Msaada wa jinsi ya kusamehe na kuachilia

Mimi roho ya kusamehe niliiacha mwaka 2012 (nilikua sijawah huru kiuchumi. Ivo ikawa inanilazimu kua Mpole)

Siku hizi roho yangu ni ya visasi tu .. Ukinifanyia ufedhuli, kama unahitaj nikulipue hapo hapo, nakulipua, kama unahitaj twende kichwa kichwa tunaenda

Kikubwa Nilichofanya, Ni kutokuchukulia kwa uzito , Yaan Unanifanyia ubaya. Nachukulia poa, lkn ukae ukitambua dawa yako ipo jikoni inakwiva na utainywa tu.

Haya maisha yamenipa Amani sana!


Kwa jambo kama lako, kwa sheria yangu, mimi sio mtu sahihi wa kukushauri hapa.
Noted The Jackal!
 
Hakuna kitu kibaya kama kuhifadhi chuki inauma sana na mbaya zaidi unaumia sana wewe kuliko aliekukosea

Mimi kuna namna mbili tu nazitumia kuzitoa chuki

1:- KUSAMEHE
Hapa ili nisamehe ni mpaka huyo alienikosea aje akili mbele yangu kuwa kakosea na aniombe msamaha ndipo nitasamehe, asipo omba msahaha siwezi kusamehe maana huenda hajui kama kanikosea
Sasa nitamsamehe vipi mtu ambaye yeye anadhani hajanikosea, na asipofanya kuomba msamaha itaniongezea chuki zaidi itanifanya niamni kuwa jamaa ana kiburi na hapo ndipo nitaitumia njia ya pili ambayo ni.......

2:-KULIPIZA KISASI
Ili niyatoe maumivu itabidi nilipize kisasi, hapa nitahisi kutulia maana maumivu yatakuwa yamehama kutoka kwangu na kuhamia kwa huyo alienikosea.

Kusema nijifanye nimesamehe bila kuombwa nisamehe nikujindanganya bure na siwezi, mbaya zaidi huyo alienikosea aendelee kuniudhi siwezi aiseeeeeeee
Uhalisia wa msamaha uanzia ndani ya moyo wako,uwezi kumsamehe mtu kwa kusema tuu "eti nimekusamehe! huo uongo ndio maana maumivu hayaishi ndani yetu kumuachilia mtu si jambo jepes kihivyo.unahitaji msaada wa Mungu ili aweze kukusaidia uweze kumsahau na kumwachilia yule aliyekutenda.
 
Kuna mbwa mmoja anaitwa Godfrey. Mbwa huyu nilimtoa jalalani na kanipigia MAGOTI mpaka nikaona ngoja nimsaidie. Alivyokuja Mara ya kwanza mabosi walimkataa lkn nilimpigia debe mpaka akaajiriwa. Lunch nikawa nampeleka za nguvu huyu mbwa kwa hela zangu. Bar na hotel asizojua tulienda nae ili apate uzoefu wa kuwa wa mujini. Eeeh bwanaeh.

Alipojua udhaifu wa big boss, alijipenyeza na majungu ya Khali ya juu mpaka kwa hiari yangu nikaacha kazi.

NEVER WAKE A SLEEPING DOG. IT WILL WAKE UP AND BITE YOU.

Na Ninyi wanawake msipende sana ku wa introduce marafiki zenu wa kike kwa boyfriend zenu au Waume zenu.
Wengi wamelia.

Pole sana mkuu bora ww huyo mbwa ni mtu baki, ngoja niishie hapa
 
Mimi kuna mtu aliwahi kuniumiza sana nikaamua kumpotezea ninaendelea na mishe zangu safi kabisa. Lakini kusema nae nimeshindwa kabisa maana tuko ofisi moja na sina kinyongo nae ila ndio hivyo kinywa kinakuwa kizito kabisa kusema nae.
Mimi ameniumizaga dada yangu ..nna 2yrs natafuta kisasi km naona vyote vyepesi ..yaan kabla corona haijapita na mimi lazima nimalizane naye kiroho safi kbs..ana kamwili kadogo kama jd bas nawazaga sijui nikambebe tu nilibwage road usk!
 
Mkuu kuna sehemu umeshindwa kujitafsiri na kujiwekea mipaka isivyokuwa na ulazima, unaupapasa uwezo wako na kujilinganisha sana na wengine (hili ni tatizo).

Kumbuka wewe ni wa pekee sana na hayupo kama wewe ila siyo lazima ujilinganishe na wengine ili kuuona upekee wako.

Tenga muda wa kutosha kwa ajili ya kujisikiliza wewe tu na siyo sauti za wengine. Kama unaweza kufanya meditation fanya.
 
Habari wana JF!

Mimi ni Muhanga wa hali hii nimevumilia sana lakini nimeshindwa. Juzi kuna jamaa yangu amekuja hapa kunihadithia kisa kilichomkuta maishani mwake ameshindwa kabisa kusamehe na kuachilia inagawaje anadai hana shida na watu waliomuumiza na kumpiga majungu.

Baada ya kunieleza kisa chenyewe akawa kama amenitonesha kidonda. Nakumbuka ilikuwa 2017 kazini (Naomba nisitaje kazi ninayofanya,ukiconnect dots naomba utulie tu). Ndipo nilipoona hamna maana ya kuwa na marafiki na kuwathamini sana na ndio kilichonifanya kutambua kuwa bado nina maumivu moyoni kama ya jamaa yangu huyu aliyenielezea kisa chake ambacho kwa leo nakiweka kipolo nieleze kisa changu kwanza.

Ilianza hivi,nilimpokea jamaa kazini akawa rafiki yangu wa karibu,alisema alishawahi kuwa mtumishi wa kada yetu huko sekta binafsi lakini akawa hakuna anachojua,nikawa msaada mkubwa kwake na tukaendelea na maisha vizuri tu,tukaendelea kupokea watumishi wengine tukawa tunaongezeka pale kazini pakachangamka sana.

Bahati mbaya Boss wetu akapata matatizo akawa kashushwa cheo,Jamaa yangu akapata kile cheo,alipopewa barua breki ya kwanza akaja kwangu akanionesha barua akaniomba nimsaidie niwe msaidizi wake namba mbili huku akirejea jinsi ambavyo tuliishi vema na msaada niliompa wakati wote. Nikakubali nikamwambia tupige kazi.

Akaja jamaa mwingine mtu mzima kama yeye! akaripoti pale kazini,kwa jinsi alivyoonekana alionekana ni Mtaratibu na mshika dini sana,basi jamaa akamchagua kuwa msaidizi chini yangu,hivyo tukawa watu watatu ndio tuna sauti pale kazini.

Sasa watumishi wenzetu wakawa wanamsema sana Boss! kuwa hajali watu anajiamuria mambo bila kushirikisha wengine,na wakati wanamsema hivyo wanasubiri mimi nikiwa nao ndio wanayasema hayo,na wengine wana sisitiza we si ndio msaidizi wake mwambie jamaa yako mambo huwa hayaendi ivo.

Basi nikajiridhisha kuwa kuna hoja ni za msingi na hoja zingine ni majungu tu! Nikamfuata ofisini nikamwambia tuongee kidogo,nikampasha nini kinaendelea pale kazini na nikamshauri kuwa mengine ni majungu lakini mengine ajaribu kuyatolea ufafanuzi wa kina kwa watumishi wenzetu ili kuondoa tashwishi na ili mambo yaendelee vizuri.

Basi jamaa akawa kama amenielewa akaniagiza niandike memo ya kuwataarifu kuwa siku flani kutakuwa na kikao,nikafanya hivyo kama alivyoagiza.

Hali ikanibadilika ghafla jamaa akaanza kunipiga vijembe, mara watumishi wengine wanalalamika kuwa ananipendelea sana mimi, mala mimi ni mzembe, mambo yakawa mengi sana.

Sikujua nifanye nini? Baada ya muda watumishi wengine wakaanza kunipa ubuyu,(Wanawake Mbarikiwe sana) Huyu Mdada tunafanya nae kazi akanieleza siku ambazo haujaja kazini jamaa yako anakusema vibaya sana,anadai humsaidii mara umebadirika sana hukuwa hivyo mwanzo,hasa baada ya kufunga ndoa umekuwa wa tofauti sana,Labda Ndoa inakusumbua?

Sikujali nikapuuza! Sasa pale ofisini jamaa sio mtaalam sana wa mambo ya mifumo ya Serikali, mimi ndie nilikuwa kilaka pale,akawa ananiagiza kufanya mambo bila malipo,nikaendelea kufanya bila shida.

Nikaja kupata taarifa kuwa yule jamaa aliyeteuliwa kuwa msaidizi wako na Boss ndie anayekufitini sana! Nikajiuliza sana,inamaana Boss hanifahamu kabisa mpaka anaamini kila anachoambiwa na Jamaa naomba hapa nimpe jina la Shemasi huyu Mfitini wangu.

Basi Shemasi akawa ndie mwandani wa Boss, sikujali sana, sasa wakaanza kuwa wana ni SIDELINE,yaani Kama wananiepuka vile,Ikawa Boss akiondoka kikazi ananiachia majukumu lakini kumbe shemasi kaagizwa anifautilie kwa ukaribu.

Hilo sikulipenda ila nikajikaza,lakini pia nikashidwa,ikabidi nimshirikishe Mke wangu!Mke wangu akaniambia fitina ni kawaida komaa nao! Usiache hiyo nafasi endelea kumsaidia jamaa ako.

Mimi Ni Mkristo nikaanza kusali na kuomba maarifa nifanyeje sasa! Ikafika kipindi hasira ikapanda sana nikasema sasa! Ngoja nikamripue huyu asinifanye mimi zuzu kwa kuwa najua anachonifanyia ila nimeamua kunyamaza tu! Nilipanga nikaseme ukweli wote na yanayoendelea kuwa najua asinifanye mie Mjinga,lakini Kabla sijafanya hiyvo nikaingia kwenye Maombi - Baada ya Kuomba nikasikia msukumo wa ajabu - Kuwa Nisiseme chochote nitulie tu! Basi nikaisikiliza ule msukumo nikatulia.

Mambo yakaendelea vile vile hakuna mabadiliko! Jamaa chuki ikazidi sana juu yangu,nikasikia anadai kuna mtumishi mwenzetu huko Chuo Kikuu akija tu! basi atanitoa na atampatia huyo Jamaa Nafasi yangu.

Kwa kweli nilipigwa majungu sana ambayo mengine siwezi eleza hapa ili kuendelea kuficha jina na Taasisi ninayofanyia Kazi.

Nikaona isiwe tabu sana! Nikamfuata Ofisini kwake kwa Upole sana! Nikamwambia Boss mi naomba nimpumzike sasa! Kama ni uzoefu wapo wengi wanaoweza kukusaidia! Mimi naomba nipumzike kwa Sababu kuna Mambo ambayo nataka kufanya yanaweza kuathiri utendaji wangu.

Hakuafiki! akaniambia unaweza kuendelea tu kunisaidia na ukaendelea na mambo yako pia! Nikakataa nikamwambia hapana kabisa.

Basi baada ya Muda Shemasi akapandishwa cheo akahama pale,na muda huo huo yule jamaa akarudi toka masomoni,Akamshawishi jamaa kuwa msaidizi wake, jamaa nae akakataa kabisa akidai wapo wakongwe na watu wenye Uzoefu mzuri kuliko yeye! inakuwaje ametoka masomoni tu afikie kushika nafasi.

Basi akaniiita akanieleza kuwa jamaa amekataa akawa amenishilikisha kuwa kati ya Hawa (Akawataja Majina) na nani anafaa? sikuweka neno la ziada zaidi ya kusema wote wanafaa,basi akachagua mmoja wa wale alionitajia majina nikamuunga mkono kuwa huyo aliyechangua ni mtendaji mzuri anafaa.

Muda si Mrefu Nikawa nimepata Nafasi ya kusimamia zoezi flani hivi lina pesa kiasi! Nikawa Boss kwa muda sikuwa na roho ya Kinyongo - Ingawaje nilipomshirikisha Wife alinishauri nisimchague kwenye hilo zoezi kabisa,lakini sikufanya hivyo nikamteua na kuteua na watu wake wa Karibu bila Kinyongo tukamaliza ile kazi,kila mtu akapata cha kwake,ingawaje yeye aliacha kabisa kunipa deal za pesa,akawa anawapa wale wanaomfurahisha tu.

Sasa Jamaa baada ya Kuja kunisimulia jinsi alivyo nyanyaswa na Mkubwa wake kazini, nimegundua kwamba nilishamsamehe jamaa lakini bado nina maumivu na mbaya zaidi nimegundulika kuwa na Matatizo ya kiafya ambayo sikuwahi kuwa nayo huko nyuma na ni imani yangu ya kuwa kwa namna moja ama nyingine huyu jamaa alivyonitendea ndio chanzo cha hypertension yangu.

Naomba msaada ndugu zangu! Sihitaji kulipa kisasi,nahitaji maisha yangu yaendelee! nawezaje kuachilia nahisi kama bado ipo hali ya kuumia kila wakati ninapokumbuka yaliyonisibu.

Asanteni.
Pamoja na maelezo yako marefu, mimi nimegundua kuwa hujui kutofautisha kati ya neno "kusamehe" , "kinyongo" na "kupuuza" na binafsi naomba nikujuze maana ya maneno hayo mawili kwa jinsi ninavyoyafahamu kimwili na kiroho:-

Kusamehe ni hali ya kuachilia jambo fulani lenye kuumiza au kukwaza pale unapokuwa umekosewa na mtu kisha mtu huyo akatambua kosa lake na akaja kukuomba msamaha, hivyo ukaamua kumsamehe au kutomsamehe (maana kusamehe siyo lazima). Sasa unapoamua kumsamehe mtu aliyekukosea/kukukwaza hakikisha msamaha huo umetoka ndani ya roho yako (usisamehe kwa mashinikizo ya viongozi wa dini au mtu yeyote yule, itakugharimu kiroho). Ukisamehe kutoka rohoni, haitakuumiza.

Kinyongo Ni hali ya kulimbikiza chuki moyoni kwa mtu aliyekukosea au kukukwaza na ukashindwa kumwambia pengine kwa kuwa ni mkubwa kwako au unamuogopa, hali hii hupelekea kujihaidi kulipa kisasi bila kujali kama unauwezo wa kulipa kisasi hicho au la, hali hii hupelekea kuhatarisha afya ya mwenye kinyongo jambo ambalo siyo zuri hasa pale kisasi kinaposhindikana.

Kupuuza ni hali ya kuachilia jambo fulani lenye kukuumiza au kukukwaza pale unapokuwa umekosewa na mtu kisha ukagundua mtu huyo hajielewe wala kujitambua kama amekukwaza, au jambo lenyewe siyo la kukupotezea muda wako maana pengine ni dogo hivyo unaamua kuliacha lakini kwa tahadhari ya kumuepuka mtu huyo bila kumsahau na kutomuhusisha tena kwenye mambo yako muhimu (hasa kama alikuwa mtu wa karibu kwa namna yoyote)

Hivyo basi kwa usalama wa afya ya mwili na roho yako, ikiwa mtu amekukosea na akakuomba msamaha siyo vibaya ukimsamehe . Ila kabla ya kumsamehe chambua faida na hasara za kutoa msamaha na hakikisha mkosaji ameonyesha kujutia kosa lake na ameomba huo msamaha (Usisamehe eti kwa kuwa YESU alisamehe maana YESU ni YESU na WEWE ni WEWE, kila mmoja ana changamoto zake na kwa wakati wake na makosa hayafanani).

Ukiona huwezi kusamehe mchukulie hatua za kisheria utakazoona zinafaa kwa muda huo, kamwe epuka kusamehe kwa kufurahisha watu maana tunatakiwa kuwapenda wenzetu kama tunavyopenda nafsi zetu (inaanza na kujipenda sisi) na umwambie kwa uwazi kamwe usimfiche kama ni deni alipe na kama ni kosa kazini awajibishwe kwa faida yako na ya umma.

MWSHO JAPO SI KWA UMUHIMU. UKISAMEHE KUTOKA ROHONI HUTOJUTIA KAMWE MAANA YATAPITA NA UTASAHAU LAKINI UKISAMEHE KIMWILI ITAKUUMIZA MAANA ITABAKI ROHONI DAIMA.
 
Mimi ameniumizaga dada yangu ..nna 2yrs natafuta kisasi km naona vyote vyepesi ..yaan kabla corona haijapita na mimi lazima nimalizane naye kiroho safi kbs..ana kamwili kadogo kama jd bas nawazaga sijui nikambebe tu nilibwage road usk!
Just forget her, time will heal you.

Ndugu yangu aliniumiza sana 2018 nikajisemea sitakaa niongee nae. Lkn after three years japo siongei nae kihivyo lkn bifu limeisha.
 
Just forget her, time will heal you...
Ndugu yangu aliniumiza sana 2018 nikajisemea sitakaa niongee nae. Lkn after three years japo siongei nae kihivyo lkn bifu limeisha.
Nashindwa


Unamsaidia mtu had kulipa fees lakini kumbe anataka kukuharibia biashara zako..ili iwaje..naona wazazi wake wamemshindwa mm ntamalizana naye..mm pia siongei naye 2yrs nw .anahaha tu kujua leo niko wapi...wanaye watanisamehe...na wananipenda ajabu
 
Mimi ameniumizaga dada yangu ..nna 2yrs natafuta kisasi km naona vyote vyepesi ..yaan kabla corona haijapita na mimi lazima nimalizane naye kiroho safi kbs..ana kamwili kadogo kama jd bas nawazaga sijui nikambebe tu nilibwage road usk!
Hahaha dah haya maisha yana mambo! Msamehe tu uendelee na maisha bila kinyongo ila ikishindikana kusamehe basi mlipue tu hakuna jinsi.
 
Pamoja na maelezo yako marefu, mimi nimegundua kuwa hujui kutofautisha kati ya neno "kusamehe" , "kinyongo" na "kupuuza" na binafsi naomba nikujuze maana ya maneno hayo mawili kwa jinsi ninavyoyafahamu kimwili na kiroho:-

Kusamehe ni hali ya kuachilia jambo fulani lenye kuumiza au kukwaza pale unapokuwa umekosewa na mtu kisha mtu huyo akatambua kosa lake na akaja kukuomba msamaha, hivyo ukaamua kumsamehe au kutomsamehe (maana kusamehe siyo lazima). Sasa unapoamua kumsamehe mtu aliyekukosea/kukukwaza hakikisha msamaha huo umetoka ndani ya roho yako (usisamehe kwa mashinikizo ya viongozi wa dini au mtu yeyote yule, itakugharimu kiroho). Ukisamehe kutoka rohoni, haitakuumiza.

Kinyongo Ni hali ya kulimbikiza chuki moyoni kwa mtu aliyekukosea au kukukwaza na ukashindwa kumwambia pengine kwa kuwa ni mkubwa kwako au unamuogopa, hali hii hupelekea kujihaidi kulipa kisasi bila kujali kama unauwezo wa kulipa kisasi hicho au la, hali hii hupelekea kuhatarisha afya ya mwenye kinyongo jambo ambalo siyo zuri hasa pale kisasi kinaposhindikana.

Kupuuza ni hali ya kuachilia jambo fulani lenye kukuumiza au kukukwaza pale unapokuwa umekosewa na mtu kisha ukagundua mtu huyo hajielewe wala kujitambua kama amekukwaza, au jambo lenyewe siyo la kukupotezea muda wako maana pengine ni dogo hivyo unaamua kuliacha lakini kwa tahadhari ya kumuepuka mtu huyo bila kumsahau na kutomuhusisha tena kwenye mambo yako muhimu (hasa kama alikuwa mtu wa karibu kwa namna yoyote)

Hivyo basi kwa usalama wa afya ya mwili na roho yako, ikiwa mtu amekukosea na akakuomba msamaha siyo vibaya ukimsamehe . Ila kabla ya kumsamehe chambua faida na hasara za kutoa msamaha na hakikisha mkosaji ameonyesha kujutia kosa lake na ameomba huo msamaha (Usisamehe eti kwa kuwa YESU alisamehe maana YESU ni YESU na WEWE ni WEWE, kila mmoja ana changamoto zake na kwa wakati wake na makosa hayafanani).

Ukiona huwezi kusamehe mchukulie hatua za kisheria utakazoona zinafaa kwa muda huo, kamwe epuka kusamehe kwa kufurahisha watu maana tunatakiwa kuwapenda wenzetu kama tunavyopenda nafsi zetu (inaanza na kujipenda sisi) na umwambie kwa uwazi kamwe usimfiche kama ni deni alipe na kama ni kosa kazini awajibishwe kwa faida yako na ya umma.

MWSHO JAPO SI KWA UMUHIMU. UKISAMEHE KUTOKA ROHONI HUTOJUTIA KAMWE MAANA YATAPITA NA UTASAHAU LAKINI UKISAMEHE KIMWILI ITAKUUMIZA MAANA ITABAKI ROHONI DAIMA.
Namshukuru sana aliyenifundisha KUPUUZA japo nae aliingia kwenye mnyoyoro wa wakoseaji😂😂😂 nikampuuza nae maisha yangu yamekuwa mepesi sana tangu niijue siri ya kupuuza, inaendana sana na ubinafsi Yani sijali kabisa siku hizi na inawezekana wapo niliowaumiza kwa haka katabia ka kupuuza🤣🤣🤣 ila ndo siwazi kabisa Ni km mtu nimetangaziwa kifo chake ndivyo nafuta mtu kichwani kwangu
Pamoja na maelezo yako marefu, mimi nimegundua kuwa hujui kutofautisha kati ya neno "kusamehe" , "kinyongo" na "kupuuza" na binafsi naomba nikujuze maana ya maneno hayo mawili kwa jinsi ninavyoyafahamu kimwili na kiroho:-

Kusamehe ni hali ya kuachilia jambo fulani lenye kuumiza au kukwaza pale unapokuwa umekosewa na mtu kisha mtu huyo akatambua kosa lake na akaja kukuomba msamaha, hivyo ukaamua kumsamehe au kutomsamehe (maana kusamehe siyo lazima). Sasa unapoamua kumsamehe mtu aliyekukosea/kukukwaza hakikisha msamaha huo umetoka ndani ya roho yako (usisamehe kwa mashinikizo ya viongozi wa dini au mtu yeyote yule, itakugharimu kiroho). Ukisamehe kutoka rohoni, haitakuumiza.

Kinyongo Ni hali ya kulimbikiza chuki moyoni kwa mtu aliyekukosea au kukukwaza na ukashindwa kumwambia pengine kwa kuwa ni mkubwa kwako au unamuogopa, hali hii hupelekea kujihaidi kulipa kisasi bila kujali kama unauwezo wa kulipa kisasi hicho au la, hali hii hupelekea kuhatarisha afya ya mwenye kinyongo jambo ambalo siyo zuri hasa pale kisasi kinaposhindikana.

Kupuuza ni hali ya kuachilia jambo fulani lenye kukuumiza au kukukwaza pale unapokuwa umekosewa na mtu kisha ukagundua mtu huyo hajielewe wala kujitambua kama amekukwaza, au jambo lenyewe siyo la kukupotezea muda wako maana pengine ni dogo hivyo unaamua kuliacha lakini kwa tahadhari ya kumuepuka mtu huyo bila kumsahau na kutomuhusisha tena kwenye mambo yako muhimu (hasa kama alikuwa mtu wa karibu kwa namna yoyote)

Hivyo basi kwa usalama wa afya ya mwili na roho yako, ikiwa mtu amekukosea na akakuomba msamaha siyo vibaya ukimsamehe . Ila kabla ya kumsamehe chambua faida na hasara za kutoa msamaha na hakikisha mkosaji ameonyesha kujutia kosa lake na ameomba huo msamaha (Usisamehe eti kwa kuwa YESU alisamehe maana YESU ni YESU na WEWE ni WEWE, kila mmoja ana changamoto zake na kwa wakati wake na makosa hayafanani).

Ukiona huwezi kusamehe mchukulie hatua za kisheria utakazoona zinafaa kwa muda huo, kamwe epuka kusamehe kwa kufurahisha watu maana tunatakiwa kuwapenda wenzetu kama tunavyopenda nafsi zetu (inaanza na kujipenda sisi) na umwambie kwa uwazi kamwe usimfiche kama ni deni alipe na kama ni kosa kazini awajibishwe kwa faida yako na ya umma.

MWSHO JAPO SI KWA UMUHIMU. UKISAMEHE KUTOKA ROHONI HUTOJUTIA KAMWE MAANA YATAPITA NA UTASAHAU LAKINI UKISAMEHE KIMWILI ITAKUUMIZA MAANA ITABAKI ROHONI DAIMA.
 
Vitu vya kawaida SANA! Unapataje hypertension?

Unatakiwa kuiacha ofisi ofisini, ukitoka mlangoni. Wewe unaibeba ofisi mpaka huku duniani??
Una kinyongo kibaya sana, usipoangalia diabetes inakuja pia.

Jichanganye na mambo mengine ya kijamii, tafuta marafiki nje ya ofisi, ofisi iwe ofisi tu, mkimaliza kunywa chai bye bye.

Utakufa mdogo, wenzako wanakula life!

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Nashindwa


Unamsaidia mtu had kulipa fees lakini kumbe anataka kukuharibia biashara zako..ili iwaje..naona wazazi wake wamemshindwa mm ntamalizana naye..mm pia siongei naye 2yrs nw .anahaha tu kujua leo niko wapi...wanaye watanisamehe...na wananipenda ajabu
Kama umeshindwa kumsamehe na muhusika haonekani kujutia kosa lake unatakiwa umchukulie hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kumueleza jinsi ulivyochukia/kuathirika na vitendo vyake viovu kwako (hii itasaidia kukuletea afueni ndani ya roho yako)
 
Back
Top Bottom