Msaada-paypal

donlucchese

JF-Expert Member
Mar 23, 2011
17,043
21,517
Nimefanikiwa kulink credt card yang na paypal. Sasa swali linakuja,pale kwenye shipping adress ivi unaweka adress yako ya posta au? Maana kwa wenzetu hususan marekani hua kuna street adress kabisa sasa mimi nakaa Goba kwa Ndambi ntafanyaje? Asanten wakuu
 
Shipping Address unatakiwa uweke address ambayo mzigo au barua inaweza kukufikia kwa kuletewa na hizi courier services kama DHL, TNT au EMS. Kama unafanya kazi ni vizuri kutumia anuani ya kazini kwako, na pia kuna sehemu unaweka namba yako ya simu, hivyo mzigo ukija tu wanakupigia simu ili wakupate. Maana huduma ya Paypal, unalipia hadi gharama ya kuletewa mzigo ulipo.
 
Nimefanikiwa kulink credt card yang na paypal. Sasa swali linakuja,pale kwenye shipping adress ivi unaweka adress yako ya posta au? Maana kwa wenzetu hususan marekani hua kuna street adress kabisa sasa mimi nakaa Goba kwa Ndambi ntafanyaje? Asanten wakuu

Naomba unijuze ulitumia CR ya bank gani?
 
Naomba unijuze ulitumia CR ya bank gani?

Kuna bank, kama sikosei ni Stanbink au Exim ambazo unaweza ukawa na credit card, ila minimum balance kwenye account iwe million 3. Nijuavyo mimi bank karibu zote Tanzania zina debit card na sio credit card. Labda wataalamu watujuvye.
 
Nimefanikiwa kulink credt card yang na paypal. Sasa swali linakuja,pale kwenye shipping adress ivi unaweka adress yako ya posta au? Maana kwa wenzetu hususan marekani hua kuna street adress kabisa sasa mimi nakaa Goba kwa Ndambi ntafanyaje? Asanten wakuu

Mkuu hongera kwa kufanikiwa kulink kadi yako. Ninaomba utufahamishe zaidi kuhusu huduma za paypal na vigezo vya kujiunga. Shukrani.
 
Mkuu hongera kwa kufanikiwa kulink kadi yako. Ninaomba utufahamishe zaidi kuhusu huduma za paypal na vigezo vya kujiunga. Shukrani.

Mkuu paypal ni huduma inayokuwezesha kulipa,kupokea malipo na kununua bidhaa mtandaoni(online shopping) ni huduma ambayo ni rahis na ya uhakika na si rahisi kutapeliwa. Kikubwa unachotakiwa kuwa nacho ni kadi ya benki yenye visa au mastercard( i used tembocard visa),unaenda kwenye benk yako nakuomba kujiunga na internet banking nao wanakupa form unajaza. Baada ya hapo unaenda paypal.com na unafata procedures rahis naam ndan ya siku 2-3 utaweza kulink card yako na kununua bidhaa new york city ikaletwa mpaka mlangon kwako tandale kwa mtogore.
 
Habari zenu wakuu....ningependa kuweka ujuzi wangu hapa.....na pia nina maswali.....
Credit card ya Exim (ambayo mie ninayo)...kuna Silver (min. Balance ni 1m na unaweza kutumia hadi laki 8)...na Gold (min. Balance ni 3m)....

Hiyo Tembo Visa Card ni kutoka benki gani?...min. Balance kiasi ngapi?....

Halafu je mabenki wanaku-charge kuitumia hiyo credit card?...yaani kuna bank charges au bank commission yeyote?....
 
Kuna bank, kama sikosei ni Stanbink au Exim ambazo unaweza ukawa na credit card, ila minimum balance kwenye account iwe million 3. Nijuavyo mimi bank karibu zote Tanzania zina debit card na sio credit card. Labda wataalamu watujuvye.

Asante Ozzie77 nitalifanyia kazi , bado ningependa kujua je ni lazima account yako iwe na dollar au Tshs?
 
Shipping Address unatakiwa uweke address ambayo mzigo au barua inaweza kukufikia kwa kuletewa na hizi courier services kama DHL, TNT au EMS. Kama unafanya kazi ni vizuri kutumia anuani ya kazini kwako, na pia kuna sehemu unaweka namba yako ya simu, hivyo mzigo ukija tu wanakupigia simu ili wakupate. Maana huduma ya Paypal, unalipia hadi gharama ya kuletewa mzigo ulipo.
No paypal sio kazi yao kukupigia simu mfano kama unanunua kitu kutoka ebay au kivuko paypal kazi yao ni kuwalipa hao ebay kupitia credit card yao sasa hao ebay kazi yao ni kuufatikia mzigo wako ulipofikia na kukujulisha kupitia email,nimeitumia sana hii ebay kununulia vitu mtandaoni na software za apple kupitia paypal hao paypal huwa kuna kaasilimia kadogo sana wanakata kutokana na huduma yao,so kama uko crdb na unataka kununua vitu vya dola 500 akaunti yako isiwe chini ya laki 8 za kitanzania usiweke pesa nyingi sana kwa akaunti ya mtandao coz wajanja siku hizi ni wengi na wazungu wwenyewe nao ni wajanja sana.
 
Take care na online purchase itakuja kuku ingiza mkenge usio tarajia na usimuone wakumdai au kumshtaki unatakiwa kujua u fake haupo kwenye bidhaa tu hadi kwenye mitandao .kuna mtu sisi huku niliko alipata ichizi baada ya jamaa kukwapua 78mil na kumuachia 5elfu tu. So unatakiwa kuwa na uelewa wa kutosha sana kujua secure webs an unsecured webs sasa hiyo lazima uwasiliane na crdb au bank yeyote yenye hiyo service before kwani kuna form ambazo kwa mfano crdb wanakupa uijaze ili ili wakuingize huko kwenye hiyo huduma. Ila naungana na mdau omary salumu kwamba usiweke pesa nyingi katika a/c ambayo unatumia katika huduma ya online purchase watuwana hack hiyo card yako na unakombewa mkwanja woooooooote unaachiwa 5000/- kitunza a/c tu anbacho huwa hakitoki. Take care na huduma hii.
 
No paypal sio kazi yao kukupigia simu mfano kama unanunua kitu kutoka ebay au kivuko paypal kazi yao ni kuwalipa hao ebay kupitia credit card yao sasa hao ebay kazi yao ni kuufatikia mzigo wako ulipofikia na kukujulisha kupitia email,nimeitumia sana hii ebay kununulia vitu mtandaoni na software za apple kupitia paypal hao paypal huwa kuna kaasilimia kadogo sana wanakata kutokana na huduma yao,so kama uko crdb na unataka kununua vitu vya dola 500 akaunti yako isiwe chini ya laki 8 za kitanzania usiweke pesa nyingi sana kwa akaunti ya mtandao coz wajanja siku hizi ni wengi na wazungu wwenyewe nao ni wajanja sana.

Asante kwa ushauri wako mkuu.
 
Take care na online purchase itakuja kuku ingiza mkenge usio tarajia na usimuone wakumdai au kumshtaki unatakiwa kujua u fake haupo kwenye bidhaa tu hadi kwenye mitandao .kuna mtu sisi huku niliko alipata ichizi baada ya jamaa kukwapua 78mil na kumuachia 5elfu tu. So unatakiwa kuwa na uelewa wa kutosha sana kujua secure webs an unsecured webs sasa hiyo lazima uwasiliane na crdb au bank yeyote yenye hiyo service before kwani kuna form ambazo kwa mfano crdb wanakupa uijaze ili ili wakuingize huko kwenye hiyo huduma. Ila naungana na mdau omary salumu kwamba usiweke pesa nyingi katika a/c ambayo unatumia katika huduma ya online purchase watuwana hack hiyo card yako na unakombewa mkwanja woooooooote unaachiwa 5000/- kitunza a/c tu anbacho huwa hakitoki. Take care na huduma hii.

Sasa kujua ipi ni nzuri ni mtihani, duh poa kwa ushauri makini.
 
Take care na online purchase itakuja kuku ingiza mkenge usio tarajia na usimuone wakumdai au kumshtaki unatakiwa kujua u fake haupo kwenye bidhaa tu hadi kwenye mitandao .kuna mtu sisi huku niliko alipata ichizi baada ya jamaa kukwapua 78mil na kumuachia 5elfu tu. So unatakiwa kuwa na uelewa wa kutosha sana kujua secure webs an unsecured webs sasa hiyo lazima uwasiliane na crdb au bank yeyote yenye hiyo service before kwani kuna form ambazo kwa mfano crdb wanakupa uijaze ili ili wakuingize huko kwenye hiyo huduma. Ila naungana na mdau omary salumu kwamba usiweke pesa nyingi katika a/c ambayo unatumia katika huduma ya online purchase watuwana hack hiyo card yako na unakombewa mkwanja woooooooote unaachiwa 5000/- kitunza a/c tu anbacho huwa hakitoki. Take care na huduma hii.
Paypal ni kitu kingine kabisa. Kuhusu kutapeliwa ni kwa kutumia njia zingine kulipa for online purchase na siyo paypal. Njia hizo ziko nyingi including Western Money Union, Moneygram nk. Tofauti wengine Paypal wana mikataba na hao unaonunua kwao. Kwa mfano ebay au amazon etc. In the event umenunua kitu say toka ebay na hakijakufikia after agreed time, paypal wanaku-refund pesa yote uliolipia.Kwa kifupi ni kwamba ukinunua kupitia PayPal hakuna swala la kupoteza fedha yako. Changamoto ni kujitaidi kununua vitu online ktk maduka yanayotumia huduma ya PayPal kwa malipo.
 
No paypal sio kazi yao kukupigia simu mfano kama unanunua kitu kutoka ebay au kivuko paypal kazi yao ni kuwalipa hao ebay kupitia credit card yao sasa hao ebay kazi yao ni kuufatikia mzigo wako ulipofikia na kukujulisha kupitia email,nimeitumia sana hii ebay kununulia vitu mtandaoni na software za apple kupitia paypal hao paypal huwa kuna kaasilimia kadogo sana wanakata kutokana na huduma yao,so kama uko crdb na unataka kununua vitu vya dola 500 akaunti yako isiwe chini ya laki 8 za kitanzania usiweke pesa nyingi sana kwa akaunti ya mtandao coz wajanja siku hizi ni wengi na wazungu wwenyewe nao ni wajanja sana.

Kwanza mkuu Paypal hawakati hata senti moja kwa mnunuzi bali wanachukua kamisheni kwa muuzaji. Pili unapolipia bidhaa kwa Paypal yaiwezekani kuibiwa, kinachofanyka ni hichi:-

Unapojisajili kwenye Paypal wao wanaweka taarifa za akaunti yako, unaponunua bidhaa kutoka kwa muuzaji yeye hawezi kuzipata taarifa za akaunti yako ila wewe unawapelekea taarifa Paypal kisha Paypal wanamlipa fedha muuzaji aliyekuuzia wewe bila ya kumpa taarifa za akaunti yako ya benki. Hivyo basi njia hii ni salama kwenye ununuzi.

Vile vile eBay sio wanaokutafuta wewe na kukutumia bidhaa unayonunua, eBay hawana bidhaa hata moja bali wauzaji mbali mbali huuza bidhaa zao kupitia mnada wa eBay. Kwa hiyo unaponunua bidhaa kwenye eBay uwe makini na kuhakikisha kwamba muuzaji yuko tayari kupost mzigo kuja Tanzania. Wengi huorodhesha nchi ambazo wako tayari kupost, ikiwa hakuorodhesha unaweza kumuandikia email na kumuuliza muuzaji kabla ya kununua, kama yuko tayari kupost Tanzania na atakuchaji shilingi au dola ngapi.

Mwisho kabisa ukilipia bidhaa kwenye eBay na kulipa kwa Paypal, iwapo mzigo haukukufikia Paypal wanakurudishia fedha zako zote bila ya kukata hata senti moja. Lakini huchukua muda kama wa mwezi mmoja kufanya uchunguzi ni kwa nini mzigo haukukufikia na kuhakikisha kwamba wewe sio tapeli uliyepokea mzigo kisha unajifanya hukuupata. Mimi binafsi nilishawahi kununua simu miaka michache iliyopita, nakumbua ilikuwa ni HTC Advantage kwa £300.00, kumbe jamaa alikuwa ni tapeli akaingia mitini kwa hiyo nililipwa pesa yangu ingawa ilichukua takriban siku 40 hivi.
 
habari zenu wakuu....ningependa kuweka ujuzi wangu hapa.....na pia nina maswali.....
Credit card ya exim (ambayo mie ninayo)...kuna silver (min. Balance ni 1m na unaweza kutumia hadi laki 8)...na gold (min. Balance ni 3m)....

Hiyo tembo visa card ni kutoka benki gani?...min. Balance kiasi ngapi?....

Halafu je mabenki wanaku-charge kuitumia hiyo credit card?...yaani kuna bank charges au bank commission yeyote?....

tembo card ni ya crdb
 
Huduma ya paypal inamilikiwa na eBay so ukilipia via paypal kununua ebay kuna uhakika zaidi kuliko kununua amazon ama alibaba
 
Back
Top Bottom