga wote.

Hapa itabidi Wanaharakati na Chadema wapeleke kesi mahakamani na kuwaambia watu wowote wanaotaka kununua viwanja kuwa kuna siku watanyang'anywa maana ni MALI ya Wananchi na CCM imefanya kutumia mabavu kama Gbagbo na kujichukulia Nchi na viwanja vyake.

Hili inabidi kulifungulia thread yake PEKE yake kama kweli CCM wanataka kufanya upuuzi huo.....

Mkuu umenikumbusha mbali sana kuhusu hivi viwanja. Nakumbuka wakati nikiwa pale Tabora watu tulikuwa tunatozwa shilingi moja moja kwa kila kitu unachonunua eti ni mchango wa uwanja.

Nakumbuka enzi hizo marehemu Laurence Mtazama Gama (RIP) ndiyo alikuwa mkuu wa mkoa na kuipandisha daraja timu ya Milambo na kuhamasisha wapenzi wa michezo kuchangia. Kitu ambacho CCM watasema chao ni kuwa uchangiaji ulipata kasi kuelekea kumbukumbu ya miaka 11 ya CCM iliyofanyikia pale Tabora mwaka 1988, Ila swali ni je zile shilingi moja moja za kwenye vibaba vya mafuta ya taa, sabuni, soda etc zilikuwa zinakatwa kwa watu wenye kadi za CCM tu?, jibu ni no, na hivyo uwanja ule ni wa wanatabora siyo wa CCM.

Ole wake atakayenunua viwanja hivi ambavyo CCM inasema vyake, ajue kuwa siku moja wenyewe watachukua mali yao.
 
kaazi kwelikweli mpaka ifike 2015 sijui tutaona na kusikia mangapi, ngoja na mimi niwahi kwa babu nikapate kikombe niwe na uhakika wa kuyashuhudia yanayoendelea mpaka hiyo 2015
 
huko ccm kuna vituko. hivi hao consultants wamepewa million mia ngapi hadi walipokabidhi ripoti hii?
 
Hata hao consultants wanao tumiwa na ccm mimi nawatilia shaka..
Na ndi hao mara nyingi wanategemewa kusukuma hili gurudumu letu la maendeleo

fred unazikumbuka synovate na redet, wao wanapenda za hivyo, wanapenda kusikia wanachopenda kuambiwa.

Katika ripoti hiyo, kwa mfano mtandao wa Jamii Forum unatajwa kuwa unamilikiwa na Chadema na kwamba umetumiwa sana kuichafua CCM ndani na nje ya nchi. inahuu!!!!!
 
Magazeti mengi yana longo longo na habari za kuwafeva baadhi ya watu kutokana na matakwa yao, ndio maana jamii yote sasa hivi inahamia kwenye free media na journalism huku hakuna longo longo ,na kwanza vigazeti vyao vingi wanachukua taarifa kutoka hapa JF.

JF is everything

Kwangu JF ndio tv, radio, gazeti, jarida na kila kitu. Nikiamka tu nawasha LT yangu naanza kuvinjari, kuvinjari (browse)
 
Huu ni UJINGA wa hali ya juu. Yaani mie kuwa JF tayari nimekuwa MALI ya Chadema?

Mtu mwenyewe hata Kadi ya chama chochote sina na leo unaambiwa "umemilikiwa na Chadema."

JF ni watu na wala siyo Maxence Melo au sijui nani. Wale ni wadhamini wetu tu.

Ukitaka kuamini hilo, jiulize kitu kimoja: Kuna forum nyingi sana za Watanzania na Blog kibao ila kwa nini JF ndiyo inatesa namna hiyo? Ni kwa makala za wadhamini wa JF au MEMBERS wa JF?

Michuzi Blog ingeliweza kuwa kwenye nafasi ya JF leo hii ila kutokana na Michuzi kubania thread za watu na comments za watu, Michuzi blog imebakia kuwa kama kitawi cha CCM na Bwawa la Maini. Blog nyingine ya wauza nywele nayo iko juu na sababu ni kuwa wanafanya vizuri sana katika Issue ambazo wameamua wazifanye. Hata Ze-Utamu na yeye alifanikiwa saaana kwa sababu HAKUBANIA habari za watu.

JF imekuwa wazi kwa watu na kuachia habari ziandikwe na kuachwa hata kama ni SIRI NZITO ya Serikali. Zimeondoloewa tu zile ambazo au zinatukana au zina majungu. Kuachia habari huku zisomwe na watu wote wanaoingia JF ndiyo kumeifanya JF iwe hapo ilipo na kuwapa SIFA za UJASIRI wadhamini wa JF.

Ila leo mtu akija na kusema JF ni mali ya Chadema ni sawa na kusifia Jiko fulani linapika vizuri na LIMEDHAMINIWA na fulani na unasahau kuwa WAPISHI wake wakihama, jiko litabako historia. Wanataka kusema mtu kama FMes ni Chadema? Kibunango ni Chadema? Malaria Sugu, Mwiba, Junius, Kishonga, Ndalu, Tumaini, Ngongo, X-Pasters na wengine wengi wanaoshinda hapa wakimtukana Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla na wao wamekuwa ni Chadema?

Hebu mwangalia Waberoya na makala zake, unataka kusema huyo ni Chadema?

Kweli MFA MAJI, HAACHI KUTAPATAPA.......... Atashika hata kitoto cha Ndege/bata ili asizame.

Sikonge,

Kama ungekuwa uko kitandani unafanya mapenzi, ningekwambia umegonga kuta zote. Sina zaidi cha kuelezea the way ulivyoeleza.
Nakugongea "AHSANTE"
 
Mkuu,

Nilicheka tu baada ya kuiona hii habari lakini nikaja kuwaza sana; hivi CCM wanadanganywa kiasi hiki? Hawa 'consultants' wanatumia vigezo gani kuwasilisha maoni yao kwa viongozi wetu wa kitaifa?

CHADEMA wanapewa credit nyingi ambazo hata mtu huwezi kuamini kama wanapewa; ni wazi CCM wanaiogopa CHADEMA sasa kwa kuamini ina hela nyingi sana mpaka inaweza kufadhili vitu vingi tu.

Twitter, FaceBook etc nazo naona zinawatisha CCM kwa ushauri huu wa 'consultant'; huu ni upotoshaji wa wazi. Nilikuwa napuuzia lakini nahisi kuna tatizo ambalo linatakiwa kuwa addressed kwa viongozi wa kiserikali na hata vyama, hivi wao ni vilaza kuambiwa uwongo wa mchana na kuuamini?

Nina wasiwasi 'consultants' hawa wanafanya kazi kwa hisia tu

Mkuu mbona unashangaa viongozi wetu kudanganywa? mbona wanadanganywa siku nyingi tu na wao wanakubali kudanganyika kama watoto wadogo...
 
Tuwapeni tu pole CCM kwani tayari wana ugonjwa wa kufisha na wako ICU. Wanajaribu kutumia mashine za oxygen na kujishtua ili warudie uhai lakini ukweli ni kwamba hata wakiamua kwenda loliondo watapata kikombe na baada ya dakika chache watakata roho. JK hawezi ifufua CCm kwani ipo kwenye point of no RETURN.
 
mkuu ni sawa kabisas!

Labda point nyingine ni kutokana na viongozi waandamizi wa CDM mara kwa mara kujitokeza hapa Jamvini kama Zitto, Regia Mtea,Dr. Slaa na wengineo.

Walichofanya CDM ni kutumia opportunity iliyojitokeza kuweza kupata mawazo ya wasomi ambao wengi wao hukutanishwa mahali hapa.

Ingekuwa ni vyema kama vyama vingine basi vikatumia nafasi hii, ikiwezekana kwa viongozi wao waandamizi kujibu au kutolea ufafanuzi wa baadhi ya hoja kama wanavyofanya CDM.

nafikiri CCM inabidi wakae chini na wajiulize, watafute busara ya kutafuta namna ya kujipenyeza kwenye jamii bila kudharau. Hebu pata picha kama Makamba au Chiligati angekuwa anajibu hoja humu ndani, sidhani wangefika hapo walipofika.

Sisemi ni lazima wafanye hivyo, isipokuwa waache kufanya mambo mengi kisiri siri, hii ni demokrasia, na chama ni vizuri kikawajibika kwa wananchi kwa kutumia njia zozote zinazowezekana.

Inawezekana chuki wanayoipata hapa huenda siku moja ikahamia CDM, CUF au NCCR. Watu kamwe hawataacha kuikosa serikali na vyombo vyake.

CCM imeipa CHADEMA heshima isiyostahili. Sidhani ni kweli CDM wamepata nguvu kiasi cha kushika maeneo yote yanayoonekana yana upinzani.

Angalizo pia kwa CDM, kwamba wasibweteke na kila kinachoendelea hapa JF, wengi ni washabiki tu ambao kesho wanaweza kushabikia upande mwingine.

Pia heshima kwa JF kutoka kwa CCM naona pia imezidi mno. Sidhani kundi la watu hawa humu jamvini likawa na athari kwa nchi nzima kwa maana ya kuiporomosha heshima ya CCM. Wapiga kura wengi wako vijijini ambao hawajui hata maana ya Internet. Na pia ni sehemu ndogo sana ya Watanzania wenye uwezo wa kupata huduma ya internet achilia mbali kupenda siasa. Hivyo basi ni kuitwisha mzigo JF na wamiliki wake ambao hauna mantiki yoyote.

Ushauri mzuri lakini nani ndani ya CCM anaweza ingia hapa JF kwa ID yake? Wanajua kabisa hawakubaliki na elites wenye free mind, wamezoea kuwasikiliza elites wenye stake kwenye government ambao wengi wao wanashindwa kueleza ukweli kutokana na mfumo wa CCM wa ku victimize badala ya ku acknowledge when they make a mistake. CCm dominat system imejengwa kwenye ideology ya zidumu fikra sahihi za kiongozi na wameshindwa kubadilika hata baada ya vita baridi kuisha na kuenda wa wakati wa ICT era ambapo access to information iko so wide. Huhitaji kumwambia mtu kijijini kuwa maisha anayoishi hayafanani na binadamu wengine kwani wana ona through television what are other people doing in various part of the world. TV ziko mpaka rural; simu etc sasa leo utamdanganya nani?

CCM is gone my friends tuisaidie tu nchi yetu maana wengi wa seniors in government na ambao ndiyo inaunda CCM elites hawatapenda kubadili status quo maana wakibadili wao wata fall a victim. While this is so wengi wa growing elites wameachwa nje ya mfumo kwani uchumi wetu marginal productivity ni almost zero so demand is bigger than supply so haiwezekani kuingizwa katika system maana the dominant system of push (supply) and pull (demand) is unbalanced ndiyo maana hata budget haijitoshelezi.

Mpaka viongozi wachache wenye power wakubali to let it go ili watu tujenge mfumo ambao you are paid for what you produce hakuna tumaini ndani ya CCM itajivua magamba yote na mwisho ita end up into natural death. Five years from now labour market ya ualimu ambayo ndiyo mwajiri mkuu itakuwa saturated; sasa fikiria hao graduates after hiyo saturation level kufikiwa watapelekwa wapi? Its a time bomb hakuna mchawi wa CCM they are bewitching themselves kwa action zao zilizopitwa na wakati. Wakae pembeni tuwaonyeshe njia; so far CHADEMA watakuwa na nguvu kwa sababu kina fanya vizuri katika ku tap vijana ambao wako ambitious na ambao wanakuwa led na viongozi ambao ni wasomi, exposed na experienced katika struggles kinyume na CCM ambao wengi wamepata nafasi kwa kubebwa na siyo kwa merits.
 
Uongozi wa CCM,

Wapelekeni hao wazee kozi ya computer na wao waje wajiandikishe hapa wawe wanajibu hoja na sio kuendeleza usanii kila kukicha. Kama wakina Msekwa; Kingunge, Makamba na wengineo mgekuwa members wa JF si mgekuwa mnatoa majibu ya hoja mnayotupiwa.

kila la Kheri endeleeni kumtafuta Mchawi ili khali mnajua fika MAdikteta BEN ALI, HOSNI MUBARAK waliondolewa madarakani kwa nguvu ya FACEBOOK,TWITTER. mtapambana na JF je FB na Twitter mtafanyaje?

Yetu Macho
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom