Kayoka
JF-Expert Member
- Jun 21, 2011
- 2,239
- 1,884
Habari Madaktari na wanadau wengine huku ndani.
Kama wahenge wasemavyo "Mficha maradhi Kifo Humuumbua" nipo njiani narudi tena hospital kuonana na daktari kufanya uchunguzi na kupata matibabu lakini ningependa kuwashirikisha na naomba msaada wenu juu ya tatizo langu.
Siku ya Jumapili nilianza kuoana dalili ambazo si za kawaida kwenye dhakari (uume) wangu kama vile maumivu makali wakati wa kukojoa, kukojoa mara kwa mara, kuwasha kwenye kichwa na kujitotokeza vipele vidogo vidogo mithili ya kama vile mba mweusi pia mwili mzima ukiwa na joto, na kuumwa kichwa.
Nikaenda hospital na kupima (mkojo na choo nikaambiwa hakuna shida), BS nikaambiwa malari wadudu wanne nikapewa dawa (Malafin & Diclofenac) na kuanza kuzitumia, nashukuru Mungu nimepata afueni na naendelea vizuri.
Lakini sasa ile hali ya kwenye dhakari kuwa na vipele na baka jeusi bado imezidi kusambaa huku nikipata maamivu, sasa naomba msaada wenu wataalamu niweze kujua taizo hili na namna ya kupata matibabu yake na nini naweza kumueleza daktari kwa uchubguzi zaidi.
Status yangu "NAISHI NA MKE"
Kama wahenge wasemavyo "Mficha maradhi Kifo Humuumbua" nipo njiani narudi tena hospital kuonana na daktari kufanya uchunguzi na kupata matibabu lakini ningependa kuwashirikisha na naomba msaada wenu juu ya tatizo langu.
Siku ya Jumapili nilianza kuoana dalili ambazo si za kawaida kwenye dhakari (uume) wangu kama vile maumivu makali wakati wa kukojoa, kukojoa mara kwa mara, kuwasha kwenye kichwa na kujitotokeza vipele vidogo vidogo mithili ya kama vile mba mweusi pia mwili mzima ukiwa na joto, na kuumwa kichwa.
Nikaenda hospital na kupima (mkojo na choo nikaambiwa hakuna shida), BS nikaambiwa malari wadudu wanne nikapewa dawa (Malafin & Diclofenac) na kuanza kuzitumia, nashukuru Mungu nimepata afueni na naendelea vizuri.
Lakini sasa ile hali ya kwenye dhakari kuwa na vipele na baka jeusi bado imezidi kusambaa huku nikipata maamivu, sasa naomba msaada wenu wataalamu niweze kujua taizo hili na namna ya kupata matibabu yake na nini naweza kumueleza daktari kwa uchubguzi zaidi.
Status yangu "NAISHI NA MKE"