Mshahara umetoka lakini hauna nyongeza

Mshahara umetoka lakini hauna nyongeza

Naombeni msaada wakuu,nimehamisha pesa kutoka Nmb mobile,kuileta M _pesa..lakin haijaja ila salio kwa account limekatwa.nafanyeje?
Wapigie kitengo Huduma kwa Wateja cha Benji ya NMB,watakusaidia.
 
Mnasema kipindi cha awamu ya 4 ufisadi ulikua umeshika hatamu, lakini cha kushangaza mishahara ilikua mitamu mno. Kila mwaka lakini itabidi tusubiri viwanda vianze kufanya kazi, mmh nimekumbuka jamani hivi ile sukari imeshuka bei?
 
Dah naona hela ni ile ile japo wametoa 2%
Reflection ya hiyo 2% ni only Tshs 3,800/-. So changes utaziona sio kwenye Malaki wala Ma Kumi Elfu, la hasha, ni kwenye maelfu tu!!
 
Mliahidiwa nyongeza??
sio suala la Ahadi hapa, Magu Mwenyewe haya aliyakuta angeyaacha kama yalivyo! Mikataba yetu ya ajira inasema kila tar 01 July kutakua na incerement, na mikataba hii imesainiwa na Mwajiri kama ishara ya kukubali kutekeleza hilo kwaiyo kwa hili Mkulu amevinja makubaliano
 
Ulimuelewa vizuri hapa kazi? alisema kwanza anapambana na hewa ya hydrogen peroxide akishaasafisha ndio mambo mazuri yatakuja kwale pyurities. Hivyo muwe na subira miezi miwili aliyoahidi mbado cha msingi chapa kazi kwa juhudi na maarifa.
Ni uchungu sana Mtu kufanya kazi vile anavyotaka yeye badala ya kufuata na kuheshimu ymutaratibu iyo 2% ya Kodi aliyotupunguzia angeiacha tu ila angefuata utaratibu wa kutufuta machozi hata ya kutuongezea fedha ya Mafuta litre 1
 
wale waliokua waneshusha madaraja yao mapya wamerudishiwa madaraja
 
Naombeni msaada wakuu,nimehamisha pesa kutoka Nmb mobile,kuileta M _pesa..lakin haijaja ila salio kwa account limekatwa.nafanyeje?
Usipende kufanya muamala kwa nmb mobile tarehe hizi ni usumbufu sana
 
Kweli niliyo yakuta ATM NMB TARIME yanaleta STRESS nimekuta ongezeko LA 5000 kwenye posho yangu ya Kila mwezi nikiwa NA TGTS D, nimechukua hako ka posho kote nikakafinyanga na kukaweka mfukoni.

Lengo la kukakomba kote ni kwanza kiduchu na pili Mzee wa mwendo kasi anaweza kuamuru karejeshwe hazina ksmetolewa ki makosa. Waswahili husema Mkamateni si mtafuteni.

Baadae nikakaa kwenye msingi wa benki nikiwa nimejishika shavu utadhani nimetangaziwa siku ya kufa. Baada ya kama nusu SAA mlinzi wa pale Benki alinitimua kuwa siruhusiwi kuketi pale.

Nauliza kama kuna wasaidizi wa Magufuli humu kuwa ndio amefikia mwisho au alikuwa anabipu atatupigia watumishi wa umma hasa walimu? Amedhamiria au anatania?
 
Back
Top Bottom