Msaada: Tumetapeliwa!

Msaada: Tumetapeliwa!

hawa freelancer wapo wengi ambao ni wezi na wengine huwa anaiswap line yako wewe ukija kustuka simu haiingii yameshapita hata masaa wife na shemeji yangu dadaye wifu wamewahi kulizw kwa njia hizi japo wao hazikuwa pesa nyingi sana katika account zao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfano, mimi nishawahi kufanya kazi ya kusajili lain. Kwenye kumuunganisha mteja na either huduma ya M-pesa, Airtel Money etc lazima mteja akupatie simu yake. Unapofikia kipengele cha kuweka password unatakiwa umpe mteja aweke mwenyewe, sasa wateja wengi, hasa kina mama (wanawake) atakwambia weka tuu, anakutajia na anakwambia yeye kwa lain zote nywila ni hiyo hiyo(habadilishi). Sasa kama freelancer ni mwizi, ataingia kwenye menyu nyinginezo kama za benk n.k na kuhamisha pesa fasta

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Apo mkuu kuna menu ukibonyeza inatokea maneno ambaye yanamtaka mhusika aweke namba ya siri then jamaa anamwambia aweke namba ya siri yeye bila kijua baada ya apo inaleta sms ile sms inapokuja inakuwa ina namba ya siri kwahiyo wakala anafungua ile sms anasoma fast then anafuta ....pole sana mkuu tuwe makin

Sent using Jamii Forums mobile app
Una make sense sana mkuu. Asante sana, umakini ndo jambo la msingi. Japo bado naumiza kichwa inakuwaje mtu anaweza kutoa pesa kwenye akaunti yako bila kuleta notification, na baadae kublock kila kitu. How is that possible kwenye Banking System?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu dunia kubwa hii acha ubishi asee .
Mimi story ya huyo jamaa haijanistua kwa mana Nina Uncle wangu nae kapigwa 2.5M mwaka huu mwezi January kwa style hyo hiyo.
Hata uyo uncle wako ni walewale...aina iyo ya uhuni naifahamu na tushawahi mkamata mmoja akiwa katika jaribio la kutaka kumuibia bi mkubwa wake na rafiki angu,wanachofanya wakati anakusajilia iyo laini mpya ya chuo anakuuliza technical questions ili kukuingiza kingi na wewe ukiwa mzembe unaingia kweli...mfano atakwambia anataka kukusajilia na m pesa so kwenye kukusajilia m pesa atakuuliza password na mara nyingi password zinakuwa zinafanana na bank,so ukimpa tu m pesa password imekula kwako..wengine atakudanganya kuwa hii line mpya tunataka tukusajilie na sim banking,hapo ndo mtu unalizwa
 
Wee jamaa siye kweli, watu wanaongelea technology we unaongelea ramli kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app

Aaaah ..! Endelea kudharau mambo yaliyo halisi..! Sasa Technology unayoiongelea itarudisha muamala ambao tayari ameshautoa ??
Mnayoongelea nyinyi ni technology ya Mzungu, tunatumia pia technology ya Mwa-Afrika...!
 
Shida wanaosajili hao wanaotembea, wanakusajilia wakimaliza kila kitu wanakuambia kunasehemu kakosea anaanza upya kukusajili, kwahiyo anasajili mbili laini nyingine inauzwa kwa hela nyingi tu kwa matapeli, halafu laini zilizofungwa kuna mtu alikamatwa kazi yake kuzifungua kwa hiyo bado kuna kazi

eheeeee?
 
Kwa nchi za Mabeberu mtu kama huyu anatafutwa na kupewa ajira kitengo maalum kwa dau kubwa ili kulinda system za mitandao ya bank, Simu, Serikali n.k
 
You've got a good sense. Nami nimefikiria hivyohivyo. Time will tell

Sent using Jamii Forums mobile app
hahaaah hamna cha it wala nini,wanawapigaga kizembe,wanakwambia sasa hi line mpya tunataka tukusajilie na m pesa..ukikubali kuna sehemu ya kuingiza password anakupa simu uingize mwenyewe...wakati unaingiza anaicheki na kui mark..kinachofuata hapo ni kilio,or tena kwa wanawake hao walivyo wavivu wakati mwingine anadai ngoja nikutajie tu...anapigwa mtu hapo,wakikuona mzembe zaidi wanakwambia sasa hii line mpya tukusajilie na sim banking kabisa,ukikubali ushaibiwa hapo coz utachezeshewa ujanja tu hapo kuja kushtuka hela zishachukuliwa..matapeli wana mbinu nyingi hakuna cha IT wala nn
 
Back
Top Bottom