Msaada: Jiko la gesi hutoa moshi mwingi kuchafua sufuria

Msaada: Jiko la gesi hutoa moshi mwingi kuchafua sufuria

Nami msaada jamani, jiko langu la plate mbili, plate moja inavuja gas, nimeshindwa hata kulitumia linatengenezeka au ndio la kutupa ninunue lingine
Polee. Nenda kwa fundi wanaochomelea vikaango kwa kutumia lead. Kuna ile chuma inayeyushwa alafu wanaziba pipe iliyotoboka. Au peleka kwa wale mafundi wanaotengeneza friji, kwa kuwa wana uwezo wa kuchomelea sehemu inayovuja. Ikishindikana kabisa, nichek nikuhonge 😛 jiko jingine...
 
  • Thanks
Reactions: ram
Polee. Nenda kwa fundi wanaochomelea vikaango kwa kutumia lead. Kuna ile chuma inayeyushwa alafu wanaziba pipe iliyotoboka. Au peleka kwa wale mafundi wanaotengeneza friji, kwa kuwa wana uwezo wa kuchomelea sehemu inayovuja. Ikishindikana kabisa, nichek nikuhonge 😛 jiko jingine...

Ahahahaahhh...kuliko kuhangaika huko kote si bora tu nikucheki unihonge hilo jiko jipya😀😀, BTW ahsante sana nitamtafuta fundi friji
 
Wanajamii forum habari za muda huu!

Jiko langu la gas linatoa masizi"produce soots" kwa nini kwani lina mwaka lakini Leo ndo linafanya hivi ni kwa nini?

Msaada tafadhali nifanyeje?

kifinko au kizbo cha jiko lako kinacho kua na vitundu kwa ajili ya kutolea ge au moto ,kime achi yani kipo loose,utafute wachomeleaji kwani mara nyingi vinakua vya shaba kama ckose kichomelewe kutumia moyo wa gesi
 
Fungua ndani ya hilo jiko pale kwenye gas burner kuna kitu kama nut(nuti) inayopitisha gas kupeleka pale penye kichwa chenye vitundu vingi patakuwa na uchafu.
Hiyo nut iliyo ktk burner ina tundu moja dogo sana linalopitisha gas kama jet. Hilo tundu hata sindano haipiti. Ondoa uchafu wote hiyo sehemu
Tafuta waya mwembamba kama wa extension cable mbovu au pasi mbovu chuna chukua kiwaya kimoja toboa vizuri hilo tundu kuzibua uchafu.

Hakikisha unafungulia gas kwa wastani, ukifungulia sana au hadi mwisho huku kikiwa na uchafu kwenye baadhi ya matundu husababisha moto wa njano ambao huleta masizi meusi. rekebisha utoke moto wa blue tu.
ANGALIZO: Usiongeze upana wa hilo tundu kwa namna yeyote vile.

Ukifanikiwa lete mrejesho hapa wafaidike na wengine. Mimi nilifanikiwa kwa hatua hizo hapo juu.
 
Hii inaashiria kama wewe ni mwanaume OA,kama ni mwanamke OLEWA!
 
Hapo tatizo ni fuel to air ratio na sio uchafu wa gesi au nini sijui! Chungulia chini ya jiko lako utakuta vijibati vya kuziba au kuachia hewa inayo ingia kwenye vijitundu vinavyo ingiza hewa kabla ya mchanganyiko wa hewa na gesi haujaingia kwenye bunners, cha kufanya pale washa jiko lako, alafu adjust vijibati hivyo slowly huku ukiangalia rangi ya flame/moto kwenye burner endelea ku-adjust mpaka moto uonekane totally blue, ukiona moto umechanganyika wa bluu na majano basi endelea kurekebisha.

Adjustment/vibati hivyo vipo chini za duct ya chuma inayoingiza gesi kwenye burner kila bunner ina adjustment moja - kazi ya vibati hivyo ni kurekebisha hewa inayo changanyika na gesi kabla haijafika kwenye bunner, hewa ikingia ndogo rangi ya flame inakuwa yellowish kama ya kibatali na kutoa moshi mweusi/masizi - hewa ikingia ya kutosha basi rangi ya flame inakuwa blue (i.e complete combustion) ukifanikiwa ku-adjust vijibati hivyo hutaona tena masizi. Goodluck.
Aisee! Umeokoa pesa yangu kuliwa. Kuna fundi nimemfatilia aje anirekebishie tatizo hili karinga balaa. Kumbe maujanja yako JF! Nimerekebisha mwenyewe hadi nimesifiwa kuwa ni mtaalamu! Ubarikiwe!
 
Aisee! Umeokoa pesa yangu kuliwa. Kuna fundi nimemfatilia aje anirekebishie tatizo hili karinga balaa. Kumbe maujanja yako JF! Nimerekebisha mwenyewe hadi nimesifiwa kuwa ni mtaalamu! Ubarikiwe!
Hapo wifi anasema
Baba fulani nakupendaga tu unajua kila kitu
 
Tatizo ni burner na sio kitu kingine. Tafuta hata used kama ukishindwa kuirekebisha.

Nliwahi nunua jiko kigamboni ikawa hivyo, nikarudi na jamaa zangu wawili muuza duka anasema aniuzie nyingine...

Wakati tunaendelea kubishana vijana wangu wa kazi wanaendelea kubadilisha burner. Kwny majiko mengine.... Tatizo likaisha kabisa
 
Asanteni wadau, hii mada imenisaidia maana nilikuwa kila nikitoa kitu sufuria linakuwa jeusi, macho yanawasha na mafua kwa mbali.

Baada ya kusoma hii nimerekebisha na sasa hivi nakunywa Alkasusu niliyopika mwenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu nina gas ya Oryx mtungi mdogo! sasa cha ajabu linatoa moshi kama napikia kuni....nimejaribu kubalance moto nimeshindwa!!

Msaada wenu, natakiwa kufanya nini ili nipate non-luminous flame?
 
Achana na huo moshi pikia moto.
Wakuu nina gas ya Oryx mtungi mdogo! sasa cha ajabu linatoa moshi kama napikia kuni....nimejaribu kubalance moto nimeshindwa!!

Msaada wenu, natakiwa kufanya nini ili nipate non-luminous flame?
 
Na kama jiko ukute upande mmoja haliwaki kabisa sometimes linawaka nafanyaje ,
 
Asante sana mkuu. Ndiyo nimetoka kulisafisha sasahivi. Yaani umeelezea kiutaalamu na nimekuelewa mia kwa mia. Hivyo vibati vya ku-adjust nimeviona ila sikujua kazi yake ni nini. Nilikuwa nime-focus kwenye kusafisha burner na duct za gesi kama walivyonishauri wadau wengi. Nilivifungua hivyo vibati ili nipate upenyo wa kusafisha duct. Then nikavirudishia, nikawasha jiko lakini sikuona changes zozote baada ya usafi. Hivi sasa ninajua chanzo cha tatizo langu na jinsi ya kutatua hilo tatizo. Asante sana mkuu. Watu wengi watafaidika na mchango wako kwani tatizo hili linawakumba wengi tu.
Hata Mimi nimefaidika sana, asanteni sana sana!
 
Hapo tatizo ni fuel to air ratio na sio uchafu wa gesi au nini sijui! Chungulia chini ya jiko lako utakuta vijibati vya kuziba au kuachia hewa inayo ingia kwenye vijitundu vinavyo ingiza hewa kabla ya mchanganyiko wa hewa na gesi haujaingia kwenye bunners, cha kufanya pale washa jiko lako, alafu adjust vijibati hivyo slowly huku ukiangalia rangi ya flame/moto kwenye burner endelea ku-adjust mpaka moto uonekane totally blue, ukiona moto umechanganyika wa bluu na majano basi endelea kurekebisha.

Adjustment/vibati hivyo vipo chini za duct ya chuma inayoingiza gesi kwenye burner kila bunner ina adjustment moja - kazi ya vibati hivyo ni kurekebisha hewa inayo changanyika na gesi kabla haijafika kwenye bunner, hewa ikingia ndogo rangi ya flame inakuwa yellowish kama ya kibatali na kutoa moshi mweusi/masizi - hewa ikingia ya kutosha basi rangi ya flame inakuwa blue (i.e complete combustion) ukifanikiwa ku-adjust vijibati hivyo hutaona tena masizi. Goodluck.
Aiseee nimehangaika sana katika pitapita zangu huku JF leo hii tar 12-05-2022 na mimi nimesaidika kupitia comment yako… asante sana, MUNGU akubariki
 
Back
Top Bottom