- Thread starter
- #41
BAK nashukuru sana kaka kwa ushauri wako, nitaufanyia kazi.Hongera sana Mkuu kwa kupita katika hii hatua ya awali. Mimi pamoja na kuwafahamu baadhi ya Watanzania lakini taratibu za kufuata baada ya kupita hii hatua ya mwanzo sizifahamu.
Ushauri wangu kwako nenda ubalozini ukaulize maswali mengine muhimu ili uweze kukamilisha taratibu zote husika.
Hakikisha unakuwa na umakini wa hali ya juu katika kukamilisha taratibu zote husika vinginevyo kosa moja tu unaweza kuiona bahati yako ya mtende inayeyuka.
Kila la heri na baraka katika kukamilisha taratibu zote husika.
NB: Ukienda ubalozini uwe makini pia unaweza kukutana na mbongo mwenzetu baadhi wana roho mbaya na hivyo kutokuwa na msaada wa kutosha au kukupa msaada nusu nusu.