Msaada: Maeneo mazuri ya kuishi Dar es Salaam

Msaada: Maeneo mazuri ya kuishi Dar es Salaam

Kila eneo ni zuri kuishi Dar es salaam, cha muhimu uwe na hela tu...hata ukikaa tandika au tandale utakuwa mfalme tu...Focus maisha kwanza achana na biashara ya maeneo gani mazuri kuishi huku unakwenda kupanga...
 
Kila eneo ni zuri kuishi Dar es salaam, cha muhimu uwe na hela tu...hata ukikaa tandika au tandale utakuwa mfalme tu...Focus maisha kwanza achana na biashara ya maeneo gani mazuri kuishi huku unakwenda kupanga...
hii ndio pointi ya msingi maeneo mengi ya dsm yanafanana fanana, na ni kawaida mji huu kukuta jirani kajenga ghorofa pembeni nyumba ya vyumba viwili, ama huyu anaishi kizungu kabisa halafu jirani anaishi kiswahili kimtaani kabisa, la msingi anagalia umbali wa unapokaa na kazini, ila lifestyle ni maamuzi yako na aina ya nyumba uliyopanga maana hata hiyo manzese yenye tandale kuna watu wamepanga apartment mpya mpya za barabarani na morogoro road , wako karibu na mwendokasi wako karibu na mjini na ubungo haf ni manzese hiyohiyo
 
Kitunda mwanagati, buza baadhi ya maeneo, tabata baadhi ya maeneo(segerea,kinyerezi etc ) goba, makumbusho, ubungo, kimara, kibamba, Kiluvya, ......nimechoka kuandika
Unataka akae Kibamba na Kiluvya serious?
 
Habari wana JF,

Kwa wale Wana-Ndugu ambao wanaifahamu Dar es Salaam vizuri, ni Maeneo au Mitaa gani ya kuishi (kupanga nyumba/chumba) ambayo yanalandana na sifa zifuatazo?

1. Sio maeneo ya uswazi/uswahilini
2. Sio pakishua sanaa/Expensive estate
3. Hayana matukio makubwa ya wizi na vibaka
4. Hakuna tatizo la maji tiririka
5. Upatikanaji wa karibu wa huduma za kijamii na kiuchumi. (maji, kiosk, etc)
6. Inaweza kuwa nje ya mji ila isiwe mbali sanaa na mjini kivile
7. Haikumbwi na mafuriko wakati wa mvua

Ahsante.
Kkoo ndio kila kitu
 
Habari wana JF,

Kwa wale Wana-Ndugu ambao wanaifahamu Dar es Salaam vizuri, ni Maeneo au Mitaa gani ya kuishi (kupanga nyumba/chumba) ambayo yanalandana na sifa zifuatazo?

1. Sio maeneo ya uswazi/uswahilini
2. Sio pakishua sanaa/Expensive estate
3. Hayana matukio makubwa ya wizi na vibaka
4. Hakuna tatizo la maji tiririka
5. Upatikanaji wa karibu wa huduma za kijamii na kiuchumi. (maji, kiosk, etc)
6. Inaweza kuwa nje ya mji ila isiwe mbali sanaa na mjini kivile
7. Haikumbwi na mafuriko wakati wa mvua

Ahsante.
Tabata ...bima,segerea,kinyerezi
 
Njoo uishi kigamboni nitakupa na sababu. Before mm nilikuwa naishi sinza, maisha ya sinza kwa kijana anaetaka kuwa na Mae ndeleo sio pazuri hata kidogo...kwa sababu kuna vishawishi vya kila aina kuhusu swala zima la starehe.

Pili aina kubwa ya watu utakakutana nao sinza, sio watu wa kukupa mawazo ya kimaendeleo wengi wao wanawaza starehe na kuvaa. Kama ujuavyo Mazingira yananguvu kubwa sana ya kubadilisha maisha ya mtu.

Nije kwenye point kwa nini kigamboni.

1. Ni mji unandelea kukua kwa kasi hivyo nirahisi ukiwa mkazi wa huku kununua eneo lako (Kiwanja) kwa ajili ya kuandaa makazi yako ya kudumu.

2. Huduma zote muhimu zinapatikana kama vile Maji, umeme, Hospitali n.k

3. Aina ya watu waliowengi waishio kigamboni ni watu wa kipato cha kati na juu, hivyo nirahisi kuwa na motisha ya kimaendeleo.

4.Usafiri unapatikana 24hrs , pia ni karibu na mjini hivyo nirahisi kufanya mambo yako kirahisi zaidi.

5. Ni mji wenye mipango mikubwa sana ya maadae, kiufupi ndio itakuwa Miami ya Dar es salaam hivyo ukifanikiwa kujenga makazi ya kudumu kigambonk i swear huwezi kujuta baadae.

6. Mazingira ya maeneo mengi ni ya kuvutia nyumba nyingi zimejengwa kisasa...hivyo hata akija mgeni wako uko proud ukiamini unakaa mazingira mazuri.

7. Ni sehemu yenye usalama, uhalifu huwezi kukosekana sehemu yoyote lakini kuna kuzidiana ukifwatilia matukio ya kiuhalifu kwa mkoa wa Dsm kigamboni utaisikia mara chache sana.

Kwa hayo machache nafikiri unaweza kufanya maamuzi mazuri.

KARIBU SANA KIGAMBONI MKUU.
duh mkuu...you are a blessing, ahsante kwa kuchukua muda wako kunielemisha ndugu.natumain kigamboni ni pana, so ni maenel gani ambayo yapo bomba zaidi..
 
Wakati Niko Dar nili enjoy Sana kuishi Kijichi.
1.Nyumba nzuri afu Bei poa
2.Usafiri upo Lami Kona zote.
3.Huduma za kijamii zipo
4.Nenda Kijichi hutajutia Tena nakupa na connection ya nyumba kama ukitaka.
Kijichi ya wapi tegeta au mbagala?
 
Back
Top Bottom