Msaada: Natafuta watu wakuning'olea visiki na kusafisha shamba

Msaada: Natafuta watu wakuning'olea visiki na kusafisha shamba

rhysrose

Member
Joined
Aug 8, 2012
Posts
13
Reaction score
4
Habarini,
mi ni mkulima na nategemea kuotesha mwezi wa 3. Nina tatizo moja, bajeti yangu ya kusafisha shamba haendani na matakwa ya wanakijiji walionizunguka kwa sasa. Niko tayari kutoa 50,000 TZS kwa eka(70X70), ukubwa wa shamba ni ekari 50.
Nimefahamishwa kuwa inawezekana kuajiri kutoka mkoani, nguvu kazi itakayoweka kambi shambani na kulisafisha. Naomba msaada kwa yeyote mwenye ufahamu, ili kufanikisha hili-- asante.

shamba liko bagamoyo--njia ya msata.
 
Je kutafuta vibarua wa mbali si ndio gharama zaidi mf. Nauli ya kuwatoa kwao, malazi, chakula au hivyo vyote ni inclusive ktk package yako?
 
Kweli bagamoyo kuzuri ila tatizo manpower. Ushauri wangu kama umeweka kibanda tafuta watu wa kudumu kutoka mbali uwalipe kwa mwezi. Vibarua uko vigumu kuwa monitor wenyeji wavivu sana.
 
Habarini,
mi ni mkulima na nategemea kuotesha mwezi wa 3. Nina tatizo moja, bajeti yangu ya kusafisha shamba haendani na matakwa ya wanakijiji walionizunguka kwa sasa. Niko tayari kutoa 50,000 TZS kwa eka(70X70), ukubwa wa shamba ni ekari 50.
Nimefahamishwa kuwa inawezekana kuajiri kutoka mkoani, nguvu kazi itakayoweka kambi shambani na kulisafisha. Naomba msaada kwa yeyote mwenye ufahamu, ili kufanikisha hili-- asante.

shamba liko bagamoyo--njia ya msata.

Mkuu tangazo lako halijakaa sawa.
Ebu niambie shamba lako lina wastani wa visiki vingapi kwa heka,ni visiki vya miti gani?una vifaa vya kun'golea?camp inausalama wa kutosha?vyakula na matibabu unaghalamia?
Nijibu alafu tuongee nikutafutie vijana3 wakufanyie kazi utafurahi.
 
Habari,
niko tayari kumpeleka mwakilishi kuliangalia!
Package ni inclusive.
Ninamalizia kibanda cha vyumba 2 shambani-- ndipo kambi itakaa!
Sina vifaa/ japokuwa kama ni lazima niko tayari kuvitafuta!


Mkuu tangazo lako halijakaa sawa.
Ebu niambie shamba lako lina wastani wa visiki vingapi kwa heka,ni visiki vya miti gani?una vifaa vya kun'golea?camp inausalama wa kutosha?vyakula na matibabu unaghalamia?
Nijibu alafu tuongee nikutafutie vijana3 wakufanyie kazi utafurahi.
 
Dah, vibarua wa kutafutia JF!!....hii nimeipenda, ngoja nifanye mpango wa udalali hapa!
 
Dah, vibarua wa kutafutia JF!!....hii nimeipenda, ngoja nifanye mpango wa udalali hapa!

Mwanzoni hata mie nilitaka kushangaa hivyo hivyo kama wewe lakini baadaye nikaona kumbe inawezekana!! Maana cheki ushauri anaopewa na wadau ama kweli huu ni ulimwengu wa dijiti mpaka vibarua wanatafutwa Jf! Mkuu nenda kaibe vibarua mpakani mwa Tz n Burundi, wale viumbe wanachapa kazi asikwambie mtu. Sasa kwa hao Wakwere si utaumia mkuu? Hao wako tayari kuacha ngese na kwenda ngomani!
 
kutokana na pesa yako kuchelea, anza na ekari chache eg 10 na watumie hao hao wakwere
 
Malazi, Matibabu, Chakula na Nauli za Kuwatoa Mkoani vikipatikana, na pia zana madhubuti kwa kazi hiyo vikiwepo hautakosa vijana.

Hata kutoka Arusha kuja huko ni rahisi
 
Mwanzoni hata mie nilitaka kushangaa hivyo hivyo kama wewe lakini baadaye nikaona kumbe inawezekana!! Maana cheki ushauri anaopewa na wadau ama kweli huu ni ulimwengu wa dijiti mpaka vibarua wanatafutwa Jf! Mkuu nenda kaibe vibarua mpakani mwa Tz n Burundi, wale viumbe wanachapa kazi asikwambie mtu. Sasa kwa hao Wakwere si utaumia mkuu? Hao wako tayari kuacha ngese na kwenda ngomani!

Nmecheka sana, ina maana Wakwere ni wavivu balaa? Mimi nina project kusini, nilishindana na wenyeji nikaamua kufuata kwetu usukumani, wanapiga kazi vibaya mno. Suala kubwa ni kutowanyonya maslahi, sivyo watarubuniwa kirahisi, wawekee mazingira mazuri ya kuishi, milo mizuri ya uhakika na malipo bila kuchelewa.
 
Nmecheka sana, ina maana Wakwere ni wavivu balaa? Mimi nina project kusini, nilishindana na wenyeji nikaamua kufuata kwetu usukumani, wanapiga kazi vibaya mno. Suala kubwa ni kutowanyonya maslahi, sivyo watarubuniwa kirahisi, wawekee mazingira mazuri ya kuishi, milo mizuri ya uhakika na malipo bila kuchelewa.

Hapo wa Ng'wise umegusa penyewe!

Misukuma inavyochapa kazi hasa kama mazingira ni mazuri mbona utaipenda?!! Huyu jamaa kama atawategemea akina Ki.kwete hapati kitu maana jamaa zangu ni wavivu mwanzo - mwisho! Mpaka Kiongozi wao ameonesha uvivu kwenye utawala!!
 
Hapo wa Ng'wise umegusa penyewe!

Misukuma inavyochapa kazi hasa kama mazingira ni mazuri mbona utaipenda?!! Huyu jamaa kama atawategemea akina Ki.kwete hapati kitu maana jamaa zangu ni wavivu mwanzo - mwisho! Mpaka Kiongozi wao ameonesha uvivu kwenye utawala!!

Lol! Ni kweli Mkuu.
 
Habarini,
mi ni mkulima na nategemea kuotesha mwezi wa 3. Nina tatizo moja, bajeti yangu ya kusafisha shamba haendani na matakwa ya wanakijiji walionizunguka kwa sasa. Niko tayari kutoa 50,000 TZS kwa eka(70X70), ukubwa wa shamba ni ekari 50.
Nimefahamishwa kuwa inawezekana kuajiri kutoka mkoani, nguvu kazi itakayoweka kambi shambani na kulisafisha. Naomba msaada kwa yeyote mwenye ufahamu, ili kufanikisha hili-- asante.

shamba liko bagamoyo--njia ya msata.

Kwa Kweli hili tatizo ni kubwa sana hapa kwetu!! cha kufanya mkuu malizia banda hilo la kuishi vibarua kisha agiza kutoka mkoani. wape mshahara hakikisha akijikwaa kazini unaruka nae kliniki ya karibu kufunga kidonda na panadoli kwa wingi. ukiwatembelea usisahau fegi na kuwaachia senti ya kwenda kupumzika na wenyeji jioni. hayo yalinikuta mimi na mambo yakawa fresh tu. ila kitu kimoja wenyeji kwa wivu huwa wanaanzisha mambo ya wizi. wataondoka hata na nguzo za mipaka ili tu uwalaumu watu wako. Puuza mambo kama hayo. majuzi nilienda shamba na badala ya kuwaachia ya kuramba MNAZI nikachomoa Scotch mbili kutoka kwenye buti. siku chache baadae wana ni beep mzee njoo utuongeze kazi ile tumemaliza 🙂 Mimi mwenyewe nilichoka kazi ya wiki wanaume wameipiga kwa siku nne. kawavute waje uwape ajira wale wanaotaka ajira. usipoteze muda ingawaje watasema sisi tupo unaenda kuleta wa nje!! swali nikwamba ufanyeje??
 
Uvivu wao unanikumbusha mbali sana jamaa hao walivamia bank nakuiba wakiwa wawili mchaga na mzaramu Kisha wakafanikiwa walipo fika kwao mchaga. Akilini mwake aliwaza akiwa njianikua wakifikatu waesabu pesa lkn mzaramu alimwambia tusubili tarifa yahabari itatangaza tumeiba kiasi gani chapesa ndio tujue idsdi hao ndio wazaramu bwana ukitaka wachapazi nenda nje yamkoa wapwani ndugu
 
Vibarua wa mashamba katika ukanda ya ni matatizo matupu.
 
Je kutafuta vibarua wa mbali si ndio gharama zaidi mf. Nauli ya kuwatoa kwao, malazi, chakula au hivyo vyote ni inclusive ktk package yako?

Bora kutoa gharama hizo tangu mwanzo kisha unajua kazi itafanyika, kuliko kusevu pesa na kila siku ukienda ukirudi unakuta watu wamejipumizisha chini ya ule mti uliosema wasiukate. ukiuliza wao wanalia njaa tu. na story nyingi kupita kiasi. mbaya zaidi wanakupa matarajio kwamba leo jua likipungua wataanza kufyeka kule juu mpaka kesho watakuwa wamemaliza. kesho ukija pako vile vile. na wao wenyewe sio kwamba wanachakarika! hapana inabidi utume mtoto akawaite kkutoka kijiwe cha ulabu. chagua muungwana gharama ama tusevu senti??
 
Pesa yako ndogo, kufyeka shamba inagharimu shilingi 70,000/= hadi 100,000/= kwa ekari moja. Kung'oa visiki angalau kwa uchache uwe na shlingi 300,000/= hadi 500,000/= kwa ekari moja, bei hii itategemea wingi wa visiki na ukubwa wa visiki.
 
Kungoa visiki laki5 duuuuu kuweni Sirius ayo mashamba mengine ndio bei kwaeka
 
Kungoa visiki laki5 duuuuu kuweni Sirius ayo mashamba mengine ndio bei yakununulia iweje umpemng'oa visiki
Reasonable 50elf
 
Habarini,
mi ni mkulima na nategemea kuotesha mwezi wa 3. Nina tatizo moja, bajeti yangu ya kusafisha shamba haendani na matakwa ya wanakijiji walionizunguka kwa sasa. Niko tayari kutoa 50,000 TZS kwa eka(70X70), ukubwa wa shamba ni ekari 50.
Nimefahamishwa kuwa inawezekana kuajiri kutoka mkoani, nguvu kazi itakayoweka kambi shambani na kulisafisha. Naomba msaada kwa yeyote mwenye ufahamu, ili kufanikisha hili-- asante.

shamba liko bagamoyo--njia ya msata.

Mchina akiwekeza hoteli akaajiri wafanyakazi toka India tunapiga kelele oo hawatoi ajira kwa wazawa! Nakushauri komaa ongeza dau uwape ajira wakwere vinginevyo utahujumiwa adi uone kizunguzugu, wewe unataka uwekeze shamba la ekari 50 afu wenyeji wasitafune hata shillingi yako! Uwekezaji endelevu lazima uwe rafiki na majirani. Angalia kama kukwepa kuwatumia wenyeji kutakuongezea faida ya kudumu, wao wanajua mazingira ya eneo hilo, wanazijua vema fursa na matatizo ya eneo hilo, kalaga baho.

 
Back
Top Bottom