Msaada: Nahisi mtoto wangu ameathirika na Runinga

Msaada: Nahisi mtoto wangu ameathirika na Runinga

Sajenti

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2008
Posts
3,651
Reaction score
414
Nina mtoto wa kike wa miaka 9 na sasa anasoma darasa la 4. Kwa ujumla katika masomo yake amekuwa akijitahidi sana hata mimi anani-impress. Tangu yuko darasa la 1 habanduki katika wale wanafunzi watano wa kwanza.

Tatizo lillilojitokeza ni tangu mwaka huu uanze. Kwa mapenzi tu kama mzazi niliamua kuwafungia Dstv pale nyumbani angalau nao wapate kuburudika. Lakini sasa naelekea kujilaumu kwani binti amekuwa anatumia muda wake mwingi kuangalia TV na hasa ile channel ya Catoon (Catoon Network).

Nilipoona anakuwa busy sana na Tv nilimueleza kwa upole tu apunguze hiyo kitu na akakubali, lakini hata binti wa kazi amenieleza kuwa anaporudi shule tu yeye yuko kwenye Tv.

Nikaamua kuwa naficha remote ninapotoka nyumbani huenda itamfanya apunguze hiyo kitu. Kiasi nafikiria hata kuachana na matumizi ya Tv kabisa maana hapo nyuma nilikuwa namnunulia DVD za catoon kama Tom & Jerry na nyingine sasa amekuwa mpaka anaenda kuazima kwa rafiki zake.

Nakosa amani kabisa.
 
The other side of utandawazi.hata ufiche remote watenda kucheki kwa jirani.
 
Huyuo ni wa kuongea nae kwenye round-table tu mkuu, na kushauriana nae.
Huwezi kumdhibiti kwasasa, maana hiyo hobby iko damuni...
 
Sajenti

ni ajabu kuwa mtoto mdogo ndo anayekuongoza hapo home. mimi watoto wangu nawapenda sana, nikirudi home wananirukia, lakini nikisema kitu fulani sitaki, hakuna anayefanya. kwasababu huwa nawarudi pia kama wakikosea.Wewe huho mtoto wako wa miaka tisa inaelekea ni yai, unaogopa kulidondosha, sasa unatengeneza bom.

Unatakiwa kumakamata, mtandike fimbo za kutosha, mwambie hakuna kuangalia luninga kwa mida uliyokataza. akirudia tena, njoo niambie. msiwalee watoto wenu kama watoto wa ulaya ambao wanawajibu hata wazazi wao, ambao mzazi umelala kitandani unashitukia mtoto tayari ameshaingia chumbani kwenu wewe na mkeo bila hata hodi anaomba kalamu, waleeni watoto wenu kwa adabu, ili wakija kuwa watu wazima wawashukuru, ukiwalea vibaya watakuja kukulaumu wakijakupata akili na watakutelekeza uzee wako utaula kwa shida.
 
Last edited by a moderator:
Kwa hapo mkuu, bakora zitasaidia kimtindo!
 
Mwana wa Mungu

Nimekupata mkuu...Si kwamba sijui kucharaza, ni mzuri sana katika kutembeza bakora isipokuwa sipendelei sana ukizingatia kwenye mambo mengi ninayomkataza anatii. Haya nitajaribu kutembeza mjeledi...
 
Last edited by a moderator:
Kwa hapo mkuu, bakora zitasaidia kimtindo!

Katavi ushauri wako mbaya wewe ..viboko vitamfanya awe sugu
swala hapo ni kuongea nae kwa upole na kumpangia ratiba ya kusoma pia ya kuangalia Tom & jerry umri huo bado ni wa kujifunza
 
Huyuo ni wa kuongea nae kwenye round-table tu mkuu, na kushauriana nae.
Huwezi kumdhibiti kwasasa, maana hiyo hobby iko damuni...
...Thanks. Hata mimi napendelea sana dialogue nae.
 
Hapo unatakiwa kumpangia ratiba ,kama ni jumamosi na jumapili

watoto wanahaki ya kupumzika, kaka mimi wala sioni sabu ya wewe kujutia uamuzi wako wa kuwafungia DStv watoto wako ilikuwa ni haki yao na umefanya hivyo kama mzazi the thing which I congratulate you. Maoni yangu ni kuwa nafikiri ushauri huu hapo juu ni mzuri mpangie ratiba tu, kuwa akitoka shule anaweza tizama Tv kwa muda fulani tu, baada ya hapo aji engage katika homework, ila nafikiri ni vizuri nawe kama huna majukumu mengi yanayokubana uwe nyumbani mapema kumsaidia kwa homework zake na kuhakikisha ratiba uliyompangai anaifuata, hapa viboko sio dawa kabisa!
 
  • Thanks
Reactions: ral
Katavi ushauri wako mbaya wewe ..viboko vitamfanya awe sugu
swala hapo ni kuongea nae kwa upole na kumpangia ratiba ya kusoma pia ya kuangalia Tom & jerry umri huo bado ni wa kujifunza
..Nimekugongea senksi kule FL1. Huwezi kuamini huyu binti huwa nazungumza nae kama mtu mzima mwenzangu kiasi kwamba mengi ninayomueleza hutekeleza mpaka nashangaa, I wish siku moja ungekaa uzungumze nae FL1!
 
....ndugu yangu ...mrushe mtoto angaza .....wale wanatoa ushauri na 'saa' ...ukifika acha ushauri chukua saa ..chagua nzuri mpe mtoto ataipenda ata chukia tv...
 
..Nimekugongea senksi kule FL1. Huwezi kuamini huyu binti huwa nazungumza nae kama mtu mzima mwenzangu kiasi kwamba mengi ninayomueleza hutekeleza mpaka nashangaa, I wish siku moja ungekaa uzungumze nae FL1!

Mbona mimi nimekushauri exactly kama FL1, (tena nilitangulia)wala hujanigongea senksi.,..Tutafika kweli wakunyumba?
 
Sajenti Hivi hapo kwako hakuna miti ukate viboko? Mboja unapoteza muda wakti vibo vipo hata maneno ya Mungu yanashauri kuwachapa. Ila usijeruhi sana!
 
NIMESOMA KWA PUPA MADA NIKIJUA AMEATHIRIKA NA UKIMWI ........daaaah mbona unnawapa watu prsha aaaah..........mi dstv inaharibu hata kazi nyumbani saa nyingine hazifanyiki kutwa moviemagic......nakuonea huruma huyo mtoto na katuni hahaha
 
this comedian is talking about beating kids on youtube

 
Last edited by a moderator:
Ohh Pole rafiki na hali hiyo. But unaweza ku mcontrol mapema, ni bado mdogo anaweza kubadilika. Samaki mkunje angali mbichi
 
Mbona mimi nimekushauri exactly kama FL1, (tena nilitangulia)wala hujanigongea senksi.,..Tutafika kweli wakunyumba?
....Sawa wa kunyumba nimegonga pale. Kotoka kuhyoma mlongo wangu chabwina lepa!!!...
 
Sajenti Hivi hapo kwako hakuna miti ukate viboko? Mboja unapoteza muda wakti vibo vipo hata maneno ya Mungu yanashauri kuwachapa. Ila usijeruhi sana!
Mkuu, miti ni kwa ajili ya matunda na kivuli si kuchapia watoto!!! Taratibu mazee!
 
Back
Top Bottom