watoto wanahaki ya kupumzika, kaka mimi wala sioni sabu ya wewe kujutia uamuzi wako wa kuwafungia DStv watoto wako ilikuwa ni haki yao na umefanya hivyo kama mzazi the thing which I congratulate you. Maoni yangu ni kuwa nafikiri ushauri huu hapo juu ni mzuri mpangie ratiba tu, kuwa akitoka shule anaweza tizama Tv kwa muda fulani tu, baada ya hapo aji engage katika homework, ila nafikiri ni vizuri nawe kama huna majukumu mengi yanayokubana uwe nyumbani mapema kumsaidia kwa homework zake na kuhakikisha ratiba uliyompangai anaifuata, hapa viboko sio dawa kabisa!
Kwa hapo mkuu, bakora zitasaidia kimtindo!
Mwana wa Mungu
Nimekupata mkuu...Si kwamba sijui kucharaza, ni mzuri sana katika kutembeza bakora isipokuwa sipendelei sana ukizingatia kwenye mambo mengi ninayomkataza anatii. Haya nitajaribu kutembeza mjeledi...
Kama anatii hayo mengine, kwa nini hilo moja awe mkaidi? Ni lazima mtoto amtii mzazi wake, vinginevyo hata maendeleo yake katika masomo yatakuwa bure. Si sahihi mzazi uanze kuhangaika na kuficha remote ya TV,au kung'oa kabisa TV kwa sababu mtoto under 10 years hataki kusikia unachosema.
"Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu" (Ufunuo Wa Yohana 1:19)
Post za zamani zilikua na akili duh!
Malezi ya kipumbavu hayo! wewe mtu mzima unategemea mtoto aache kutazama Tv muda wote wakati hajui madhara yake!!
Mtoto unamuelimisha taratibu na kumuonya kuhusu madhara ya kutazama television, asipokusikia ni fimbo tu.
ukilikoroga lazima ulinywe. Kazi kwakoNina mtoto wa kike wa miaka 9 na sasa anasoma darasa la 4. Kwa ujumla katika masomo yake amekuwa akijitahidi sana hata mimi anani-impress. Tangu yuko darasa la 1 habanduki katika wale wanafunzi watano wa kwanza.
Tatizo lillilojitokeza ni tangu mwaka huu uanze. Kwa mapenzi tu kama mzazi niliamua kuwafungia Dstv pale nyumbani angalau nao wapate kuburudika. Lakini sasa naelekea kujilaumu kwani binti amekuwa anatumia muda wake mwingi kuangalia TV na hasa ile channel ya Catoon (Catoon Network).
Nilipoona anakuwa busy sana na Tv nilimueleza kwa upole tu apunguze hiyo kitu na akakubali, lakini hata binti wa kazi amenieleza kuwa anaporudi shule tu yeye yuko kwenye Tv.
Nikaamua kuwa naficha remote ninapotoka nyumbani huenda itamfanya apunguze hiyo kitu. Kiasi nafikiria hata kuachana na matumizi ya Tv kabisa maana hapo nyuma nilikuwa namnunulia DVD za catoon kama Tom & Jerry na nyingine sasa amekuwa mpaka anaenda kuazima kwa rafiki zake.
Nakosa amani kabisa.
Mkuu, miti ni kwa ajili ya matunda na kivuli si kuchapia watoto!!! Taratibu mazee!
Hapo unatakiwa kumpangia ratiba ,kama ni jumamosi na jumapili