chinchilla coat
JF-Expert Member
- May 16, 2016
- 5,107
- 10,981
kuweni wapole
fanya ujasiriamali usitegemee mshaharaJamani mbona mshahara wa mwezi huu umepungua na hakuna ongezeko lolote!
Kuwa na mshahara wa serikali usifikiri hatufanyi ujasiliamali.watumishi wa serikali waliowengi mbona wana miradi yao mingi tu.fanya ujasiriamali usitegemee mshahara
Salary out lakini hakuna nyongeza yoyote. Acha tuisome 1 3 47889
Wewe nawe unashangaza jamii. Sasa kama hizo pesa ni kidogo wewe ungesusa tu huo mshiko au ungezichukua kisha kuzichana mbele ya bosi wako huku ukimtukana kuwa huwezi ishi kwa mshahara huo ukizingatia una machangu na mke wa ndoa unaowatunza. Kwa vyovyote angekuonea huruma na kukuongezea mshahara.
Unapozungumzia wafanyakazi, ondoa waalimu maana wao kama wamerogezewa hivi.endapo mwezi huu usipokuwa na nyongeza ya mshahara nashauri wafanyakazi wagome na waingie barabarani na mabango ya kutosha kama sheria yao inavyosema...maana hadi sasa TUCTA ipo kimya maana raisi Wa CWT ndio huyo huyo Wa TuCTA sasa tusitegemee lolote kutoka kwake...haiwezekani mfanyakazi awe na mshahara huo huo kwa miezi 14+ huku bei ya vitu ikipanda Mara dufu....huu ni uuaji.
wafanyakazi amkeni..tuungane October...
Kabla ya kugoma wafikirie kwanza.kwamba kama wakiondolewa serikali itapata hasara gani???
Unaweza goma kesho unafika getini mlinzi anakukabidhi barua ya kufukuzwa kazi.