Ref my previous post
Namshukuru mwenyezi Mungu muumba wq mbingu na ardhi kwa pumzi na afya njema aliyonijaalia
ilinichukua miaka mitano na nusu kuacha kazi ya serikalini nashukuru Mungu kwa walionisupport juu ya uamuzi wangu huo
nliwakwepa wale wote ambao nlihic watanikatisha tamaa hasa wazazi wangu ilibidi nimtengenezee mazingira ya kutokuniomba hela ya kila mwezi kwa kumwekea pooltable linalomwingizia 150000 kila mwezi
Ninachofanya baada ya kuacha kazi
Ninalima matikiti maji,Zukini na pilipili za kuwasha nimeanza na tikiti maji heka 3 pilipili za kuwasha nusu heka na zukini nusu heka
Zukini na pilipili ndo zao ninalolitegemea kulifanya liwe zao la biashara nimelilima chache kwasababu ckuwahi kulima zukini na pilipili so natafuta experience
tikiti ziko poa ntawaonyesha picha za zilipofikia
Biashara
nimefanya biashara ya mbolea ya mavi ya kuku kwa muda wa week 2 nimeingiza faida ya laki4 though changamoto imekuja kwenye savings kila nkipata hela mahitaji ya shamba yanaongezeka mf dawa mbolea ya dukani kuwalipa posho vibarua nk
Uzuri wa kujiajiri
unaamua ufanye nini muda gani mwenyewe yaani kama nkiamua nisafiri hata nw naweka mipango sawa naenda popote inshort nipo huru
changamoto kuubwa nliyoiona
Savings na mifuko ya jamii
faida inapaswa ihifadhiwe kiac kikubwa kuliko kukitumia mara nyngi tunatumia hela pale tunapokua nazo tusipokua nazo ni ngumu sana kuzitumia natamani nijifunze mbinu ya kisave
natamani nijiunge na ule mfuko binafsi wa penshen tatizo huku Jaribu(kibiti) hakuna hicho kitu
View attachment 848013View attachment 848015View attachment 848016
Sent using
Jamii Forums mobile app