Mzee wenzako wanatangaza ndoa kila kunapokucha, wewe unaulizia format ya talaka? Pole sana mkuu! Bila shaka yamekukuta. Raha au ugumu wa ndoa ni hadi hapo utakapoiingia. Mwamuzi wa mwisho ni wewe. Hawa wengine watakushauri, watawapatanisha lakini cha moto unakipata peke yako wao wakiwa hawapo. So pakifika mahali ambapo hapavumiliki, bora tu kuwa huru.
Kiujumla talaka haina regular format. Kuna watu wanaandika misitari miwili tu ya kwamba kuanzia leo sikutambui kama mke wangu. Mwingine anaandika kwa kurefer cheti cha ndoa, kwa hiyo anaanza kuandika kwa kuelezea kwamba mimi.... navunja ndoa iliyofungwa tar... kwa kutoa talaka tar... kwamba ... kutokana na.... nk nk. Lakini kuna wengine wanaamua kuiandika kisheria. Kwa hiyo unaweza kumtafuta mwanasheria akakuandikia kwa kufuata sheria za talaka. Lakini katika hali zote inategemea zaidi wewe ni mtu wa kariba gani.
Mwisho, kabla hujaamua kutoa talaka, mpe kwanza last warning. Kama ni tabia ya kawaida naamini atajirekebisha, labda kama ni uzinzi, huko siwezi kushauri lolote, maana machungu ya kumegewa bila shaka unayajua mwenyewe. Ila kama ni haya mengine jaribu ushauri wa biblia. Mshauri wewe peke yako, asipokusikia waite wazee wamshauri, asipowasikia lishirikishe kanisa, na kama hatalisikia hata kanisa, basi muache aende kwa amani.