Msaada: Anayeweza kuniunganisha na masoko ya mbao DSM bila dalali

Mapand

Senior Member
Nov 9, 2022
134
202
Habari wakuu!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Mimi ni kijana wa miaka 25, naishi Mafinga-Iringa (na ndiyo nyumbani) nilipozaliwa.

Sasa baada ya kuhitimu chuo miaka miwili iliyopita na katika kuendelea kufikiria namna ya kupata mtaji wa kufungua biashara yoyote yenye kunifanya nikaendesha maisha na yasinisumbue sana hata baada ya kuoa, bahati nzuri ndugu yangu mmoja aliniamini akanihitaji nisimamie biashara zake na ninashukuru Mungu niliweza kusimamia biashara.

Mpaka naondoka kwenye usimamizi wa hizo biashara mwezi uliyoisha juzi, palikuwa na maendeleo makubwa ya kukua kwa biashara pamoja na kuongezeka kwa wateja kwa wastani wa asilimia hata sabani ukilinganisha na mtangulizi wangu aliyekuwepo kabla yangu, japo naye hakufanya vibaya sana.

Sasa katika kutafuta fursa za kibiashara hapa mkoani kwetu (Iringa) nikaona biashara ambayo naweza kuifanya na ninaipenda ni ya timber production (uzalishaji wa mbao).

Kusema ukweli kwa hapa Mafinga kuna masoko mengi sana ya mbao na wanunuaji wanalipa cash bila usumbufu wowote.

Lakini tatizo la hawa wanunuzi wa mbao (Wachaga) nakiri kabisa ndiyo waliyoharibu bei za mbao kwenye masoko ya hapa kwetu kwasababu pesa wanazonunulia ni ndogo sana ukilinganisha na ugumu wa kazi yenyewe.

kwasababu ninayezalisha mbao kumbuka nanunua mti kama ulivyosimama na kumbuka katika shamba utakuta karibu kila mti unauzwa bei yake, sasa hasara huja pale kama hukufix vizuri bei ya kila mti kulingana na size ya mbao itakayozalishwa kwenye mti husika.

Sasa kutokana na changamoto ya bei ya kuuzia mbao kwa hapa nyumbani (Mafinga) nikafikiria kupeleka mwenyewe kwenye masoko makubwa yaliyopo Dar es Salaam, kutokana na bei zao kuwa nzuri kidogo kwasababu kwa masoko ya mbao hasa pale Buguruni bei niliona ziko juu sana ukilinganisha na bei ya huku kwetu, hata kama kuna transport costs na gharama zingine za ushuru serikalini.

Tatizo kubwa lililopo Dar ni madalali, tena bora wawe waaminifu, lakini hawa watu ni wahuni kiujumla na ninaweza kuwaita suyo madalali tena kwasababu udalali ni kazi halali na inatambulika na serikali.

Nasema madalali wa Buguruni ni wahuni na matapeli kwasababu kuna ndugu yangu alishawahi kupeleka mzigo wa mbao pale na akatapeliwa mpaka leo huwa anaziba maskio kabisa kupeleka mzigo Dar es Salaam hata kama siyo Buguruni tu.

Baada ya kujieleza kwa urefu zaidi, naomba kama kuna mtu yeyote anayeweza kuniunganisha na mfanyabiashara wa mbao (anayenunua kwa jumla) ili tufanye biashara kwasababu kikubwa ni uaminifu tu.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.
 
Mkuu, sina hoja inayoendana na swali lako ila ningeomba kukuuliza swali. Kule mafinga ninaweza kupata miti ya cypress kwa wingi?
 
Sasa humu pia ndo Nyumbani kwa Mataperi!

Na kama hutaki Dalali kwenye deals zako, basi usihangaike kutaka connection straight kwa Buyer, coz Buyers pia hawahangaikagi na Srangers Seller kwa deal kubwa kwa kukutana Mtandaoni!

Hutaki Dalali funga Safari mwenyewe nenda Dar mwenyewe katafute Buyer, na sio issue ya siku moja kukutana na Buyer, unaweza kukutana na Watu wa kati pia, hawakwepeki, labda utumie muda wako kujua Buyer ni yupi na yupi ni mtu wa kati!!!
 
Sasa humu pia ndo Nyumbani kwa Mataperi!

Na kama hutaki Dalali kwenye deals zako, basi usihangaike kutaka connection straight kwa Buyer, coz Buyers pia hawahangaikagi na Srangers Seller kwa deal kubwa kwa kukutana Mtandaoni!

Hutaki Dalali funga Safari mwenyewe nenda Dar mwenyewe katafute Buyer, na sio issue ya siku moja kukutana na Buyer, unaweza kukutana na Watu wa kati pia, hawakwepeki, labda utumie muda wako kujua Buyer ni yupi na yupi ni mtu wa kati!!!
Mtoa mada fuata ushauri huu
 
Sasa humu pia ndo Nyumbani kwa Mataperi!

Na kama hutaki Dalali kwenye deals zako, basi usihangaike kutaka connection straight kwa Buyer, coz Buyers pia hawahangaikagi na Srangers Seller kwa deal kubwa kwa kukutana Mtandaoni!

Hutaki Dalali funga Safari mwenyewe nenda Dar mwenyewe katafute Buyer, na sio issue ya siku moja kukutana na Buyer, unaweza kukutana na Watu wa kati pia, hawakwepeki, labda utumie muda wako kujua Buyer ni yupi na yupi ni mtu wa kati!!!
Asilimia 80 ya wakazi wa dar ni au Wana asili ya kautapeli mkuu fwata huu ushauri nenda buguruni dadisi kwanza uwajue matajiri direct vinginevyo kupigwa ni 80+%
 
Asilimia 80 ya wakazi wa dar ni au Wana asili ya kautapeli mkuu fwata huu ushauri nenda buguruni dadisi kwanza uwajue matajiri direct vinginevyo kupigwa ni 80+%
Si kweli Mkuu, Mataperi wapo kila sehemu, hata Mikoani ni wengi sana, sema Madalali wengi wa Dar sio Waaminifu, Utaperi ni Fani Mkuu.

Na watu wengi wa Mikoani ni rahisi kutapeliwa kwa sababu ya Tamaa ama Ubinafsi, wakishatapeliwa lawama zote kwa Wakazi wa Dar!

Ni Vile tu mtoa mada hajataka mtu wa kati, ningemuunganisha na soko la Tegeta, Tegeta kuna Soko zuri la Mbao, na Buyers ni really, soko ni kubwa na wanaenda kununua wenyewe Mbao Iringa, wako Buyers wakubwa wanaleta Malori yao wenyewe, pia wapo Buyer wadogo wanachangishana watu kadhaa wanaenda kuleta mzigo!

Sasa kama seller anaweza kuleta mzigo mwenyewe anauza tu Cash na Chap kwa haraka!
 
Tafuta na masoko ya nje kama Zanzibar na Comoro. Funga safari uende uonane na wanunuzi wa jumla ukiwa muaminifu utafanya nao kazi
 
Mkuu , sina hoja inayoendana na swali lako ila ningeomba kukuuliza swali...kule mafinga ninaweza kupata miti ya cypress kwa wingi?
Kwa uzoefu kidogo nilio nao wa Mufindi, cyprus ni miti adimu mno, shamba kubwa lipo karibu na kijiji cha Nundu ni la SAO HILL. Watu binafsi hawaoteshi Cyprus, hata ukiiona sehemu, basi ni ya taasisi kama makanisa au shule au familia bora.

Kwa kuokoteza nenda kijiji cha Ng`ang`ange wilaya ya Kilolo Iringa karibu na Boma Ng`ombe, waweza pata miti miwili mitatu hivi.
 
Lakini tatizo la hawa wanunuzi wa mbao (Wachaga) nakiri kabisa ndiyo waliyoharibu bei za mbao kwenye masoko ya hapa kwetu kwasababu pesa wanazonunulia ni ndogo sana ukilinganisha na ugumu wa kazi yenyewe.

kwasababu ninayezalisha mbao kumbuka nanunua mti kama ulivyosimama na kumbuka katika shamba utakuta karibu kila mti unauzwa bei yake, sasa hasara huja pale kama hukufix vizuri bei ya kila mti kulingana na size ya mbao itakayozalishwa kwenye mti husika.

Kaka usiwasingizie WACHAGA, Naomba nikupe ushauri

kuna kitu kinaitwa SAWING (hapa utakuta una plain sawing and Quater sawing ndizo kuu) hiyo plain sawing ndio njia ya ukataji ambayo inapunguza waste kabisa.

sasa mnaweka gogo kwenye mashine unakuja kulaumu Wachaga, kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake.

hizi ndio njia kuu za kuchana mbao kulingana na mti, Usikate mbao kama unakata nyama buchani hutapata faida.
 
Kaka usiwasingizie WACHAGA, Naomba nikupe ushauri

kuna kitu kinaitwa SAWING (hapa utakuta una plain sawing and Quater sawing ndizo kuu) hiyo plain sawing ndio njia ya ukataji ambayo inapunguza waste kabisa.

sasa mnaweka gogo kwenye mashine unakuja kulaumu Wachaga, kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake.

hizi ndio njia kuu za kuchana mbao kulingana na mti, Usikate mbao kama unakata nyama buchani hutapata faida.
Nadhani hata hujaelew kwanini nimetaja hao watu,hata sijui kuna namna ipi kati ya hizo ulizonitajia unaweza kutoa ubao wenye vipimo vyake bila kutakiwa kutoa hizo wastes
 
Nadhani hata hujaelew kwanini nimetaja hao watu,hata sijui kuna namna ipi kati ya hizo ulizonitajia unaweza kutoa ubao wenye vipimo vyake bila kutakiwa kutoa hizo wastes

Nadhani ungeuliza vizuri uelezwe ni jinsi gani inafanyika, nyie mmejifungia misituni mkiamini mbao mnavuna wenyewe tu dunia hii, wenzako wanakata mbao kwa kujua gogo hili wakate njia gani.
 
Sasa humu pia ndo Nyumbani kwa Mataperi!

Na kama hutaki Dalali kwenye deals zako, basi usihangaike kutaka connection straight kwa Buyer, coz Buyers pia hawahangaikagi na Srangers Seller kwa deal kubwa kwa kukutana Mtandaoni!

Hutaki Dalali funga Safari mwenyewe nenda Dar mwenyewe katafute Buyer, na sio issue ya siku moja kukutana na Buyer, unaweza kukutana na Watu wa kati pia, hawakwepeki, labda utumie muda wako kujua Buyer ni yupi na yupi ni mtu wa kati!!!
Kwani hao mtu kati waliwakuaje buyers, wamejazana mpaka pale karume mtumbani.wengi kushinda wanunuzi na wafanyabiashara kwa umoja wao.
 
Nifwate inbox tuyajenge nikusaidie mi nimzoefu wa hayo mambo
Habari wakuu!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Mimi ni kijana wa miaka 25, naishi Mafinga-Iringa (na ndiyo nyumbani) nilipozaliwa.

Sasa baada ya kuhitimu chuo miaka miwili iliyopita na katika kuendelea kufikiria namna ya kupata mtaji wa kufungua biashara yoyote yenye kunifanya nikaendesha maisha na yasinisumbue sana hata baada ya kuoa, bahati nzuri ndugu yangu mmoja aliniamini akanihitaji nisimamie biashara zake na ninashukuru Mungu niliweza kusimamia biashara.

Mpaka naondoka kwenye usimamizi wa hizo biashara mwezi uliyoisha juzi, palikuwa na maendeleo makubwa ya kukua kwa biashara pamoja na kuongezeka kwa wateja kwa wastani wa asilimia hata sabani ukilinganisha na mtangulizi wangu aliyekuwepo kabla yangu, japo naye hakufanya vibaya sana.

Sasa katika kutafuta fursa za kibiashara hapa mkoani kwetu (Iringa) nikaona biashara ambayo naweza kuifanya na ninaipenda ni ya timber production (uzalishaji wa mbao).

Kusema ukweli kwa hapa Mafinga kuna masoko mengi sana ya mbao na wanunuaji wanalipa cash bila usumbufu wowote.

Lakini tatizo la hawa wanunuzi wa mbao (Wachaga) nakiri kabisa ndiyo waliyoharibu bei za mbao kwenye masoko ya hapa kwetu kwasababu pesa wanazonunulia ni ndogo sana ukilinganisha na ugumu wa kazi yenyewe.

kwasababu ninayezalisha mbao kumbuka nanunua mti kama ulivyosimama na kumbuka katika shamba utakuta karibu kila mti unauzwa bei yake, sasa hasara huja pale kama hukufix vizuri bei ya kila mti kulingana na size ya mbao itakayozalishwa kwenye mti husika.

Sasa kutokana na changamoto ya bei ya kuuzia mbao kwa hapa nyumbani (Mafinga) nikafikiria kupeleka mwenyewe kwenye masoko makubwa yaliyopo Dar es Salaam, kutokana na bei zao kuwa nzuri kidogo kwasababu kwa masoko ya mbao hasa pale Buguruni bei niliona ziko juu sana ukilinganisha na bei ya huku kwetu, hata kama kuna transport costs na gharama zingine za ushuru serikalini.

Tatizo kubwa lililopo Dar ni madalali, tena bora wawe waaminifu, lakini hawa watu ni wahuni kiujumla na ninaweza kuwaita suyo madalali tena kwasababu udalali ni kazi halali na inatambulika na serikali.

Nasema madalali wa Buguruni ni wahuni na matapeli kwasababu kuna ndugu yangu alishawahi kupeleka mzigo wa mbao pale na akatapeliwa mpaka leo huwa anaziba maskio kabisa kupeleka mzigo Dar es Salaam hata kama siyo Buguruni tu.

Baada ya kujieleza kwa urefu zaidi, naomba kama kuna mtu yeyote anayeweza kuniunganisha na mfanyabiashara wa mbao (anayenunua kwa jumla) ili tufanye biashara kwasababu kikubwa ni uaminifu tu.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.
 
Back
Top Bottom