Msaada: Hawa mtu na mkewe siwaelewi kabisa

Msaada: Hawa mtu na mkewe siwaelewi kabisa

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,973
Reaction score
30,154
Wadau,

Kuna Jamaa mmoja tunafanya kazi ofisi za karibu hapa Town hivyo sometimes tunakutana Lunch hour kwenye menu jirani na tunapofanyia kazi, na bahati nzuri zaidi Mke wa huyu jamaa alikua class mate wangu wa primary ila hatukua na mazoea kivile kipindi hicho. Jamaa hatujazoeana kihivyo ila tunajuana tu kwa sura na ofisi tunazofanyia kazi.

Kama miezi miwili nyuma ofisini kwa huyu jamaa kulikua na family day ambapo ndugu wa staff wa ofisi yao walikua wanakutana ofisini kisha wanaenda wenyewe kuspend wanakokujua ndio nikabahatika kumuona mkewe huyu jamaa tukasalimiana na mkewe, na tukatambulishana na jamaa pia mambo yakawa poa.

Issue ilikuja kua baada ya siku chache after ile shughuli yao, yule jamaa akawa ananitafuta, kuonana akanipa namba ya mkewe kwamba ananitafuta. Mi kumpigia mkewe akadai kua alikua ananizimikia toka primary na anashukuru sana ameniona. Anataka japo tuwe wapenzi a.k.a michepuko tu. Kusema ukweli sikutaka kumsikiliza nikakata ile simu na nikawa sipokei tena simu yake. Next day yule jamaa (mumewe) akanifuata ofisini kuniambia Mkewe analalamika kwanini nilimkatia simu jana yake.

Baada ya kama wiki hivi yuleyule mumewe akanipa na bahasha imepigwa stapler, kuifungua ni ujumbe kutoka kwa mkewe kua ananipenda sana na anataka tuwe wapenzi. Kaweka na $70.00 pamoja na siku + direction ya kukutana mahali nikifika nilipie chumba tufanye yetu. Yaani ujumbe huu umepitia kwa mumewe!!!!!!!!!!!!!!. Nilishangaa sana nikasema huu mtego ama vipi. Jioni yake nikapata msg kutoka kwa mkewe kuulizia kama nilipata ujumbe kupitia kwa mumewe, nikamjibu kua niliupata ila nitampa jibu.

Kesho yake wakati niko lunch nakula, mume wa yula ex-mate akaja kuniuliza kua why simjibu mkewe mpaka ye anasumbuliwa kila mara kunitafuta. Nilitaka nimuulize kama anajua kitu kinachozungumziwa ama lah ila nikasita. Nilimjibu tu kua nafuatilia nitamjibu mkewe nilipofikia. Nikamuuliza mkewe kwanin anawasiliana na mimi issue za kuchepuka kupitia mumewe? anamchukulia vipi mumewe? Ni ----- ama vipi.

Sasa jana nimepewa appointment kua wikiend hii tukutane hoteli fulani hivi, ujumbe umekuja kupitia kwa yuleyule mumewe lakini kupitia bahasha, na safari hii ameweka $100.00 na Tshs 50,000/= ya hoteli na Taxi. Tena Mumewe kasisitiza niharakishe hii issue (anaijua???) iishe mapema maana yeye amechoka kusumbuliwa. Nimeshindwa kuwaelewa hawa Mtu na Mkewe, sielewi huyu jamaa ni ----- kihivyo au kuna mipango inaendelea nyuma ya pazia. Wadau naombeni ushauri wenu, niko njia panda!!
 
Dah,mkuu achana nae,hizo jumbe anazokutumia pamoja na pesa zitunze,we endelea kumkwepa mpaka uone mwisho wake.
 
duuuuh!!!!
mkuu ngoja kwanza nitarudi tena hili zito sio la kukurupuka..!!!!
 
Ungeuliza kuwa wana watoto?
nilishawahi kuweka kisa humu cha Ujerumani zamani
kuna alimlipa tu atembee na mkewe ili wapate watoto
kumbe alielipwa nae hawezi pia...na yeye kabambikiwa watoto na mkewe
walienda hadi mahakamani
 
Could be a sperm trap, or a manaja twa. I'd breeze past, real fast, if I were you, Chief. Unless, it's just another story.
 
Mh! Hizo pesa na bahasha zikusanye kama zilivo kuja alafu mkionana na mmewe lunch mwambie naomba tuonane weekend sehem flan then na mkewe vile vile mtaarifu kwa sms mkutane eneo moja na mmewe ila usmtaarifu kama mmewe atakuwepo,
wakishafika ndio mda wa kuwaambia kuwa hupendi ujinga na pesa zao wakabidh ikiwezekana nenda na yf wako au grlfrnd uwatambulishe.
 
Ungeuliza kuwa wana watoto?
nilishawahi kuweka kisa humu cha Ujerumani zamani
kuna alimlipa tu atembee na mkewe ili wapate watoto
kumbe alielipwa nae hawezi pia...na yeye kabambikiwa watoto na mkewe
walienda hadi mahakamani
Mkuu kuhusu mtoto sijauliza. Ila siwaelewi hasa huyu jamaa. Saa zingine nikikutana nae lunch hua namkwepa nachukua take away. Nabaki najiuliza hivi haya mambo ni kweli ama naota. Nilifikiri kama hana uwezo wa kumpa mkewe mimba basi siko tayari kupoteza damu yangu bure
 
Mkuu kuhusu mtoto sijauliza. Ila siwaelewi hasa huyu jamaa. Saa zingine nikikutana nae lunch hua namkwepa nachukua take away. Nabaki najiuliza hivi haya mambo ni kweli ama naota. Nilifikiri kama hana uwezo wa kumpa mkewe mimba basi siko tayari kupoteza damu yangu bure

Kama sio mimba basi ni ushirikina
wamesha kutazama kishirikina wameona 'kitu'
cc mshana jr MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
Tugawane hiyo dola mia nipe 50, mi nakuja nawanangu wawili tunakuwekea ulinzi mkali hata wa obama cha mtoto ukamgegede huyo dem,na mme wake akija kuleta soo tunamgegeda sisi sawa?
Naweza nikakutana nae hapo na tukabadili kiwanja na simu ya mkewe nikaificha. Ila je ni kweli wako njama moja na mumewe? Au ye hajui anageukwa?
 
Jiongeze kidogo, muulize mumewe anajua nini mkewe anachofuatilia? Then msikie jibu lake halafu utajua cha kufanya. Pengine wamepanga wote kuna tatizo ndani yao. Vipi wamejaliwa kupata watoto?
 
Naweza nikakutana nae hapo na tukabadili kiwanja na simu ya mkewe nikaificha. Ila je ni kweli wako njama moja na mumewe? Au ye hajui anageukwa?

Acha maswali Mengi fuata maelekezo, si anataka kugegedwa na ushaidi unao unaogopa nini ?na bado mimi nipo kukupa ulinzi.
 
Shemeji acha tamaa, utaliwa mchana kweupe achana nao na bahasha usipokee...

Sio kwamba mumewe ni Mume-bweg.e au anamuamini sana mkewe? Au nae ananiona mimi ndio bweg.e karibia naingia mkenge? Nimefikiria nimuulize huyu jamaa kama anaaelewa tunachozungushana na mkewe muda wote lakini roho inasita.
 
Back
Top Bottom