Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 302
Kama ni kosa la kiufundi walilofanya CCM ni kumteua kada wao na mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Abdulrahman Kinana kuwa msemaji mkuu wa kampeni ya Kikwete.
Post hiyo muhimu ilitakiwa ijazwe na mtu safi asiye na doa kwa vile anakuwa ni kioo cha chama husika.
Mbali na utata wa uraia wa Kinana inasemekana vyombo vyake binafsi anaviruhusu kufanya biashara haramu ikiwemo ya usafirishaji wa meno ya Tembo nje ya nchi.
Ingawa Kinana anasema hahusiki na biashara hiyo lakini amekiri kuwa ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya uwakala wa meli ya Sharaf Shipping Agency, iliyohusika kusafirisha makontena yaliyokuwa na nyara za serikali mwaka jana, kabla ya kukamatwa nchini China yakiwa safarini kupelekekwa Hong Kong.
Nasema ni kosa kubwa la CCM kwa sababu kama Kinana ni msemaji wa Chama na yeye tayari ana madoa,atawezaje kutetea sera ya maliasili inayohubiriwa na viongozi wake na makombora yanayorushwa na wapinzani wao likiwamo la JK kuhusika kwenye wizi wa pesa za EPA?
Badala ya yeye kuwa mtetezi wao inabidi mwenyewe aanze kwanza kujisafisha kuwa hahusiki na vitendo hivyo viovu kabla ya kukisemea chama.
Uraia wake bado ni kitendawili, watu wanasema ana asili ya Kisomali na tujuavyo wasomali wengi wanajihusisha na vitendo vya ujangili ukiwemo utekaji nyara wa meli za mizigo.
Kwa mwananchi wa kawaida ni vigumu sana kukubali au kutenganisha biashara yake ya meli na ujangili unaofanywa na watu wa jamii hiyo.
Nauliza hivi CCM walikosa mwanachama mtanzania halisi mwenye uraia usio na utata mwenye biashara isiyo na utata, kuwa msemaji wa chama wakaishia kutuletea Kinana anayeshirikiana na majangili kwa kuruhusu vyombo vyake kuihujumu nchi anayodai kuitetea?
Post hiyo muhimu ilitakiwa ijazwe na mtu safi asiye na doa kwa vile anakuwa ni kioo cha chama husika.
Mbali na utata wa uraia wa Kinana inasemekana vyombo vyake binafsi anaviruhusu kufanya biashara haramu ikiwemo ya usafirishaji wa meno ya Tembo nje ya nchi.
Ingawa Kinana anasema hahusiki na biashara hiyo lakini amekiri kuwa ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya uwakala wa meli ya Sharaf Shipping Agency, iliyohusika kusafirisha makontena yaliyokuwa na nyara za serikali mwaka jana, kabla ya kukamatwa nchini China yakiwa safarini kupelekekwa Hong Kong.
Nasema ni kosa kubwa la CCM kwa sababu kama Kinana ni msemaji wa Chama na yeye tayari ana madoa,atawezaje kutetea sera ya maliasili inayohubiriwa na viongozi wake na makombora yanayorushwa na wapinzani wao likiwamo la JK kuhusika kwenye wizi wa pesa za EPA?
Badala ya yeye kuwa mtetezi wao inabidi mwenyewe aanze kwanza kujisafisha kuwa hahusiki na vitendo hivyo viovu kabla ya kukisemea chama.
Uraia wake bado ni kitendawili, watu wanasema ana asili ya Kisomali na tujuavyo wasomali wengi wanajihusisha na vitendo vya ujangili ukiwemo utekaji nyara wa meli za mizigo.
Kwa mwananchi wa kawaida ni vigumu sana kukubali au kutenganisha biashara yake ya meli na ujangili unaofanywa na watu wa jamii hiyo.
Nauliza hivi CCM walikosa mwanachama mtanzania halisi mwenye uraia usio na utata mwenye biashara isiyo na utata, kuwa msemaji wa chama wakaishia kutuletea Kinana anayeshirikiana na majangili kwa kuruhusu vyombo vyake kuihujumu nchi anayodai kuitetea?