Suala la Mrema kama linavyoreportiwa ni suala kubwa sana na halipaswi kuchukuliwa kiushabiki wa kumshabikia Magufuli tuu kama inavyoonekana hapa. Nimesoma tuhuma za Mrema magazetini hazitofautiani sana na zile za mafisadi papa. Lakini ninavyofahamu mimi issue ya Mrema haitofautiani sana na ile ya Late Gavana wa Benki Kuu Tanzania. Kama magufuli anania ya kweli katika issue ya Mrema na si kuweka watu wake ili aweze kuendelea na mambo tunayoyafahamu basi alipaswa apate maelezo ya Mrema juu ya tuhuma hizo na ikibidi amshitaki na sio kumfukuza kazi tuu. Kinachoendelea TANROADS na Wizara ni struggle of power na sio ufisadi wa Mrema kwani ufisadi wote unatokea Wizarani na sio kwa Mrema yeye ni mtekelezaji tuuu. Natoa rai kwa wale waandishi wa habari za kiutafiti kulifanyia kazi na waujuze Umma wa Kitanzania unaopotoshwa kila kukicha na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi.
Hivi Lowassa na Pombe hawapo "kambi" moja?
wapo wwengine kama wawili hivi.....namuomba pombe awatoe
I don't understand this; kwani Kawambwa alishindwa na kitu gani au Magufuli kaja na nguvu gani nje ya zile ambazo Kawambwa alikuwa nazo; this just make Kawambwa aonekane vibaya. Haiwezekeni watu wamsubiri Magufuli. Msije kuniambia kuwa hata ATCL sasa imepata kiongozi?
Sijui kama wanajamvi kuna kitu tunajifunza hapa sijasikia hoja ya uonevu au kaondolewa kwasababu ya dini yake ?.Ngoja mtendaji mkuu wa NSSF aguswe utasikia hana kosa anaonewa kwasababu ni .......ebo wakati mwingine tunatakiwa kukua kidogo mtu akikosa asitetewe kwa vigezo vya dini au kabila lake.
Sio swala la kupumbaza watu kusherehekea hilo!! maana wote wezi hao, wanajipanga nyie mnashangilia nini? Magufuli silolote si Chochote hajarudisha nyumba alizouza anatoa beki anaweka beki nyie mnashangilia kuweni makini Jamani maana hata huyo Mrema yawezekana katolewa kwasababu Mchaga