Mrithi wa REGIA ni Cecilia Paresso

Mrithi wa REGIA ni Cecilia Paresso

Uzuri wa magamba ni kwamba wanaleta tu changamoto. Leo wakimteua mgombea urais aliyetoka kaskazini, watageuka wote na kusema hakuwai kutoka rais kaskazini. Lakini ikiwa ni cdm watasema ni ukanda! You'll take my word siku atakapoteuliwa Lowasa na chama chao! Hao wanaojiita Rejao, ms, FF, hakuna atakayezungumzia ukaskazini na kusini tena!

Tuwaache tu maana chama chao kimepoteza mwelekeo na wasiposema propaganda kama hizo, watasema nini sasa? Wakae kimya!?
 
Mbona watu mnajadili kiu-CCM? Kumbukeni kwamba jukumu la kumteua mbunge sio la chama bali ni tume ya taifa ya uchaguzi. Chama kinapendekeza majina na wasifu wao halafu tume inapitia na kuteua halafu inarudisha tena majina kwenye chama na chama kinaridhia. Kwenye uchaguzi wa 2010, CDM walipendekeza majina 28, tume ikateua 25 wakabaki kwenye list 3. Kwahiyo, this time inaangalia ilipoishia na kuteua jina na baada ya hapo wanapeleka CDM kwaajili ya kuridhia kama mteuliwa bado ni mwanachama halali na hajapoteza sifa. Sasa inashangaza kuona watu mnaibuka na kuropoka tu.
 
Kuna watu wanajaribu kutwanga maji kinuni. Kuwaelewesha watu juu ya utatatibu wa kupata replacements wa viti naalym wakati watu aameshajitungia utaratibu vichwani mwao ni an exercise in futility!
 
mtoa hoja anaonyesha anajua mchakato wote wa namna ya kumpata mgombea wa viti maalum ila yeye anataka kujua historia ya maisha ya bunge wetu mtarajiwa wa viti maalum baada ya regia mtema
 
jamani tusibadili mada mbona swali liko wazi tu linahusu CV ya mrithi wa regia sio namna ya kumpata mrithi wa regia
 
Kuna watu wanajaribu kutwanga maji kinuni. Kuwaelewesha watu juu ya utatatibu wa kupata replacements wa viti naalym wakati watu aameshajitungia utaratibu vichwani mwao ni an exercise in futility!
u mean

Viti Maalumu vya Wabunge Wanawake
[TABLE="align: right"]
[TR]
[TD]
rally5.jpg
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Kulingana na Ibara Na. 66 na 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Vyama vya Siasa vitapendekeza kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi majina ya wanawake ambao Tume inaweza kuwatangaza kuwa Wabunge kama ikiridhika kwamba wana sifa zinazostahili.
Tume inatakiwa kutangaza majina ya wanawake kwa idadi isiyopungua asilimia 30 ya Wabunge wote kwa ajili ya viti maalumu kwa wanawake. Mgawanyo huo utazingatia uwiano wa kura ambazo kila chama kimepata katika uchaguzi wa Bunge. Endapo mgombea ubunge amepita bila kupingwa, kura za mgombea Urais wa chama cha mbunge zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge huyo. Kama hakina mgombea Urais, asilimia 51 ya idadi ya wapiga kura walioandikishwa zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge wa chama husika. Hata hivyo, chama kinaweza kupata nafasi ya viti maalumu cha mbunge mwanamke endapo kimepata 5% ya kura zote halali za uchaguzi wa wabunge.
Ili kutekeleza hilo hapo juu, Vyama vya Siasa vina wajibu wa:

  1. Kupendekeza majina ya wanawake kwa idadi itakayopendekezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulingana na Ibara ya 66(1b) na Ibara ya 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 kwa mpangilio wa upendeleo (preference) na kuituma Tume siku 30 kabla ya Uchaguzi.
  2. Kuhakikisha kwamba wanaopendekezwa wanajaza Fomu za Uteuzi
Dokezo: Kujaza Fomu za Uteuzi

Wanawake watakaopendekezwa hawatakiwi kuweka dhamana ya shilingi Elfu Hamsini (50,000/=).
Viti Maalumu vya Madiwani Wanawake
Viti maalumu kwa upande wa madiwani, vinapatikana kutoka kwa kila chama kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya viti ambavyo kila chama kimepata katika uchaguzi wa Madiwani katika Halmashauri ya Jiji, Manispaa, Mji na Wilaya.
Viti hivyo ni theluthi moja ya jumla ya madiwani wa kuchaguliwa na wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi katika eneo husika.
Ili kutekeleza hayo:


  1. Vyama vipendekeze majina ya wanawake ambao watakuwa ni theluthi moja ya jumla ya madiwani wote wanaowakilisha kata na wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi. Orodha ya majina hayo ipelekwe siku 30 kabla ya siku ya upigaji kura.
  2. Vyama vya Siasa vihakikishe kwamba vinapendekeza wanawake wenye sifa za kuwa Madiwani
  3. Wanawake wa viti maalumu vya Madiwani wanaopendekezwa na vyama vya Siasa wanajaza Fomu za Uteuzi
  4. Wanawake hawatakiwi kuweka dhamana ya Shilingi Elfu tano (5,000/=).
 
Nadhani tukisema CV wote tunajua kuwa ni record ya mtu au historia yake katika maisha yake,sasa kwa huyu ambaye anaenda kuwa kiongozi naamini tulitakiwa kupata historia yake ya shule/elimu,uzoefu alionao/kazi,uwezo wa kiuongozi kwa maana ya uzoefu na kwa kuwa huyu ni mwanasiasa naamini tungependa kujua zaidi kuhusu maisha yake ya kijamii kwa maana ya mahusiano yake na watu wanaomzunguka.

nasikitika kuna wanaojitahidi kuchafua hali ya hewa hapa wakati hii ni Great thinker's Forum, au tumezoea huko kwenye facebook ambapo unaweka picha yako na kubadilisha kila baada ya nusu saa unasubiri comments.........................................................................................
 
u mean

Viti Maalumu vya Wabunge Wanawake
[TABLE="align: right"]
[TR]
[TD]
rally5.jpg

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Kulingana na Ibara Na. 66 na 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Vyama vya Siasa vitapendekeza kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi majina ya wanawake ambao Tume inaweza kuwatangaza kuwa Wabunge kama ikiridhika kwamba wana sifa zinazostahili.
Tume inatakiwa kutangaza majina ya wanawake kwa idadi isiyopungua asilimia 30 ya Wabunge wote kwa ajili ya viti maalumu kwa wanawake. Mgawanyo huo utazingatia uwiano wa kura ambazo kila chama kimepata katika uchaguzi wa Bunge. Endapo mgombea ubunge amepita bila kupingwa, kura za mgombea Urais wa chama cha mbunge zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge huyo. Kama hakina mgombea Urais, asilimia 51 ya idadi ya wapiga kura walioandikishwa zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge wa chama husika. Hata hivyo, chama kinaweza kupata nafasi ya viti maalumu cha mbunge mwanamke endapo kimepata 5% ya kura zote halali za uchaguzi wa wabunge.
Ili kutekeleza hilo hapo juu, Vyama vya Siasa vina wajibu wa:
  1. Kupendekeza majina ya wanawake kwa idadi itakayopendekezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulingana na Ibara ya 66(1b) na Ibara ya 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 kwa mpangilio wa upendeleo (preference) na kuituma Tume siku 30 kabla ya Uchaguzi.
  2. Kuhakikisha kwamba wanaopendekezwa wanajaza Fomu za Uteuzi
Dokezo: Kujaza Fomu za Uteuzi

Wanawake watakaopendekezwa hawatakiwi kuweka dhamana ya shilingi Elfu Hamsini (50,000/=).
Viti Maalumu vya Madiwani Wanawake
Viti maalumu kwa upande wa madiwani, vinapatikana kutoka kwa kila chama kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya viti ambavyo kila chama kimepata katika uchaguzi wa Madiwani katika Halmashauri ya Jiji, Manispaa, Mji na Wilaya.
Viti hivyo ni theluthi moja ya jumla ya madiwani wa kuchaguliwa na wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi katika eneo husika.
Ili kutekeleza hayo:

  1. Vyama vipendekeze majina ya wanawake ambao watakuwa ni theluthi moja ya jumla ya madiwani wote wanaowakilisha kata na wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi. Orodha ya majina hayo ipelekwe siku 30 kabla ya siku ya upigaji kura.
  2. Vyama vya Siasa vihakikishe kwamba vinapendekeza wanawake wenye sifa za kuwa Madiwani
  3. Wanawake wa viti maalumu vya Madiwani wanaopendekezwa na vyama vya Siasa wanajaza Fomu za Uteuzi
  4. Wanawake hawatakiwi kuweka dhamana ya Shilingi Elfu tano (5,000/=).

Mkuu tunaomba CV ya Cecilia PERASO,kamanda mpya sio taratibu za kumpata mbunge wa viti maalum.
 
dk slaa atakuwa ana cv yake coz alipokuwa mbunge wa krt kpnd kile alikuwa akiishi pale kwao,dingi yake na cecilia ni swahiba a dr slaa!wenye cv yake atupe!

Duh ..kama ni kweli full kujuana as usual CDM

Na kuna watu wanadai tume ndio imechagua ... Je hayo majina kabla hayajafika tume yalitokea wapi ?
 
Hapa ndipo CDM walipokosea....ingebidi mrithi wake atoke angalau Morogoro. Hawajawatendea kabisa haki wale vijana wote waliotumia nguvu zao siku ya msiba wa Regia kule Ifakara.

Naona sasa hoja una ila unatekeleza hii falsafa yako ya kitumbafu kwamba.........
If you can't convince them, confuse them.
 
Hongera yake, na amini baada ya msitari jina lililofuatia ni la Cecilia si U kaskazini eti. Mie nampa hongera yake na akafanye kazi nzuri ya kumuenzi kipenzi chetu Rejia.
 
Magamba hakika ni wagumu kuelewa na wepesi kusahau!!! Hivi unajisikiaje kueneza uongo ilhali nafsini mwako ukweli unaujua? Unaenda msikitini/kanisani kufanya nini? Uteuzi wake Bi. Cecilia Paresso mbona ushafafanuliwa kwa kina humu JF? Regia alikuwa namba 25, Cecilia alikuwa namba 27, yule namba 26 alihama chama, sasa unataka nini? Ulitaka mama yako awekwe namba 26 kwenye list iliyopelekwa NEC na CDM mwaka juzi?
 
Nafasi hii kapewa naye Dr aingize wake baada ya mkewe.

Kwani Mh Ndesamburo amepewa nafasi ya Mtoto na Mkwe.
Mh mgombea urais wa Znz kupitia Chadema ametoa mtoto wa Dada yake.
Tindu lisu ametoa dada yake.
Padre Slaa ametoa mke na labda huyu mrithi wa Regia.

Mh Alfi -- hajapewa
Mh Zitto -- hajapewa.

Je kunani hapo? Dini au shares hazikutosha kwa Zitto na Alfi kupewa nafasi nao waweke wao?

ndio maaana tunasema viti maalum ni unafiki mtupu na upendeleo na ikhsani na fitna kubwa kwa jamii. mfikirie kuviondoa.
We kilaza, kule kwenye uzi wa A.Tibaijuka ajiuzulu umeweka unafiki kuwa unasimamia sheria inasemaje! Sasa hapa tuambie sheria inasemaje inapotokea mbunge wa viti maalum amefariki, nafasi yake inajazwa vipi?! Nilishakwambia hata shaitwani anakushangaa kwa unafiki na chuki zako.
 
sheria za uchaguzi na uteuzi wa wabunge wa viti maalum unazifahamu? waombe wajf hapa watakupa nadhani utaridhika. Kwa kifupi tume ya uchaguzi ndiyo inapendekeza jina , linapelekwa ktk chama husika kupewa baraka.

Mkubwa tupe elimu maana wengine huwa tunadandia gari kwa mbele tena mlimani!!
 
Magamba mbona wepesi wa kusahau nyie? Amina chifupa alipofariki mbona alilithiwa na Getrude Lwakatare? acheni uchonganishi na utoto nyie watu
 
kama ni kweli nasikitika sana,CHADEMA hawakupaswa kuteua mtu kutoka karatu...kisiasa inapunguza credit zao.wana jamii sometimes tuwe fair hata kama tunaipenda chadema lakini kwa mambo ambayo yatatoa picha mbaya kwa wananchi tunapaswa kuepuka.Sitaki kuamini kuwa hakuna mtanzania mwingine kutoka sehemu nyingine mwenye sifa za kushika hii nafasi..naomba viongozi wa chadema tuwe makini kwenye maamuzi
 
Back
Top Bottom