everlenk
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 11,628
- 15,037
Nataka nimchukue ndugu au rafiki yangu mmoja nimhadithie hii issue, pili nichunguze wanakaa wapi hawa watu sna nimuonyeshe huyo ndugu yangu, Kisha ndio nifikirie kama naweza kukutana na huyu mdada huku jamaa yangu akiwa anafuatilia kimya kimya.
Ndugu yangu Shark huko kote kwanini kuzunguka hivyo na kujipa makazi mengi yasiyo na maana, wewe ni kidume baba mface mwanaume mwenzio muulize mweke mtu Kati akupe yake kisha temana nao na mizigo yao wape waambie wewe si wa kihivyo wakuchukulie poa tu, na mpe warning hizo biashara na wewe waziache kabisa la sivyo.....malizia mwenyewe.
Pili uje umshirikishe ndugu au Rafiki yako wakati wewe kama wewe ushachukua hatua, na huko mahali anakokupea vitu vyake kama ni sehemu ya Kula unaweza badilisha kama mbadala upo ukawa unaenda sehemu nyingine hapa ni kiusalama zaidi.
Hata kama hitaji ni mtoto Ina maana miaka yote hiyo huyo mwanamke alikuwa anakungoja wewe tu? Kashindwa vipi kuchepuka huko kwingine kote azingoje sperm zako tu na kazijuaje zako ndizo zenye mtoto,na anamshirikisha mumewe, Wacha kabisa upumbavu huu peleka huko.
Siku hizi baba hela inatafutwa kwa udi na uvumba, poteza hela pata hela, kama si ushirikina basi ni dili la pesa mzee, na kama ndo unakijiuwezo chako na wanajua hapo job uko sekta nzuri ya mpunga na wana uhakika na salary yako nenda huko kakutane na huyo mwanamke ushushiwe jumba bovu la fumanizi, utafilisiwa hadi boxa uliyovaa,heshima yako yote kushney , hiyo case ya fumanizi ndo itakuwa fimbo ya kukuchapia kila wanachohitaji kutoka kwako wapate ili wewe ulinde tu heshima yako.
Haya ni baadhi tu yapo mambo mengi yanayoweza kuwa suspected. Stuka baba stukaaaa!!! Hii ni dunia, mjini shule......
Last edited by a moderator: