Msaada tafadhali: Nimechaguliwa katika US Green Card

Msaada tafadhali: Nimechaguliwa katika US Green Card

Wakuu unaposhiriki dv lottery visa ni lazima uwe na paspoti mkononi?
 
Naona wametangaza mchakato wa kuomba tena mwaka huu unaanza October
 
Dirisha linafunguliwa mwezi gani wakuu!!!na je unavyojiregistar kuna pesa unatakiwa ulipie au ni bure tu?
 
Fake hiyo.
Achana NAyo.
Dv lottery ni Bure na inaanza oktoba 3
Naomba nisaidieni mimi najalibu kujiunga naulizwa jina, emailna education level nikisubmit wananiambia narusiwa kucheza sasa section no 2 naambiwa nilipie sasa hapa nashindwa ntalipiaje na ntajuaje ni sh ngapi nalipia natak kulipiwa kwa western union je ntajuaje account yao nisaidieni wakuu.
 
Habari ya jumapili Ndugu zangu, niende kwenye mada moja kwa moja. Mwaka Jana mwezi wa kumi na moja nilicheza US green card lottery na mwezi huu wa tano nimefanikiwa kupita katika mchujo wa kwanza unaofanywa na Kentucky Consular Center (KCC) niliingiza confirmation number katika website ya dvlottery.state.gov nikakuta barua kuwa nimefanikiwa kuchaguliwa, lakini ile barua inasema kwamba kuchaguliwa katika mchujo huu haimaanishi kuwa tayari nimepata visa hapana bado kuna hatua nyingine za kufuata ili kuwezesha kupata visa. Pia ile barua inasema kuwa kuna form inaitwa DS-260 Immigrant visa and Alien Registration Application, kwahiyo mpaka sasahivi bado sijaelewa hiyo form ninaipata wapi na baada ya hapo nini kitafuata?, je, ni vitu gani vya kuzingatia ili niweze kushinda na kupata visa. Msaada wenu ndugu zangu ni wa muhimu sana.
Cc: BAK, Nyani ngabu, Mzizi mkavu, ogah, masanja na wengine ambao wanafahamu mambo haya naombeni mniambie. Mbarikiwe sana.
mkuu kuishi marekani na kuacha mapori mabichi ya kulima ni utumwa wa fikra wa hali ya juu kabisa wa kuitwa sir.
 
Sie tunaofanyia ubalozi tulitaka kukujibu,but coz kuna majina umeyapa kipaumbele ngoja waje kukujibu hayo maswali yako...
Mkuu ndio umeghairi[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
mkuu kuishi marekani na kuacha mapori mabichi ya kulima ni utumwa wa fikra wa hali ya juu kabisa wa kuitwa sir.
Mkuu usemacho ni kweli kabisa ila tambua kuwa tunatofautiana mitizamo na kila mmoja ana haki ya kufanya kile anachoona kwake ni sahihi ndio maana nikachagua njia hiyo.
 
Unatakiwa kuwa na soft copy passport size 1 kwaajili ya kuattach wakati wa kujisajili, cha msingi wakati unajaza detail zako hakikisha unajaza taarifa zilizo sahihi.
Nimekuelewa sana mkuu
 
Wadau nisaidieni kitu. Nami niliomba hii kitu lkn majibu hayakuwa poa. Sasa kuna vitu kama vitatu navihisi kuwa vilisababisha mimi kukosa. Kwanza ni kwamba sikuweka details za mwenza (ki ukweli sina mwenza); pili sikuangalia majibu on time so nahisi hata kama ningepata ningekuwa nimecherewa; tatu ni kuhusu kwamba ni bahati nasibu kwa hyo sikubahatika tu. Je mnasemaje kuhusu hizo hisia zangu? Hasa hiyo ya kwanza na ya pili. Nataka next time nisifanye makosa.
Hapo kwenye mwenza hata mimi wananichanganya mkuu, ni kama wanalazimisha uwe nae, ukiwa single na huna watoto nafikiri inakuwa mtihani jinsi ya kuomba
 
Katika hayo yote uliotaja jibu ni moja tu ni kwamba hukubahatika kuchaguliwa, cha msingi kama ulipata confirmation no wakati ulipoomba ktk maombi ya mwanzo basi tayari ulikuwa na vigezo vya kuchaguliwa, lakini kwakuwa hii ni kama mchezo Wa bahati nasibu basi hukushinda bahati hiyo, Jaribu tena mwaka huu nazani kuanzia mwezi October.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona ni kama wanalazimisha uwe na mchumba au mimi ndo sijaelewa?
 
Mbona ni kama wanalazimisha uwe na mchumba au mimi ndo sijaelewa?
Utakuwa hujaelewa mkuu, swala la mwenza wanasisitiza uweke details zake ili ikitokea umeshinda uambatane nae coz ukiandika upo single itakuwa ngumu yeye kuku join au itachukua muda mrefu kujoin, hivyo basi wanafanya hivyo coz hawataki kuvunja ndoa za watu.
 
Utakuwa hujaelewa mkuu, swala la mwenza wanasisitiza uweke details zake ili ikitokea umeshinda uambatane nae coz ukiandika upo single itakuwa ngumu yeye kuku join au itachukua muda mrefu kujoin, hivyo basi wanafanya hivyo coz hawataki kuvunja ndoa za watu.
pia ni moja ya sheria kwamba, kama ni mwana ndoa alafu ulipocheza hauku sema kama umeoa au kuwa na watoto siku ya kwenda kwa ubalozi hautopata visa utakuwa disqualified coz hukuwa mkweli, na hautopata visa.
 
Je kuna gharama zozote kushiriki bahat nasibu hii ndg zang
Hakuna garama yoyote ili mr adi uwe na kigezo chochote kati ya viwili wqlovoviweka. 1. uwe umesoma angalau hadi high school, 2. expérience ya kazi ya miaka 2 walizoziorodhesha kweny instructions zao.
 
Wakuu unaposhiriki dv lottery visa ni lazima uwe na paspoti mkononi?
kama unamaanisha passport ya kusafiria, sio lazima uwe nayo mkononi ila ukishashinda ndiyo utaanza mchakato wa kutafuta hiyo passport kwa ajili ya safari coz itahitajika ubalozini.ili mr adi majina yako yawe sana na cheti cha kuzaliwa unayo jiregister siku ya kucheza.
 
Back
Top Bottom