Mkasa wa kweli: Nilifanywa boya kwa zaidi ya miaka kumi na mitatu akidai ana mtoto wangu

Aug 13, 2020
25
72
Mwaka 2008 nilikutana na Binti nikawa nampatia lift kuelekea Posta tukaingia kwenye mahusiano, nilimuuliza Kama ameolewa akasema hapana anaishi na wazazi wake. Mimi nilimwambia kuwa Nina mke na familia hivyo tukawa na mahusiano ya Siri kubwa Sana.

Sasa mwaka 2017 katika mahusiano akasema anahitaji mtoto tukakutana akasema ana ujauzito wangu nikawa namhudumia kwa ukaribu zaidi, kila nikimwambia mbona huendi clinic akawa ananiambia atakwenda. Kuna siku akanipigia simu kuwa Yuko clinic anahitaji taarifa zangu zote nikampatia, siku za kujifungua zilipokaribia akaenda Muhimbili na dadayake na ndugu zake.

Akafanyiwa operation na kupoteza fahamu siku tatu kabla ya hapo alinitumia message kuwa akifa mtoto yupo na dadayake wa masaki. Kwa Neema yake Mungu akazinduka tukaongea na dadayake na mama yake na yeye mwenyewe. Hivyo akawa anaishi kwa dadayake wa huko masaki na shemeji yake, nikawa nawasiliana nao Mara kwa Mara hasa kwa njia ya message nikitumia simu ya mzazi mwenzangu.

Miaka ikawa inasonga kila nikitaka kumwona mtoto vizingizio kibao Mara Yuko busy Mara mtoto hayupo n.k. Alipotimiza miaka miwili nilimwambia anitumie picha kwa njia ya WhatsApp, alituma hiyo picha ya mtoto wa kiume. Alipofikisha miaka mitatu akasema amempeleka shule huko huko Masaki wanakosoma watoto wa dadayake na gharama zake milioni mbili kwa mwaka na usafiri Mimi nichangie.

Nilimkatalia kuwa hukunishirikisha kwanza, pili gharama kubwa kwa chekechea. Mimi kipindi hicho hicho hali yangu ya kifedha ilikuwa sio nzuri. Akawa anasomesha mwenyewe Mimi nachangia vitu vidogo tu, Shule ikifunga namwambia nakuja huko huko masaki kumwona mtoto anasema ameshamsafirisha Singida kwa bibi yake na likizo nyingine kwa kaka yake Dodoma eti kwa vile sichangii gharama za shule.

Mara akaniambia kahamishwa kwenda Mtwara kikazi Mara kasema kahamishwa Mtwara kwenda Morogoro Mara kahamishwa Yuko Iringa kikazi kumbuka Mimi ninatoa mshahara wa Binti wa kazi wa kumlea mtoto wangu. Mara ya mwisho kasema kampuni yake inampeleka kusoma Canada kwa miaka mitatu na mtoto atamwacha kwa dadayake wa masaki.

Tukawa tunawasiliana na dadayake na shemeji yake kwa mahitaji madogo yakijitokeza. Naye tulikuwa tukiwasiliana Mara kwa mara akiwa huko chuoni Canada. Kwa miaka miwili alikuwa anarudi December tunakutana wakati wowote ule nikimhitaji na wakati wa usiku Kama bi mkubwa wangu hayupo tunapigiana WhatsApp call. Sasa mwaka wa pili mwishoni karudi December mwaka huu 2022 mwishoni na tarehe 31 December akanipigia simu kuwa nisipokee simu yake ikipigwa akajichanganya akasema simu ameidondosha.

Na Mimi nikajisemea kimoyo moyo nitapokea ikipigwa. Kweli ikipigwa nikapokea akajitambulisha kuwa yeye ndiye mume wa huyo mke tangu mwaka 2010 na wamezaa watoto wawili wa kwanza miaka kumi na WA pili miaka minane. Nami nikamwambia kuwa huyo nimekuwa na mahusiano miaka kumi na tatu hadi Sasa na nimezaa naye mtoto wa kiume kwa Sasa ana miaka mine.

Akaniuliza ulisha wahi kumwona huyo mtoto, nikasema hapana kwa Sasa anaishi masaki kwa sababu huyo Yuko masomoni Canada. Akaniambia Hana dadayake masaki hajawahi hata kupanda ndege hajawi kufanya kazi Mtwara, Morogoro Wala Iringa.

Hana mtoto wa kiume wa miaka hiyo minne Wala Hana mashamba Singida ekari thelathini Wala Hana nyumba Morogoro wala Hana gari Wala Hana kazi ni mama wa nyumbani Wala Hana nyumba Pugu Wala Hana nyumba Chanika. Hayo yote alikuwa aliniambia kuwa anavyo vitu hivyo kumbe ni mwongo wa kutupwa ni mafia wa kimataifa.

Alisema anafanya kazi maeneo ya Mtava katika kampuni inayoshughilika na furniture. Niliongea Sana na mume wake kuwa wazazi wake wanamjua na mama yake mzazi yupo Dar maeneo ya Zingiziwa Wala sio huko Singida pia baba yake mzazi hajazikwa Singida ila kazikwa hapa Dar kwangu alisema walisafirisha. Kwangu alisema dadayake wa kwanza yeye wa pili na dadayake alizaa akiwa form two na wadogo zake watatu kumbe mwongo yeye wa kwanza na mdogo wake mmoja tu na mdogo wake wa kike ni mmoja ambao hai wote walikuwa wanaishi kwa shemeji Yao na huyu mdogo kamaliza form four mwaka Jana.

Kuna mengi Sana aliyokuwa akinidanganya kuwa kavamiwa Mtwara, kavamiwa Morogoro kavamiwa Chanika kapewa sumu na mtoto alipewa sumu n.k. Ila za mwizi arobaini zimeshatimia nawashauri wengine kuchukua tahadhari Kama hizi mimi nimepigiwa nilifanywa boya kwa zaidi ya miaka kumi na mitatu tunashare mke mmoja na wanaume wawili bila kujulikana.

Ila siku aliyopigiwa simu kuwa tumekutana na Mimi mke nasikia alizimia kwa ufupi ndio mwisho wa mawasiliano yake na yangu uamuzi atabakiwa kwa mume wake. Ila nilimshauri kuwa asimwache kwa vile kazaa naye naye alinishauri niende kwa mama yake mzazi wa mke tukaongee issue hii nilikataa.

Kuna mengi Sana sijaandika ila kwa ufupi mume wake aliniambia mke wake anahusudu Sana waganga wa kienyeji sijui aliniloga Mimi na akamloga mume wake pia. Mungu ndiye mweza wa kila jambo na wakati wake. Tafakari chukua hatua uanze kumtukana maana huu mkasa wa kweli utawasaidia na wengine kwa wanawake wa tabia Kama hizi za kupenda huku na huku.

Mungu awabariki wote mtakaosoma ujumbe huu najua hata wahusika watausoma ujumbe huu. Nimefunga mwaka kwa haya nadhani na mume wake amefunga mwaka kwa hivyo, Amina.
 
Maisha haya ya mahusiano kizungumkuti sometimes...
ila next time be carefully, ungetafuta kama 150k-250k vijana wakihuni kibao wanaofanya kazi kampuni za simu kwa 200k au 250k wanatrace namba kibishi night kali japo wakikamatwa ni msala lakini wana wanapiga dili hizo kujua mawasiliano yake au ungemtafuta afande mdogo wa upelelezi ungemshikisha 150k au 200k ungempa namba ungemwambia nataka nijue mawasiliano ya hii namba ange'trace kupitia kampuni za simu si wana authority ya kupewa taarifa kwa shughuli za kiusalama/kipelelezi tu kama wanavyo'trace wezi wa simu au waharifu wengine na sms ungeprintiwa angekupatia.
hizo sasa ni njia za kimafia ungeona kila kitu, kusuka au kunyoa ingekuwa juu yako maadam hakuna kutajana.

Nb: Wewe ulikolea sana ndio maana ulishindwa kumfatilia kwa undani.
 
Back
Top Bottom