Msaada tafadhali: Nimechaguliwa katika US Green Card

Msaada tafadhali: Nimechaguliwa katika US Green Card

Pale US anapofanikiwa kuifanya nchi yake kuwa pepo ya dunia....., ckupingi bro nawaza tu...
 
Huko zamani wazungu na waarabu walikua wanakuja kutafuta watu(watumwa) huku kwenye bara letu kwa mitutu, lakini sasa hivi nastaajabishwa kuona watu wenyewe kwa jitihada zao wanagharamia kuwa watumwa. TULIA CHINI MWAKO UJENGE NCHI YAKO USIKIMBILIE KWENDA KUKATA VITUNGUU
 
Kweli mkuu. Hata mie nilitaka nimpe ushauri unaofaa nikasita kidogo baada ya kuona ameshajichauglia watu wa kumjibu... Ngoja hao watu wake waje hapa kumfaa...
Ungepita bila kuchangia kama hakukutaja. Huezi jua kawataja hao labda kagundua wana uelewa katika ishu za Green Card
 
Sie tunaofanyia ubalozi tulitaka kukujibu,but coz kuna majina umeyapa kipaumbele ngoja waje kukujibu hayo maswali yako...
Acha zako. Umeulizwa kama unafanya kazi ubalozini? Au kiherehere tu? Kama huhitaji kusaidia kisa hujatajwa si upite kushoto tu
 
Pale US anapofanikiwa kuifanya nchi yake kuwa pepo ya dunia....., ckupingi bro nawaza tu...
Najaribu kuwaza Tanzania tungekuwa na ishu ya namna hii hivi watu wangekuwa wangapi mkuu?
 
Ebhan hii kitu lini tena..wengine tupo bongo bahati mbaya!!
 
"Dunia iweke tuzo za wachukiaji ..Bongo kuna watu wana vipaji"
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Wadau nisaidieni kitu. Nami niliomba hii kitu lkn majibu hayakuwa poa. Sasa kuna vitu kama vitatu navihisi kuwa vilisababisha mimi kukosa. Kwanza ni kwamba sikuweka details za mwenza (ki ukweli sina mwenza); pili sikuangalia majibu on time so nahisi hata kama ningepata ningekuwa nimecherewa; tatu ni kuhusu kwamba ni bahati nasibu kwa hyo sikubahatika tu. Je mnasemaje kuhusu hizo hisia zangu? Hasa hiyo ya kwanza na ya pili. Nataka next time nisifanye makosa.
 
Wadau nisaidieni kitu. Nami niliomba hii kitu lkn majibu hayakuwa poa. Sasa kuna vitu kama vitatu navihisi kuwa vilisababisha mimi kukosa. Kwanza ni kwamba sikuweka details za mwenza (ki ukweli sina mwenza); pili sikuangalia majibu on time so nahisi hata kama ningepata ningekuwa nimecherewa; tatu ni kuhusu kwamba ni bahati nasibu kwa hyo sikubahatika tu. Je mnasemaje kuhusu hizo hisia zangu? Hasa hiyo ya kwanza na ya pili. Nataka next time nisifanye makosa.
Katika hayo yote uliotaja jibu ni moja tu ni kwamba hukubahatika kuchaguliwa, cha msingi kama ulipata confirmation no wakati ulipoomba ktk maombi ya mwanzo basi tayari ulikuwa na vigezo vya kuchaguliwa, lakini kwakuwa hii ni kama mchezo Wa bahati nasibu basi hukushinda bahati hiyo, Jaribu tena mwaka huu nazani kuanzia mwezi October.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika hayo yote uliotaja jibu ni moja tu ni kwamba hukubahatika kuchaguliwa, cha msingi kama ulipata confirmation no wakati ulipoomba ktk maombi ya mwanzo basi tayari ulikuwa na vigezo vya kuchaguliwa, lakini kwakuwa hii ni kama mchezo Wa bahati nasibu basi hukushinda bahati hiyo, Jaribu tena mwaka huu nazani kuanzia mwezi October.

Sent using Jamii Forums mobile app
Poa thanks
 
Habari ya jumapili Ndugu zangu, niende kwenye mada moja kwa moja. Mwaka Jana mwezi wa kumi na moja nilicheza US green card lottery na mwezi huu wa tano nimefanikiwa kupita katika mchujo wa kwanza unaofanywa na Kentucky Consular Center (KCC) niliingiza confirmation number katika website ya dvlottery.state.gov nikakuta barua kuwa nimefanikiwa kuchaguliwa, lakini ile barua inasema kwamba kuchaguliwa katika mchujo huu haimaanishi kuwa tayari nimepata visa hapana bado kuna hatua nyingine za kufuata ili kuwezesha kupata visa. Pia ile barua inasema kuwa kuna form inaitwa DS-260 Immigrant visa and Alien Registration Application, kwahiyo mpaka sasahivi bado sijaelewa hiyo form ninaipata wapi na baada ya hapo nini kitafuata?, je, ni vitu gani vya kuzingatia ili niweze kushinda na kupata visa. Msaada wenu ndugu zangu ni wa muhimu sana.
Cc: BAK, Nyani ngabu, Mzizi mkavu, ogah, masanja na wengine ambao wanafahamu mambo haya naombeni mniambie. Mbarikiwe sana.
Hongera sana Dibaji..
 
Hongera sana Dibaji..
Kwa wale wanaotaka kushiriki mwaka huu vigezo ni kati ya hivi viwili...
1. Uwe umesoma hadi high school na
2. Angalau uwe una expérience ya miaka 2 ya kufanya kazi au zaidi tangu siku unafanya entre ya application..

Angalizo hii kitu jamani ni ya ukweli Watanzania tushiriki hii lottery, dunia nzima wanashiriki 2018dv lottery jumla ya washiriki walicheza individuals milioni 23 naushee bt waliochaguliwa ni jumla ya watu 110,000 pamoja na wanafamilia lakini wanaotakiwa kwenda ni watu 50,000 tu tanzania jumla ya washindi ni 173. Tuwaombee Mungu waweze kupata..
 
Ndugu nielekeze unaingiaje kucheza nami nijalibu bahati yangu

IRON LADY!!!!
 
Back
Top Bottom