Msaada: Kampuni ya Sunranch ni halali au ni utapeli mwingine?

Msaada: Kampuni ya Sunranch ni halali au ni utapeli mwingine?

Acha uongo. Anunue jana na apate jana?

Iko hivi: unanunua mnyama. Mfano - bata anauzwa sh 50000/=. Kinachofanyika utakuwa unalipwa sh 2000 kila siku kwa muda wa miezi 3. Siyo unalipwa yote 180,000/= utapewa kwa pamoja.

Unaweza kununua mnyama zaidi ya mmoja na malipo ni kwa kila mnyama.

Yuko padri mmoja msomi kanunua wanyama wenye thamani ya sh 6m. Analipwa sh 92,000/= kila siku. Nabatalipwa hivyo kwa miezi 6.

Utata ni je project itadumu kwa huo muda wote? Wewe unayefikiria kujiunga leo, utakula kama hawa wanaokula sasa hivi?

La kujifunza ni kuwa hii michezo yote inapoanza hulipa sana. Halafu network huanza kusumbua na kisha wahusika hupotea.

You may join for your own risk.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Aisee
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza wakuu.

Kuna kampuni hii ya mtandaoni inaitwa "Sunranch", hii ni kampuni ambayo unanunua mnyama mtandaoni na kuanza kupiga faida kila siku.

Kuna mtu ananishawishi nijiunge lakini moyo unasita.

Kama kuna mtu ambaye ameshashiriki ninaomba dodoso tafadhari.

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
Take risk, ukilizwa iwe Siri yako lakini
 
Ukiuliza kwa sasa hivi majibu ni lazima yatakuwa chanyatu, watu wanapiga hela.

Huu ni muda wa matangazo ya word of mouth

Baadaye ikija kufika juu mzunguko ukakua pesa ikaonekana au ikaanza kupungua yaani pale top. Hapo ndo utasikia, tutarejea hewani baada ya muda mfupi muwe na utulivu
Tayari wanalia watu
 
Kipanya hao ni wamakonde.. nawe ni CHAMAKI NCHANGA wataKUMEMENA 😂🤣

Siijui hiyo kampuni ila kwa maelezo yako tu, hapo vilio vitaibuka mida si mrefu, hao ni wale wale kina mr. Kuku
Asee km.ulijua tu
.tumepigwa
 
Back
Top Bottom