David ngayanimo
Member
- Nov 8, 2018
- 23
- 27
FAMILIA YA MUZIKI TUUNGANE : MSANII G . POP WA CREW YA PLANET 2000 ANAHITAJI MSAADA WETU
Habari za wakati huu Ndugu, jamaa na Marafiki pia kwa heshima na taadhima kwa niaba ya Familia ya Ndugu JAMES KADUMA, napenda kuwataarifu kuwa Mwana Iringa mwenzetu JAMES KADUMA (G. POP) kutoka kundi la Muziki la PLANET 2000 CREW lenye Maskani yake Mkoani Iringa anaumwa sana na hali yake kiafya sio nzuri amelazwa Hospitalini Mkoani Njombe kwa matibabu zaidi.
Awali kabla ya kuanza kuugua James Kaduma (G.Pop) alikuwa akifanya kazi zake za kujitafutia kipato Kahama, Shinyanga na baada ya kuanza kuumwa na hali yake kiafya kubadilika alichukuliwa na Kaka yake aitwaye CHRIS anayeishi Mkoani Njombe kikazi kwa ajili ya matibabu zaidi.
James Kaduma (G.Pop) ni mmojawapo kati ya Wasanii watatu (3) waliokuwa wanaunda Kundi la PLANET 2000 CREW wakiwemo YAKUBU G. CHENGULA (YB) na FREDY EDWIN "Gwandumi" (FREDY E) na kundi hilo kufanikiwa kurekodi wimbo wa BAB KUBWA mnamo Mwaka 2000 chini ya Utayarishaji wa Producer PROFESSOR LUDIGO, kwenye Studio za MJ RECORDS Masaki, Jijini Dar Es Salaam na baada ya hapo kufanikiwa kutoa Album yenye jumla ya nyimbo kumi (10) zilizorekodiwa kwenye Studio nyingine tofauti.
Hivyo kwa unyenyekevu mkubwa nawaomba Ndugu zangu wote wana IRINGA LEGENDS tuendelee kumuombea kwa SALA na MAOMBI vilevile kwa yeyote atakayewiwa, tunaomba mchango wako kwa chochote ulichojaaliwa na Mwenyezi Mungu ili kuweza kuchangia gharama za matibabu ya Ndugu yetu.
Kwa mawasiliano zaidi au kuweza kuchangia unaweza kutuma kwa namba ya Mixx By Yas: 0655 579 299 Jina limesajiliwa YAKUBU GEORGE CHENGULA, Ahsanteni sana na Mungu awabarik....
Ukwaju wa kitambo
0767 542 202
Habari za wakati huu Ndugu, jamaa na Marafiki pia kwa heshima na taadhima kwa niaba ya Familia ya Ndugu JAMES KADUMA, napenda kuwataarifu kuwa Mwana Iringa mwenzetu JAMES KADUMA (G. POP) kutoka kundi la Muziki la PLANET 2000 CREW lenye Maskani yake Mkoani Iringa anaumwa sana na hali yake kiafya sio nzuri amelazwa Hospitalini Mkoani Njombe kwa matibabu zaidi.
Awali kabla ya kuanza kuugua James Kaduma (G.Pop) alikuwa akifanya kazi zake za kujitafutia kipato Kahama, Shinyanga na baada ya kuanza kuumwa na hali yake kiafya kubadilika alichukuliwa na Kaka yake aitwaye CHRIS anayeishi Mkoani Njombe kikazi kwa ajili ya matibabu zaidi.
James Kaduma (G.Pop) ni mmojawapo kati ya Wasanii watatu (3) waliokuwa wanaunda Kundi la PLANET 2000 CREW wakiwemo YAKUBU G. CHENGULA (YB) na FREDY EDWIN "Gwandumi" (FREDY E) na kundi hilo kufanikiwa kurekodi wimbo wa BAB KUBWA mnamo Mwaka 2000 chini ya Utayarishaji wa Producer PROFESSOR LUDIGO, kwenye Studio za MJ RECORDS Masaki, Jijini Dar Es Salaam na baada ya hapo kufanikiwa kutoa Album yenye jumla ya nyimbo kumi (10) zilizorekodiwa kwenye Studio nyingine tofauti.
Hivyo kwa unyenyekevu mkubwa nawaomba Ndugu zangu wote wana IRINGA LEGENDS tuendelee kumuombea kwa SALA na MAOMBI vilevile kwa yeyote atakayewiwa, tunaomba mchango wako kwa chochote ulichojaaliwa na Mwenyezi Mungu ili kuweza kuchangia gharama za matibabu ya Ndugu yetu.
Kwa mawasiliano zaidi au kuweza kuchangia unaweza kutuma kwa namba ya Mixx By Yas: 0655 579 299 Jina limesajiliwa YAKUBU GEORGE CHENGULA, Ahsanteni sana na Mungu awabarik....
Ukwaju wa kitambo
0767 542 202