Msaada: Kutoka kwa wanasaikolojia wa mapenzi

Msaada: Kutoka kwa wanasaikolojia wa mapenzi

Ila kuoa sio lazima mkuu, we kama unahisi huna sifa tuliza ball kwanza ukishapata uwezo unaoufikiria waweza kuoa tu hakuna shida.

Busara za Davion nikiwa Yenu Bar :crazy:
 
hahahahhaaaaaa we mwenyewe ujidhamin sa utadhaminiwajeee?


acha uoga uende pepon,mtoto mzuri ajali,jiweke apo shetan asikuone
 
we kama unajijua masikini watoto wakishua unawafatilia ili iweje,nenda kwa masikini wenyako mtengeneye poverty cycle.walimu wa kibongo bana majanga
 
Natanguliza shukrani. Mimi ni kijana wa miaka ya 27 nina shahada ya ualimu na ndo kazi yangu, niliyoipata mwaka huu. Tatizo langu wana MMU ni kwamba nimebahatika kuwa na wapenzi 2 kwa vipindi 2 tofauti ambao wanatoka kwenye familia bora ikifika kipindi cha kipindi cha uchumba huwa najiona sina hadhi ya kumuoa huyo binti na hivyo kuanza kumukwepa na hatimae kuachana. Hii inatokana na kuanza kujirudi mwenyewe kwa kuangalia background yangu. Nimetoka familia fukara sana ambapo nimekulia ujombani, nimesoma kwa misaada ya watu mbalimbali, nimeishi kwa kutothaminiwa na mtu yoyote. Yapo mambo mengi ya kusimulia. Na sasa nimempata mwngine ambaye tulisoma wote lakini wazazi wake ni wasomi na heshima zao pamoja na uchumi wa kati. Binti yupo tayar tuanze uchumba lakini yale mawazo yashaanza kunijia kwa kujiona sifai. Je nifanyeje au nisioe kabisa. Nahitaji msaada wenu wana MMU, asanteni

Jiamini kama mwanaume,amini kua unaweza kutafuta na ukasomesha watoto na mkawa na familia bora kama za kwao,unachotakiwa kufanya kama umekutana na mwanamke uwe muwazi juu familia yako fukara na kule utokako ili achague kunyoa au kusuka,lakini nijuacho mimi wanawake hupenda kua na mwanaume anaejiamini ktk kutafuta na kumsimamie yeye mwenyewe,wameumbwa hvyo.akikuona upo kama mwanaume wa kweli haijalishi ametoka familia tajili atakukubali tu.acha uoga uoga
 
we kama unajijua masikini watoto wakishua unawafatilia ili iweje,nenda kwa masikini wenyako mtengeneye poverty cycle.walimu wa kibongo bana majanga

Si kwamba ninawatafuta mkuu, tunakutana tu kweny mangira mfano vyuoni na sehemu za kazi. Kwa mfano huyu wa sasa hiv tulisoma wote O level, nikapangiwa kazi wilayan kwao ndo tukaanza kukutana na hatimae ndo tukazungumzia haya masuala ya mapenzi
 
Jiamini kama mwanaume,amini kua unaweza kutafuta na ukasomesha watoto na mkawa na familia bora kama za kwao,unachotakiwa kufanya kama umekutana na mwanamke uwe muwazi juu familia yako fukara na kule utokako ili achague kunyoa au kusuka,lakini nijuacho mimi wanawake hupenda kua na mwanaume anaejiamini ktk kutafuta na kumsimamie yeye mwenyewe,wameumbwa hvyo.akikuona upo kama mwanaume wa kweli haijalishi ametoka familia tajili atakukubali tu.acha uoga uoga

Nashukuru sana G'tax
 
acha uoga wa maisha ticha...unataka kuoa mwanamke maskini ili wanao waje pata tabu kama ulizopata wewe?!
hata vitabu zinasema hoeni sehemu zilizo bora
 
swali nikuulize, we umesema umesomeshwa na watu mbalimbali na ujombani, je elimu yako imefika hadi ya chuo kikuu? na kwa sasa bado unakaa ujombani au unaishi kwako walau chumba kimoja? kifupi kuwa watu wengi hasa baba zetu wakisimulia njia walizopitia ktk kusomana kulelewa utasikitika sana ila mwishowa siku tunaangalia sasa ni nani, yupo kitengo gani, ana elimu gani na maisha gani. kama elimu yako imefika chuo kikuu basi jua unaendana nao achana na mawazo ya historia yako,
 
kijana wala usiogope kwanza Mungu anakupenda sana kukupa mwanamke ambaye kwao wana uwezo amekupunguzia majukumu fulani so unachotakiwa nkufanya ni kumtunza huyo mwanamke
 
Wassira anasema watanzania tuache ujanja mwingi ambao hauna maana coz historia inaonyesha wote tumetoka maporini tukaja mjini,brother unatatizo la kisaikolojia ambayo inakupa inferiority complex,japo mi sio mtaalam wa matatizo hayo ila ningekuwa karibu na wewe ningekujenga kuwa na postive altitude,nilipokuwa chuo kikuu kuna vijana walitaka kuacha chuo waludi kijijini kwa matatizo kama mikopo na kujiona hawana samani katika jamii,ufaulu wao ulikuwa dv 1.5,niliwafanyia counselling mpaka leo wapo vizuri,tuliopitia seminary huduma hizi ni sehemu ya maisha yetu.
 
Self-esteem yako mkuu iko low kabisa. Ujiamini mkuu.
 
Back
Top Bottom